arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » Articles for 06.02.2010

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» JE, UNGEPENDA KUPATA RAFIKI ...
» MSHANGAO!
» Rais Kabila aomba wakafungw ...
» Waraka wa Papii watua kwa J ...
» Aunt Ezekiel alivyopigika k ...
» JERRY: NASAKWA NIUAWE!
» KIGOGO WA MURO NAYE KUKAMAT ...
» TANGU ENZI HIZO BADO NA ...
» Mambo ya Msondo
» ZANZIBAR INASIKITISHA
» MTIKILA MAHAKAMNI
» Nimerudi kutoka kuzimu- ...
» Binti kiziwi atoboa sir ...
» Using’ang’anie penzi li ...

 

Wito watolewa kufuta madeni yote ya Haiti

photos  
Wito watolewa kufuta madeni yote ya Haiti
Cephas Lumina

Mtaalamu wa kujitegemea wa Umoja wa Mataifa kuhusu madeni ya nje na haki za binadamu , Cephas Lumina ametoa wito wa kufutwa mara moja madeni ya Haiti inayodaiwa na wadeni mbalimbali na kuipa nchi hiyo fedha za msaada zisizo na masharti yoyote, na sio mkopo mpya...
    (6 February 2010)
Views: 84 | Maoni (4) | Soma Zaidi

 

Wito wa utulivu watolewa, ghasia zikiongezeka Ivory Coast

Habari mbalimbali  
Wito wa utulivu watolewa, ghasia zikiongezeka Ivory Coast
Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Ivory Coast umeshuhudia ghasia hivi karibuni kwenye miji ya Katiola na Divo, na umetoa wito wa kuwepo na hali ya utulivu wakati shughuli ya uandikishaji wapiga kura kuelekea uchaguzi mkuu ujao ikifanyika...
    (6 February 2010)
Views: 52 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

KUTOKA MOMBASA:MKEREKETWA AKOSOA VIONGOZI KWA KUBEZA KISWAHILI KENYA.

Habari mbalimbali  
KUTOKA MOMBASA:MKEREKETWA AKOSOA VIONGOZI KWA KUBEZA KISWAHILI KENYA.
Mkereketwa wa kiswahili nchini Kenya, Bw.Ludovick Mbogholi, alipokuwa akiongea na mwandishi wa Global nyumbani kwake jijini Mombasa .
Mwana Kiswahili huyu alizua sokomoko nchini Tanzania mwaka 1995 wakati alipochukuliwa na CCM kumfanyia kampeini Ben Mkapa kupitia tungo na mikutano ya hadhara mkoani Kilimanjaro. Kampeni zake zilisaidia CCM kuibuka na ushindi licha ya malalamiko ya upinzani. Hivi sasa amezua gumzo tena baada ya kuwakashifu viongozi wa Kenya kuwa wanabeza kiswahili.


Na KAZUNGU SAMUEL, MOMBASA
Mkereketwa wa lugha ya Kiswahili mwenye uasili wa taifa la Tanzania amewakosoa vikali viongozi na washika dau nchini Kenya kwa kuwa kikwazo katika juhudi za taifa hili kukifanya Kiswahili kuwa lugha ya taifa. Kwenye kikao na mwandishi wa habari hizi nyumbani kwake mtaani Bamburi kwenye viunga vya jiji la Mombasa , Bw Ludovick Mbogholi alisema kuwa viongozi wa Kenya ikiwemo wajumbe wameingiwa na kasumba ya kutukuza lugha ya kiingereza hivi kwamba wanapuuza kabisa Kiswahili. “Ikiwa hata viongozi wetu wanasimama mbele ya
    (6 February 2010)
Views: 109 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

FAO kusaidia mfumo rahisi wa umilikaji ardhi

Habari mbalimbali  
FAO kusaidia mfumo rahisi wa umilikaji ardhi
Serikali ya Finland na shirika la chakula duniani FAO wamekubaliana kuzisaidia nchi mbalimbali kuanzisha mfumo endelevu na ulio rahisi wa umilikaji ardhi , ili kuimarisha udhibiti wa ardhi katika maeneo ya vijijini na mijini...
    (6 February 2010)
Views: 45 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

Kampeni yazinduliwa Sudani kukabiliana na masuala ya uhamiaji

photos  
Kampeni yazinduliwa Sudani kukabiliana na masuala ya uhamiaji

Shirika la kimataifa linalohusika na masuala ya uhamiaji IOM limezindua kampeni ya utoaji taarifa nchini Sudan kuhusu athari zitokanazo na uhamiaji holela, kama sehemu ya juhudi za kupambana na matatizo ya uhamiaji Afrika ya Mashariki na pembe ya Afrika...
    (6 February 2010)
Views: 41 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

UNICEF: Ongezeko la ukeketaji latia hofu

Habari mbalimbali  
UNICEF: Ongezeko la ukeketaji latia hofu
UNICEF na Shirika la Afya Duniani WHO wameelezea wasiwasi juu ya kuongezeka kwa wahudumu wa afya wanaoendesha vitendo vya ukeketaji. Inakadiriwa kuwa wanawake milioni 120 hadi 140 wamekeketwa na wasichana milioni 3 bado wako kwenye hatari ya kukeketwa kila mwaka...
    (6 February 2010)
Views: 37 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

Serikali yatenga bilioni 19 kwa ajili ya wakulima

Habari mbalimbali  
Serikali yatenga bilioni 19 kwa ajili ya wakulima
Na Hemed Kisanda.
Serikali imeidhinisha kiasi cha sh. Bilioni 19 kwa ajili ya kutoa mikopo kwa wakulima kupitia benki ya rasilimali ya Tanzania TIB...
    (6 February 2010)
Views: 54 | Maoni (2) | Soma Zaidi

 

FRESH JUMBE, TWANGA WALIVYOIPAISHA BAHATI NASIBU YA SHINDA GARI

photos  
Usiku wa kuamkia leo, bendi kongwe ya muziki wa dansi nchini, The African Stars ‘Twanga Pepeta’ pamoja na mwanamuziki wa kibongo anayeishi nchini Japan, Fresh Jumbe walizikonga vilivyo nyoyo za wanazi wa burudani nchini, katika onesho lao ‘babkubwa’ lililofanyika ndani ya ukumbi wa Hoteli ya Landmark, Ubungo , jijini Dar es Salaam. Onesho hilo lilienda sambamba na Promosheni ya Bahati nasibu ya Shinda Gari aina ya Toyota Vitz na zawadi nyingine kibao kutoka kampuni ya Global Publishers Ltd, wachapishaji wa magazeti ya Ijumaa, Uwazi, Risasi, Amani, Championi, Ijumaa Wikienda na mtandao huu. Ilibamba si kitoto mtu wangu, hebu cheki mapicha haya...



FRESH JUMBE, TWANGA WALIVYOIPAISHA BAHATI NASIBU YA SHINDA GARI
Wasanii wa Twanga wakishambulia jukwaa.

FRESH JUMBE, TWANGA WALIVYOIPAISHA BAHATI NASIBU YA SHINDA GARI
Wanenguaji nao walikandamiza kinoma.

FRESH JUMBE, TWANGA WALIVYOIPAISHA BAHATI NASIBU YA SHINDA GARI
Haya ni manjonjo tu ya wanenguaji hao...
    (6 February 2010)
Views: 69 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

CCM YAADHIMISHA MIAKA 33

photos  
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, Dk. Jakaya Kikwete, leo aliwahutubia wananchi katika maadhimisho ya sherehe za miaka 33 ya chama hicho tangu kuzaliwa kwake zilizofanyika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Miongoni mwa mambo aliyosistiza kwa viongozi wa chama hicho ni utendaji bora, hasa wabunge na madiwani, kwani yeyote atakayeonesha udhaifu na kukataliwa na wananchi wake katika kampeni, chama chake hakitatumia mbinu yeyote kubadili fikra za wananchi hao.

CCM YAADHIMISHA MIAKA 33
Kabla ya kuanza kuhutubia, Rais JK aliwaomba wananchi wasimame kwa sekunde kadhaa kumkumbuka Hayati Rashid Mfaume Kawawa, aliyeaga dunia hivi karibuni.

CCM YAADHIMISHA MIAKA 33
Baadaye JK alianza kuhutubia

CCM YAADHIMISHA MIAKA 33
Sehemu ya wananchi waliohudhuria sherehe hizo

CCM YAADHIMISHA MIAKA 33
Kampteni John Komba (katikati) akitoa burudani kwa nyimbo za kwaya viwanjani hapo


PICHA: RICHARD BUKOS /GPL
    (6 February 2010)
Views: 36 | Maoni (1) |

 

Gazeti la Championi lapongezwa kwa kuandika habari makini.

photos  
Gazeti la Championi, linaloandika habari za michezo nchini, limepongezwa kwa kuwa miongoni mwa magazeti makini yanayoandika habari za uhakika na ambazo zimekuwa zikitoa mchango mkubwa katika maendeleo ya michezo nchini.

Pongezi hizo zilitolewa jana usiku na Kampuni ya bia ya Serengeti Lager katika hafla fupi ya kuukaribisha mwaka 2010 na kuwapongeza waandishi mbalimbali wa habari hapa nchini kwa kazi nzuri wanazozifanya.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo fupi alikuwa Mhe. Muhammed Seif Khatib, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Rais (Muungano). Katika sherehe hiyo iliyofanyika katika ndani ya ukumbi wa Msasani Beach Club, uliopo Mikocheni jinjini Dar es Salaam, kampuni hiyo ilitoa zawadi ya cheti kwa gazeti la Championi linalomilikiwa na Global Publishers Ltd kwa mchango wake mkubwa wa kuandika habari zilizomakini kwenye medani ya michezo.

Gazeti la Championi lapongezwa kwa kuandika habari makini.
Mhariri wa gazeti la Championi Jumatano, Denis Fusi (anaye anekana mgongo) akipeana mkono na Jaji Mstaafu Mark Bomani ambaye kwa sasa ni Mweyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Serengeti mara baada ya kukabidhiwa cheti na Waziri Khatib.

Gazeti la Championi lapongezwa kwa kuandika habari makini.
Msanii wa kundi la Wanne Star akionesha ufundi wake wa kucheza na moto.

Gazeti la Championi lapongezwa kwa kuandika habari makini.
Waziri Khatib akisakata muzik na Afisa Uhusiano wa kampuni ya Serengeti Lager, Teddy Mapunda.
    (6 February 2010)
Views: 29 | Maoni (0) |

 

KIMBUNGA CHA ZUA BALAA MORO MJINI!

photos  
Upepo mkali, uliosindikiza mvua kubwa iliyonyesha jana kuanzia mida ya saa nane na nusu mchana na kukadiriwa kudumu kwa muda wa saa moja, umesababisha hasara kubwa kwa baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Morogoro pamoja na Shirika la kuangaza maisha yetu, (Tanesco). Mvua, hiyo ambayo iliannza kama mvua nyingine, ilibadilika ghafla na kutishia baadhi ya wakazi wa Morogoro Mjini kwa kuonesha dalili kama za Kilosa (Mafuriko) ambayo baadae iliisha kabisa na jua kuchomoza utafikiri kulikuwa hakuna mvua. Lakini mara baada ya kukatika kwa mvua hiyo, kilichoshuhudiwa na mwandishi wetu ni uharibifu mkubwa wa magari, nyumba na nyaya za simu na umeme ambazo zilikatika baada ya kuangukiwa na miti mikubwa iliyongo'lewa kwa upepo. Athari nyingine iliyoonekana ni kuharibika kwa magari ambayo yaliangukiwa na kupondeka kabisa na barabara nyingi kuwa hazipitiki baada kuangukiwa na miti....ilikuwa ni kizaazaa cha aina yake...

KIMBUNGA CHA ZUA BALAA MORO MJINI!
..watu wakishangaa uharibifu uliosababishwa na mvua hiyo ya upepo.

KIMBUNGA CHA ZUA BALAA MORO MJINI!
....mitaa mingi iliathirika kwa kuangukiwa na miti

KIMBUNGA CHA ZUA BALAA MORO MJINI!
...iling'olewa hadi miti mikubwa kama unavyoonekana huu

KIMBUNGA CHA ZUA BALAA MORO MJINI!
...miti mingi iling'olewa na kuangukia barabarani

KIMBUNGA CHA ZUA BALAA MORO MJINI!
..gari haitamaniki baada ya kuangukiwa na mti

KIMBUNGA CHA ZUA BALAA MORO MJINI!
..askari wa usalama barabarani wakiangalia uharibifu huo

PICHA NA STORI: Prince Sab, Morogoro
    (6 February 2010)
Views: 25 | Maoni (0) |

 

FLYOVERS

photos  
FLYOVERS
Mh. Rais JK kishaagiza viongozi wa Manispaa za Dar kuangalia uwezekano wa kujenga barabara za juu kwa juu (Fly Overs) ili kupunguza msongamano wa magari. Siku moja jiji la Dar linaweza kuwa na sura kama hii?
    (6 February 2010)
Views: 126 | Maoni (9) |

 

ZIARA YA RAIS KIKWETE JIJINI DAR ES SALAAM

photos  
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete jana aliendelea na ziara yake ya kutembelea Mkoa wa Dar es Salaam.
Katika ziara hiyo, akiwa kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo Viwanja vya Sabasaba Temeke, aliongea na watendaji mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi wa Wilaya hiyo ambapo aliwasisitiza juu ya kujiletea maendeleo.

ZIARA YA RAIS KIKWETE JIJINI DAR ES SALAAM
Rais Kikwete akisalimiana na wenyeji wake mara baada ya kuwasili katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere.

ZIARA YA RAIS KIKWETE JIJINI DAR ES SALAAM
Rais akiongea na watendaji mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) waliofurika katika ukumbi huo.

ZIARA YA RAIS KIKWETE JIJINI DAR ES SALAAM
Baadhi ya watendaji wa CCM Wilaya ya Temeke, wakimpungia mikono Rais Kikwete mara baada ya kuingia ukumbini.

ZIARA YA RAIS KIKWETE JIJINI DAR ES SALAAM
Watendaji wa Wilaya ya Temeke, wakimsikiliza kwa makini Rais Kikwete alipokuwa akiwahutubia.

ZIARA YA RAIS KIKWETE JIJINI DAR ES SALAAM
Kundi la ngoma za asili la Chama Cha Mapinduzi wilayani Temeke, likitumbuiza baada ya Rais Jakaya Kikwete kuwasili katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere ambapo aliongea na watendaji wa wilaya hiyo.

Picha: Issa Mnally/GPL
    (6 February 2010)
Views: 21 | Maoni (0) |

 

Rada ya Tanzania yaigharimu BAE

Habari mbalimbali  
Rada ya Tanzania yaigharimu BAE
BAE Systems, mojawapo ya makampuni makubwa kabisa duniani ya uundaji wa vifaa vya kijeshi, itatozwa faini ya dola milioni 400...
    (6 February 2010)
Views: 274 | Maoni (3) | Soma Zaidi

 

FATAKI ASAKWA

risasi jumamosi  
FATAKI ASAKWA
Na Mwandishi Wetu
Goodluck Kimaro, yule kigogo mwenye skandali la ufataki, anasakwa na hivi sasa dawa yake ipo inachemka ndani ya Jeshi la Polisi, Risasi Jumamosi lina kitu kamili...
    (6 February 2010)
Views: 862 | Maoni (3) | Soma Zaidi
Back  <<  1 2  >>  Next Page
 

Kura Yako / Poll

Habari Katika Picha


Gazeti la Uwazi


Nani Yupo / Alikuwepo


Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

 hit counter

counters

2008 © globalpublisherstz.com