Baada ya kuchoma gari la bwana na bibi harusi na kujificha kwenye Jumba la Watawa kwa muda mrefu, ikiaminika kuwa alishakufa, hatimaye Maryjose ambaye hivi sasa anaitwa Sista Theresa, amejitokeza na kueleza kila kitu alichokifanya mpaka kuchoma moto gari na Alice (bibi harusi) kufariki dunia huku mume wake (David) akipata upofu wa maisha. Ni habari ya kusikitisha sana.
Yote hayo ni sababu ya mapenzi, pale Maryjose alipowekeza utajiri wake wa urithi kwenye matibabu ya David aliyekuwa na Kansa ya Uboho wa Mifupa, lakini alipopata nafuu na kupona akamwacha Maryjose na kumchukua rafiki yake Alice. Jambo hili lilimuumiza sana Maryjose na kuamua kulipa kisasi kisha kujiunga na Utawa ili ajifiche na kweli akafanikiwa kulifanya jambo hilo.
Sasa amejitokeza na baada ya maelezo yake anakamatwa na kupelekwa mahabusu, siku iliyofuata vyombo vyote vya habari vilikuwa vimeandika habari yake na ilitangazwa kwenye televisheni na redio, ikamfikia David na kuthibitisha alichokuwa amekifikiria. Baadaye wazazi wa Alice, mama yake mzazi walikuja ofisini kwake kumfariji na kumtaka amsamehe Maryjose kwa sababu alishaomba msamaha.
Akawawekea sharti moja; kama wanataka amsamehe basi wampeleke mahabusu akaongee naye, baada ya hapo ndiyo angeweza kutoa msamaha! Wakakubali bila kuelewa kuwa, David ameficha bastola yake kiunoni, hukaa nayo ofisini kwake kwenye droo kwa ajili ya kujilinda. Je, nini kitatokea? SONGA NAYO...
Ndege iliyopata ajali baada ya kuanza kushughulikiwa.
Ndege ya BA ikiwa imeharibika baada ya kuanguka.
BARAFU iliyokuwa imeganda na kuziba njia za kupeleka mafuta kwenye injini ndiyo sababu ya kuanguka kwa ndege ya shirika la British Airways (BA) la Uingereza miaka miwili iliyopita, imesema Idara ya Upelelezi wa Ajali za Angani ya Uingereza (AAIB) katika ripoti yake ya mwisho kuhusiana na ajali hiyo iliyotokea tarehe 17 Januari, 2008...
JENGO refu zaidi duniani (ghorofa) ambalo lilifunguliwa kwa mbwembwe mwezi mmoja uliopita nchini Dubai, limefungwa ghafla, jambo ambalo limewafadhaisha watalii waliokuwa wanapenda kwenda kwenye sehemu yake ya juu zaidi na kuangalia mandhari iliyo chini. Vilevile kitendo hicho kimeleta mashaka iwapo wapangaji wa kudumu katika jengo hilo wanaweza kuwa wamehamia humo katika majuma kadhaa yajayo.
Matatizo ya umeme yanaweza kuwa baadhi ya sababu za kufungwa kwa sehemu hiyo ya juu ya jengo hilo linaloitwa Burj Khalifa ambalo urefu wake kwenda juu ni nusu maili, urefu ambao ni sawa na sehemu ya (0.8) ya kilomita. Kutokuweko kwa habari yoyote kutoka kwa mmiliki wa jengo hilo kumefanywa kufungwa kwake kuache mashaka mengi kuhusiana na jengo hilo ambalo sehemu kubwa haina wapangaji.
Tanzania: Radio main source of news A survey has revealed that 66 percent of Tanzanians rely on radio as their main source of news. The research which was in the form of SMS raffle was intended to establish the main source of news for members of the public and also popularize the Journalists of the Year Awards in Tanzania, which were held December 19, 2009. According to the government owned Daily News despite having over 650 registered publications, the survey showed that only 14 percent of respondents preferred newspapers as source of news. “The poll actually shocked us,
Kutana na Immaculate Mosha, msichana mwenye kipaji aliyeoongoza nchi nzima katika matokea ya mitihani ya kidato cha Nne 2009. Video kwa hisani ya Varsity College Tanzania.
Kichwa cha habari cha News Of The World, gazeti lillofichua kashfa hii
Watoto watano wakiuzwa wote kwa dola 30,000.
Guerson, mtumishi wa kituo cha kulelea watoto aliyefichuliwa na waandishi akiuza watoto.
YATIMA mdogo aitwaye, Roudy, aliyejikuta katika hali hiyo kutokana na kupoteza wazazi wake katika tetemeko la ardhi lililoikumba nchi ya Haiti, anaitazama kamera ya waandishi wa habari bila wasiwasi wakati akiuzwa kwa wageni kwa bei ya Paundi 65. Anauzwa na mtu mmoja mwenye tamaa ya fedha ambaye ni kiongozi wa chama kinachotakiwa kuwasaidia watoto wa Haiti waliokumbwa na tatizo hilo na kubakia yatima...
Aliyekuwa rais wa Marekani Jimmy Carter amewasili nchini Sudan kwa mashauriano na rais wa nchi hiyo, Omar al-Bashir na maafisa wengine wakuu serikalini...
HUJUMA ZAIBUKA KIWANDA CHA PARETO MAFINGA .chadaiwa kukwepa kodi mamilioni ya shilingi .Vigogo wa serikali wahusishwa (ONLINE VERSION)
Kiwanda cha Pareto Mafinga
Na Rashid Mkwinda, Mufindi HUJUMA na ubadhirifu vimeibuka katika kiwanda cha kampuni ya Pareto (Pyrethrum Company of Tanzania (PCT) chenye makao yake makuu mjini Mafinga, Mufindi mkoani Iringa baada ya rasilimali za kiwanda hicho zenye thamani ya mamilioni ya fedha kuuzwa kiholela huku mwekezaji chini ya usimamizi wa Meneja Mkuu raia wa Uganda Bw. Martin Oweka, akidaiwa kuhusika. Taarifa zinaeleza kuwa, kiwanda hicho ambacho kiliwekwa jiwe la msingi na aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Sokoine Agosti 19, 1977, kilianza rasmi uzalishaji wake mwaka 1984 chini ya serikali ya Jamhuri ya Muungano kikisimamiwa na Bodi ya Pareto Tanzania ambapo hatimaye kilibinafsishwa mwaka 1998 kwa mwekezaji wa kigeni kampuni ya International Chemical Producers (ICP) ya nchini Afrika Kusini.
Inazidi kuelezwa kuwa kampuni ya ICP nayo iliuza hisa zake kwa kampuni ya....
Fundi wa kiwanda cha Pareto kilichopo Mafinga wilayani Mufindi akifungua moja ya mashine ya kusindika sumu ya pareto kwa ajili ya kuuzwa kama vyuma chakavu.
Utafiti uliofanywa na wataalamu kutoka Marekani wamependekeza, Waafrika wanaougua malaria huenda wakawa wanapata matibabu ya kiwango cha chini.
Watafiti kutoka kundi la Pharmacopeia wamegundua kwamba baina ya asilimia 26 na 44 ya dawa za kupambana na malaria Uganda, Senegal na Madagasacr ni zenye uwezo mdogo.
Kundi hilo, ambalo linafanya utafiti kwa niaba ya shirika la afya duniani WHO, limesema dawa za viwango vya chini zinatumiwa na watabibu wa hospitali za umma pamoja na za binafsi.
WHO wameonyesha wasiwasi kwamba dawa hizo zenye udhaifu mkubwa zinaweza kusababisha mwili usiweze kupambana na vijidudu vya malaria.
ULE mjadala moto wa sakata zito la utoaji zabuni ya ufuaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond Development LLC, utakuwa wa siku moja tu; siku ya mwisho ya Mkutano wa 18 wa Bunge la Jamhuri....
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, ameuagiza uongozi wa mkoa wa Morogoro na wa wilaya ya Kilosa kujenga makazi ya muda katika shule wanazosomea wanafunzi walioathirika na mafuriko yaliyoikumba wilaya hiyo ili waishi hapo na kuwaepusha wasichana kupata mimba...
UTAPELI MKUBWA WAZIMWA UWANJA WA NDEGE DAR Mtego wa Polisi wanasa mmoja (ONLINE VERSION) Mtuhumiwa wa utapeli, Ashrafu Kingu,(kati) akiwa amedhibitiwa na askari kanzu wa uwanja wa ndege. Kulia nyuma ni Bi. Hilda. Christopher Lissa na Richard Bukos. Walinzi wa Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam, kwa kushirikiana na askari kanzu , Februari 3, mwaka huu walifanikiwa kuzima jaribio la utapeli mkubwa wa mamilioni ya fedha uliokuwa ufanyike uwanjani hapo. Katika sekeseke hilo, Polisi walifanikiwa kumnasa mtu mmoja aitwaye Ashrafu Kingu ambaye inadaiwa ni tapeli mzoefu kutoka katika genge moja lenye mtandao mkubwa wa shughuli hiyo uliosambaa nchini kote na hata nje ya nchi. Inadaiwa kuwa, matapeli hao walisuka ....... ...imeshakuwa soo...nitaficha wapi uso wangu...Ashrafu Kingu. ...dili limebumburuka...Ashrafu Kingu