Waandishi Wetu, Dodoma na Dar Lile ‘saga’ la kigogo, Michael Karoli Wage (60), anayelalamika kuombwa ‘mlungula’ wa shilingi milioni 10 na Mtangazaji ‘the big name’ wa Shirika la Utanzazaji Tanzania (TBC), Jerry Muro, sasa kibao kimemgeukia ‘mkubwa’ huyo, Risasi Jumamosi limetonywa...
Na Hemed Kisanda Siku chache baada ya Miss Tanzania 2010, Wema Sepetu kuhamishia penzi lake kwa mwanamuziki wa Bendi ya African Star ‘Twanga Pepeta International’, Charles Gabriel a.k.a Chalz Baba, kumeibuka minong’ono mingi kutoka kila pembe ya jiji la Dar es Salaam, ikitaka kujua kama kweli Chalz Baba ataweza kuhimili vituko vya mlimbwende huyo baada ya Yusuf Jumbe kushindwa...
Na Hemed Kisanda Nyota wa muziki wa Bongo Fleva Lawrence Malima a.k.a Marlaw amewaomba radhi wakazi wa mkoa wa Mwanza ‘Rocky City’ kwa kitendo chake cha kufanya shoo kiduchu wakati wa tamasha moja la muziki lililofanyika miezi michache iliyopita mjini humo na kuwaacha mashabiki wake wakiwa bado na hamu naye...
Kigali, Rwanda WASANII Pfla, Jay Polly, Green P, Bull Dogg na Fire Man wanaounda kundi mahiri la muziki wa Kizazi kipya pande za Kigali nchini Rwanda lijulikanalo kama Tuff Gung Bati wamedai kushangazwa na kitendo cha makundi ya muziki kama huo hapa Bongo yakivunjika kila kukicha huku kwao yanaibuka kwa kasi, ishu hii anakudondoshea Hemed Kisanda...
Na Hemed Kisanda GWIJI wa muziki wa Bongo Fleva, anayetamba hivi sasa na ngoma ya King and Queen, Ambwene Yesaya a.k.a A.Y amesema kuwa, anataka kwenda kinyume kidogo na hali iliyozoeleka hapa nchini katika mfumo wa msanii kuwa mtawaliwa katika shughuli zake...
ILIPOISHIA Lakini kuna kitu kilinipa moyo kutokana na pesa na misaada mingi niliyokuwa nampa laima atauona umuhimu wangu wa kuniacha niendelee na kazi. Vilevile hata kama ningekimbia bado nafasi ya kwenda nje kusona ningeikosa na muda ulikuwa umebaki mchache sana kuteua jina la mtu wa kwenda kusoma nje, nilisikia kuna mtoto wa mkubwa ndio kaandaliwa. Nilijikuta nikipoteza woga wote na kuwa tayari kwa lolote ili mradi nafasi ile niipate... Sasa endelea...
Mungu aliyemuumba Adam na Hawa ndiye huyo huyo aliyetufanya mimi wewe tuwepo kwenye sayari hii ya dunia. Ni mwema kwa kila kitu, hivyo tumshukuru na kumhimidi kwa sababu anaendelea kuweza...
ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA “Lakini wengi waliokuwepo ni wageni hawakuji pia kutokana na kauli yako ilionesha sisi ni wapenzi wa muda mrefu.” “Mmh basi, sina jinsi maji yameisha mwagika.” “Jamani huku nyuma kuna kesi gani tena?” Faudhia aliyekuwa siti ya mbele aliuliza. SASA ENDELEA...
Justine na Austine ni watoto mapacha waliozaliwa na mama mmoja porini, ambaye aliwaacha na kutambaa hadi barabarani ambako aliokotwa akiwa taaban sababu ya kuvuja damu nyingi, akakimbizwa hospitali ambako baadaye alikufa bila mtu kufahamu kwamba kabla ya kufika barabarani alizaa watoto wawili mapacha sehemu tofauti. Austine akaokotwa na mwanamke wa Kimasai, akakulia kwenye familia ya wamasai mpaka mwanamke huyo alipofariki ndiko akachukuliwa na padri ambaye alimsomesha hatimaye naye akawa Padri mwenye ndoto ya kuwa Papa wa kwanza mweusi!
Akiwa Vatican kwa masomo, padri aliyemsomesha Austine akafariki na kumwachia simanzi kubwa lililomfanya apoteze ndoto yake ya kuwa Papa, akatoroka Vatican ambako anatafutwa! Alipofika kwenye uwanja wa ndege wa Schiphol, Amsterdam, akiwa njiani kuelekea Tanzania anakamatwa kwa tuhuma za mauaji ya watu watatu, jambo ambalo anaamini hakuwahi kulifanya na anasafirishwa kuja Tanzania kujibu tuhuma zake.
Upande wa pili Justine aliokotwa na familia ya Wamarekani (Bwana na bibi Lawrence Green) ambao walipoondoka Tanzania walirejea Marekani huko North Carolina, wakamlea Justine na kumsomesha, hatimaye akawa mchezaji maarufu wa mpira wa kikapu nchini humo na kutajirika kabisa! Cha kusikitisha, Justine hajui ukweli wa historia yake, amefichwa na anaowajua kwamba ni wazazi wake kwa muda mrefu.
Amekutana na msichana aitwaye Nancy kwenye chuo kikuu cha North Carolina, aliporejea kwa mapumziko kutoka Los Angeles ambako amehamia na kujiunga na timu ya Lakers akitokea San Antonio Hot Spurs. Msichana huyo amemchanganya kabisa, ametumia kila mbinu mpaka amefanikiwa kumwalika Los Angeles, anampenda mno lakini ameshindwa kumweleza ukweli sababu alionywa asimwendee kwa pupa, ni msichana mgumu kupatikana.
Kwa tamaa zake anaamua kumchungulia Nancy kupitia dirishani usiku akiwa wamelala, bila kujua kuwa msichana huyo hakuwa usingizini, yeye pia alikuwa akiteseka sana kwa mapenzi aliyokuwa nayo kwa Justine lakini alishindwa kusema. Nancy alipomwona Justine akimchungulia dirishani, aliamka kitandani na kuvua nguo zote kisha kulala chali akiwa ameelekeza mwili wake dirishani. Hali hiyo ilimchanganya kabisa Justine na kujikuta akiamua kwenda kumgongea. Je, nini kilitokea? SONGA NAYO…
Dakika chache kabla ya Karandinga kung’oka na Jerry Moro katika Mahakama ya Kisutu kuelekea Segerea kuanza Maisha mapya juhudi za ndugu na jamaa wa mshtakiwa huyo zimeweza kuzaa matunda ya kupata dhamana na jamaa kurudi uraiani.
Jerry Muro akitolewa mahabusu na maafande wa magareza ambao tayari walishampokea kutoka Jeshi la Polisi.
Jerry Muro (katikati) akionesha tabasamu baada ya kuwekewa dhamana.
Vanessa Perroncel ‘aliyeasisi’ kashfa hiyo dhidi ya Terry.
KOCHA mkuu wa timu ya soka ya England, Fabio Capello, atakutana na nahodha wa timu hiyo, John Terry, ambaye anadaiwa kuwa na uhusiano wa mapenzi na mwanamke ambaye hufanya kazi ya kutangaza mitindo ya nguo za ndani (chupi) katika kampuni moja nchini humo...
Jerry Muro akirudishwa rumande mchana huu baada ya kukosa dhamana ambapo mpaka tunaelekea mitamboni juhudi za kumnasua asiende kulala Segerea zilikuwa zikiendelea.
Mapaparazi wakifuatilia tukio la Jerry kufikishwa mahakanani leo mchana.
Na Dkt. Masangu Matondo Nzuzullima (USA) Profesa Mbele, amekuwa akisema mara kwa mara kwamba Watanzania tunapenda sana kuponda raha. Tunachangishana mabilioni ya shilingi ili kufanya harusi za kifahari lakini hatuwezi kuchangishana ili kujenga shule au kununua madawati kwa ajili ya watoto wetu wanaosomea chini; au kuchimba visima vya maji vijijini tulikotoka. Tunasema hii ni kazi ya serikali...
MWANDISHI wa habari wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Jerry Muro, amepandishwa kizimbani na wenzake wawili ambao ni Deogratius Mgassa (35) na Edmund Kapama (52) ambapo wamesomewa mashitaka matatu yafuatayo:
Kukusudia kuomba rushwa, kula njama za kutenda kosa na kujifanya maafisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), kosa linalowahusu Kapama na Mgassa.
Hadi tunakwenda mitamboni, Kapama alikuwa amepewa dhamana, ambapo Muro na Mgassa walikuwa bado wakihangaikia suala hilo.
Katika kesi hiyo, Muro anawakilishwa na mawakili Pascal Kamala na Anney Semmu.