arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » Articles for 07.02.2010

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» JE, UNGEPENDA KUPATA RAFIKI ...
» JIDE HOI
» MSHANGAO!
» Rais Kabila aomba wakafungw ...
» HUKUMU YA BABU SEYA!
» Waraka wa Papii watua kwa J ...
» Aunt Ezekiel alivyopigika k ...
» From china with true lo ...
» Vifo vya mastaa 2009
» Umafia!
» Vifo vya wanafunzi Irin ...
» Ni Ghana na Misri fain ...
» sasatel KULETA MAPINDUZ ...
» Wamachinga warejea kwa ...

 

My Black Chapter -30

hadithi za Shigongo  
Maryjose anarejea nchini kutoka India akiitwa Sista Theresa na kukabidhiwa kituo cha watawa wa shirika la Mt. Francisca, watawa wasiotoka nje, kazi yao ikiwa ni kusali tu! Anajishughulisha sana na kazi ya kutoa misaada kwa jamii, hakuna anayemkumbuka lakini siku moja David na wafanyakazi wake walipokwenda kwenye ofisi yake kutoa msaada wa shilingi bilioni mbili zimsaidie, David aligundua kuwa sauti ya Sista Theresa ni ya Maryjose lakini sista alikana.

Baada ya kugundua kwamba alikuwa mbioni kugundulika kwa David, Sista Maryjose anaamua kujitokeza mwenyewe na kujisalimisha lakini kabla hajafanya hivyo anakwenda Ukumbi wa Mkutano Maelezo huko anaomba mkutano na waandishi wa habari ambao wanafika kumsubiri ili aje aseme wapate habari za kuandika kwenye magazeti yao.

Sista Maryjose anafika lakini cha kushangaza anaonekana kuwa chini ya ulinzi wa polisi anaketi kwenye kiti na kukohoa kidogo kisha kuanza kutoa historia ya maisha yake na kuwaomba watu wote msahama akiwemo David kwamba alijulikana kwa jina la Sista Theresa lakini ukweli yeye alikuwa sista Maryjose na ndiye aliyehusika na kuchomwa kwa gari ambako kulisababisha kifo cha Alice na David kuwa mpofu.

Akaendelea mbele huku akisoma karatasi iliyokuwepo mbele ya meza yake, huku baadhi ya watu wakibubujikwa na machozi. Jovina alishindwa kabisa kujizuia, macho yake yakaanza kulengwalengwa. Historia ya Sista Theresa ambaye sasa alikuwa Maryjose tena ilikuwa ya kusikitisha mno na iliwafanya watu wote kwenye ukumbi wa Mkutano Maelezo waingiwe na huruma, baadhi wakahisi alistahili kufanya alichokifanya.

Alipofika hapo akanyanyuka na kutamka maneno kwamba tayari alikuwa kuhukumiwa kwa makosa aliyoyatenda, polisi mmoja akazunguka kwa mbele kuchomoa pingu kiunoni mwake na kumfunga Maryjose na kumtembeza kwenda naye nje, ambako waandishi waliendelea kupiga picha za matukio akapandishwa kwenye gari kisha kuondoka kwa kasi ya ajabu.

Je, nini kitaendelea huko anakopelekwa? Sista Maryjose atanyongwa? Je, taarifa hizi zimemfikia David? SONGA NAYO…
    (7 February 2010)
Views: 675 | Maoni (9) | Soma Zaidi

 

WALEVI WASHINDWA KUFANYA 'SHOPPING'

Videos  
Bonyeza PLAY uwashuhudie walevi hawa wawili waliokwenda 'Supermarket' kufanya manunuzi lakini kilevi kikawazidia na kuamua kuuchapa usingizi ndani ya 'Supermarket' hiyo!
    (7 February 2010)
Views: 13 | Maoni (0) |

 

WANAFUNZI WA KIGENI KUPUNGUZWA UINGEREZA

Habari mbalimbali  

WANAFUNZI WA KIGENI KUPUNGUZWA UINGEREZA
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uingereza, Alan Johnson.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uingereza, Alan Johnson, amesema kuwa serikali itapunguza idadi ya hati za kuingilia nchini humo au visa kwa wanafunzi wa kigeni ikiwa ni hatua inayolenga kukomesha utumiaji vibaya wa mfumo huo...
    (7 February 2010)
Views: 511 | Maoni (3) | Soma Zaidi

 

NANI ZAIDI KATIKA SOKA? FAINALI NI KESHO!

champion  
NANI ZAIDI KATIKA SOKA? FAINALI NI KESHO!

BAADA ya kuona matokeo ya juma lililopita kati ya makipa, Juma Kaseja wa Simba na Obren Curkovic wa Yanga, leo katika safu hii ya nani zaidi, tunakuletea washambuliaji wawili wa klabu hizo. Washambuliaji hao ni Mussa Hassan Mgosi wa Simba na Mrisho Ngassa wa Yanga, kwa ufupi ni kwamba wachezaji hawa wote wanacheza katika timu ya taifa ya Tanzania, (Taifa Stars), inayonolewa na Kocha Marcio Maximo raia wa Brazil. Katika msimamo wa wafungaji wa Ligi Kuu ya Vodacom, wanapishana kwa mabao mawili, ambapo Mgosi anaongoza akiwa na mabao 11 huku Ngassa naye akiwa amezifumania nyavu mara mara 9. Anza kupiga kura yako sasa kwenye sehemu ya kura kulia mwa page hii au toa coments zako hapa
    (7 February 2010)
Views: 483 | Maoni (46) |

 

WIKIENDI YA MUZIKI ILIVYOKUWA DAR

photos  
KATIKA kuwafahamisha wateja wetu shamra za wikiendi zilivyokuwa jijini Dar es Salaam, kamera yetu ilivinjari sehemu kadhaa ambako wakazi wake walikuwa wakimalizia wikiendi kwa burudani ya muziki. Ungana na kamera yetu:

WIKIENDI YA MUZIKI ILIVYOKUWA DAR
Wanenguaji wa bendi ya African Stars (Twanga Pepeta) wakiongozwa na mwimbaji Chalz Baba wakiserebuka katika onyesho la bendi hiyo lililofanyika jana usiku katika ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni.

WIKIENDI YA MUZIKI ILIVYOKUWA DAR
Kijana anayedaiwa kujihusisha na ushoga ambaye anajulikana kama 'Shoga Mtoto' akiwa amelivamia jukwaa na kunengua katika onyesho la bendi ya African Stars (Twanga Pepeta).

WIKIENDI YA MUZIKI ILIVYOKUWA DAR
Mtoto aliyejitambulisha kwa jina la Saidi Mhando akiwa anacheza nyimbo za Michael Jackson katika viwanja vya Leaders kuwaburudisha waliofika hapo.

WIKIENDI YA MUZIKI ILIVYOKUWA DAR
Mwanamuziki wa bendi ya Diamond Musica, Allain Kashama Mulumba, akiimba wimbo wa ‘Alowela’ katika Viwanja vya Leaders ambako wasanii mbalimbali hukutana kila siku za Jumamosi.

(Picha na Issa Mnally /GPL)
    (7 February 2010)
Views: 63 | Maoni (1) |

 

RAIS ZUMA AOMBA RADHI

Habari mbalimbali  

RAIS ZUMA AOMBA RADHI
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma

Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ameomba radhi kwa kitendo chake cha kujipatia mtoto kinyume na taratibu baada ya wananchi kulalamika...
    (7 February 2010)
Views: 451 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

Tu Kama Ng'ombe Kipofu Na Ng'ombe Aliyevunjika Mguu!

Habari mbalimbali  
Tu Kama Ng'ombe Kipofu Na Ng'ombe Aliyevunjika Mguu!
Na Maggid Mjengwa

Ndugu zangu Wahehe wana msemo; Isenga imbofu na isenga indenyoofu. Kwamba ng’ombe kipofu ni sawa tu na ng’ombe aliyevunjika mguu, wote watakufa njaa. Ng’ombe kipofu hawezi kuyaona majani, na yule aliyevunjika mguu hawezi kujikokota kwenda kutafuta nyasi za kula. Tafakuri yangu iliyopita nilimalizia kwa kuuliza swali: Je, unafikiaje uamuzi wa ama kuingia vitani, au la? Huu ni mwendelezo wa nilipoishia. Naam. Tunavyoendenda kama jamii wakati mwingine ni sawa na ng’ombe kipofu na yule aliyevunjika mguu. Unaweza kuliona hilo nyumbani kwako, katika ukoo wako na hata mahala pako pa kazi. Tumekuwa jamii ya ovyo ovyo. Tunafanya mambo ya ovyo ovyo. Ni kutoka ngazi ya familia na hata ngazi ya kitaifa.

Ona migongano ya wanasiasa wetu sasa. Ona wanavyogawanyika katika makundi yao. Hawatangulizi hata kidogo maslahi ya wengi. Wanajigawa kwenye
    (7 February 2010)
Views: 117 | Maoni (1) | Soma Zaidi
 

Kura Yako / Poll

Habari Katika Picha


Gazeti la Uwazi


Nani Yupo / Alikuwepo


Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

 hit counter

counters

2008 © globalpublisherstz.com