arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » hadithi za Shigongo

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» Mpenzi mwenye tabia hizi m ...
» (SIMULIZI ZA CHUMBANI) MDUA ...
» Mduara wa Mahaba (19)
» (SIMULIZI ZA CHUMBANI) MDUA ...
» Aisha Madinda: NGONO INANIU ...
» JACKLINE AMUANIKA ALIYEMTOA ...
» KANUMBA: NARGIS ALINITESA ...
» UNATAKA NIKUKANDAMIZE M ...
» BAKWATA KWAFUKUTA!
» TUMEWALETEA MWENGE!
» Kikwete sasa aichambua ...
» The Assassination -22
» WAISLAM, WAKRISTO WAGOM ...
» Mbongo ashinda Sh milio ...

 

THE BLOOD DEAL! (Kazi ya damu- 28)

hadithi za Shigongo  
Muddy, mlemavu ambaye si rahisi kumgundua kuwa ni muuaji kutokana na alivyoonekana machoni mwa wananchi analisumbua Jeshi la Polisi kwa kipindi kirefu, kazi yake kubwa ni kuua wanawake na kuwakata sehemu zao za siri kisha kuwagonga muhuri wenye alama ya 10000DY! Kazi ambayo ana ndoto kubwa ya kujipatia utajiri baada ya kumuuzia mganga wa kienyeji mwenyeji wa Zambia kwa ajili ya mambo ya kishirikina, wakiamini viungo hivyo hufanya migodi itoe dhahabu nyingi.

Baada ya kufanikiwa kuwatoroka askari hatimaye Muddy anapata lift ya Fuso akijifanya mwanafunzi nia yake atoke katikati ya Jiji la Dar es Salaam anapotafutwa kwa udi na uvumba, hata hivyo ndani ya Fuso alipowekwa nyuma ya bodi inasikika harufu kali sana, mwisho anajitetea kuwa ni dawa ya tumbo aliyoiweka.

Askari wanaamua kumfuatilia muuaji huyo na kuweka geti kila njia inayotoka jijini ili kukagua magari ya abiria na mizigo wakimtafuta Muddy. Ndani ya Fuso alipokuwa Muddy dereva anaulizwa na askari iwapo amebeba abiria mlemavu, bila kuficha kutokana na maelezo ya askari anafichua siri kuwa amebeba mlemavu mwenye mfuko unaotoa harufu kali, zoezi la kumtia mikononi Muddy linakuwa rahisi, wanamfikisha Kituo cha Polisi Kibaha na baadaye akasafirishwa mpaka jijini Dar es Salaam, wakuu wote wa jeshi hilo pamoja na Inspekta Jenerali anamshuhudia Muddy aliyekuwa akiwanyima usingizi. Anapigwa hali inayomfanya aombe kuelezea kilichotokea. Je, Muddy anataka kuwaeleza nini askari? SONGA NAYO...
    (6 January 2009)
Views: 300 | Maoni (9) | Soma Zaidi

 

GAMBOSHI- 28

hadithi za Shigongo  
Msichana mrembo Deborah Minja, anashiriki mashindano ya urembo na mara zote anaibuka mshindi, ila utata mkubwa unaibuka kutokana na vifo vinavyotokea katika mazingira ya kutatanisha kwa wasichana wenzake ambao walikuwa wanapewa nafasi kubwa ya kushinda!

Anashinda Miss Sinza, Kinondoni na hatimaye Miss Tanzania kabla ya kwenda New Delhi, India kushiriki mashindano ya dunia ambapo aliibuka na ushindi ila baada ya kutokea vifo kama vilivyotokea katika mashindano mengine yaliyopita.
Anarudi nchini akiwa na ushindi huo mzito, matokeo ya kidato cha sita yalipotoka alikuwa amefaulu katika kiwango kizuri, hivyo akapata nafasi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambapo alianza kutafuta Shahada yake ya Kwanza ya Uchumi. Akiwa chuoni hapo alijikuta akiwa na uhusiano wa kimapenzi na kijana Bryson ambaye walikubaliana kutoshiriki tendo la ndoa hadi watakapofunga ndoa.

Siku moja Bryson anashindwa kuvumilia na kumbembeleza Deborah akubali kufanya naye mapenzi! Deborah hakuwa na ujanja tena, tamaa za mwili zilikuwa zimewaka, akajikuta akikubali! Baada ya kumalizika kwa tendo hilo, Bryson akafariki papo hapo! Baada ya hapo Deborah hakuwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi tena hadi alipomaliza masomo yake na kuanza kufanya kazi katika Benki ya CRDB Tawi la Moshi Mjini. Hapo ndipo alipokutana na James Simalenga ambaye alisoma naye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Baada ya mazungumzo waliyoyafanya katika Hoteli ya Coffeetree, walijikuta wakiingia katika uhusiano wa kimapenzi lakini katika mazingira ya kushangaza James alipata ajali mbaya ya gari wakiwa njiani wakitokea Bomang’ombe walipokwenda kufurahia maisha huko kwa usiku mzima.

Anitha ambaye sasa anaishi na Bw. & Bi. Massawe, amefunguliwa duka la simu katika eneo la Stendi Kuu ya Mkoa, ambapo baadaye aliamua kufungua akaunti. Akiwa amekwenda Benki, akashangaa kukutana na mtu aliyefanana kwa kila kitu na Malikia Jinani. Msichana huyo ni Deborah, kwanza alisita kumwambia, lakini baadaye walipozoeana na kukubali kwenda kwa Deborah, alimweleza ukweli.

Hapo ndipo Anitha alipoona giza nene mbele yake, kabla ya mwanga kurudi taratibu na kuwa katika hali ya kawaida. Hakuwa nyumbani kwa Deborah tena, alikuwa katika mazingira mengine mapya, mbele yake akiwa Deborah aliyemhakikishia yeye ndiye Malikia Jinani wa Gamboshi na kwamba asingetoroka tena baada ya kumkata ulimi.
Je, nini kitatokea? Hali ya Richard na wazazi wa Anitha ikoje huko Gamboshi? SONGA NAYO...
    (5 January 2009)
Views: 420 | Maoni (7) | Soma Zaidi

 

Tumaini la mwisho - 33

hadithi za Shigongo  
Kazi ya kumsaka Dk. Terrence inazidi kuwa ngumu kwa Greyson, kila anapokaribia kupata mwanzo wa kuelekea kwenye mafanikio, anakutana na vikwazo. Akiwa bado anashangazwa na hali ya afya ya Suleiman Yakubu ambaye alikuwa akiumwa ugonjwa wa akili, anakutana na maiti ya Hamid Usuni akiwa amejinyonga, pembeni kukiwa na majibu ya ukimwi pamoja na ujumbe aliouacha unaosema ameamua kufa baada ya kugundua ana ukimwi.

Greyson hakubaliani na matukio hayo, anachokifanya ni kwenda kupima alama za vidole vya mtu aliyetumia kamba pamoja na barua iliyoachwa iliyokuwa ikionyesha kwamba marehemu alikufa kwa ugonjwa wa ukimwi. Baada ya kupima majibu anayoyapata yanaonyesha kwamba alama za vidole siyo vya Hamid Usuni.

Akiwa anatafakari, akaamua kwenda kupumzika katika msitu wa Nyandah, lakini akiwa huko akashangaa kuona akifuatiliwa na magari mawili meusi na baadaye kukutana na mengine yakiwa yameegesha mbele yake. Mpambano wa kurushiana risasi unaanza, lakini baada ya Greyson kupigwa risasi ya paja na kuanguka chini, anagundua bastola yake ilikuwa imeisha risasi!

Hakuwa na ujanja tena, akakamatwa na kufungwa bomu kwenye mti! Bomu likawa limetegeshwa lilipuke baada ya saa moja, akaachwa porini akisubiria kifo chake. Greyson alijitahidi kujinasua lakini hakufanikiwa. Zikiwa zimebaki dakika tano tu, kabla bomu halijalipuka, Michelle mke wake alifika porini ambapo alijitahidi kulitoa lile bomu na kulitupia pembeni.
Likalipuka mbele ya macho yao, baada ya hapo akajitahidi kumfungua minyororo na kufanikiwa. Wakakumbatiana wakilia kwa huzuni, lakini msimamo wa Greyson ulikuwa ule ule, kumsaka Dk. Terrence na kumtia mikononi mwake. Je, nini kitatokea? SONGA NAYO...
    (5 January 2009)
Views: 279 | Maoni (4) | Soma Zaidi

 

Mtumwa wa ngono (62)

hadithi za Shigongo  
Familia mbili za kitajiri zenye furaha na upendo zinaondoka London nchini Uingereza kwenda kutembea California nchini Marekani, masaa machache wakiwa eneo la Luziana kunatokea kimbunga kiitwacho Katrina na hapo ndipo matembezi hayo yanapogeuka huzuni na kilio. Gari la familia ya Joan pacha wake Joseph linapata ajali mbaya baada ya kubebwa na kimbunga cha Katrina na kutupwa chini ya daraja hali inayosababisha Joan apoteze fahamu, anapozinduka anajikuta akilia kwasababu mumewe na mwanaye mpendwa John hawapo. Hilo linamfanya aone yupo ndotoni, hakuamini watu waliokuwa wakiongea nao ndani ya gari muda mfupi walishakuwa marehemu, baadaye anazunguka eneo hilo bila mafanikio na mwisho anaokota nguo za mwanaye zikiwa mita ishirini toka gari lilipoangukia, analia sana akimuomba Mungu afanye miujiza aweza kumpata mumewe na mwanaye.Je, Bravo na John wataonekana? SONGA NAYO...
    (3 January 2009)
Views: 408 | Maoni (7) | Soma Zaidi

 

GAMBOSHI (27)

hadithi za Shigongo  
Baada ya Deborah kugoma kufanya ngono na Bryson kwa muda mrefu, hatimaye Bryson alimbana na kujikuta wakifanya mchezo huo mchafu! Muda mfupi baada ya kumaliza, Bryson anaanza kutokwa na mapovu puani na mdomoni kisha akatupatupa miguu kabla ya kutulia kabisa. Bryson alikuwa amekufa!

Deborah akapiga kelele ambapo watu walijaa pamoja na Polisi wa Kituo Cha Mlimani, Bryson akapelekwa Zahanati ya Chuo, alipopimwa ikagundulika alikuwa amekufa. Deborah akatakiwa kupelekwa Polisi kwa ajili ya kuisaidia Polisi. Je, nini kitatokea? SONGA NAYO....
    (2 January 2009)
Views: 434 | Maoni (9) | Soma Zaidi

 

THE LAST HOPE (tumaini la mwisho) 32

hadithi za Shigongo  
Kitendo cha kumkuta Suleiman Yakubu anaumwa ugonjwa wa akili, kilimchanganya sana Greyson, lakini alichanganyikiwa zaidi baada ya kwenda Khartoum kuonana na Hamid Usuni kwa mara ya pili, halafu akamkuta amekufa.

Akili yake haikukubaliana kabisa na kifo chake, alijua wazi kulikuwa na mkono wa Dk. Terrence! Je, ni kweli ni mkono wa Dk. Terrence? Yupo hai? Nini kitatokea katika maisha ya Greyson na mkewe Michelle? SONGA NAYO...
    (1 January 2009)
Views: 329 | Maoni (10) | Soma Zaidi

 

Beyond Love 14

hadithi za Shigongo  
Tom yupo shimoni akiwa hana uwezo wa kupumua vizuri, anaomba sala ya ‘baba Yetu’, akiamini ingemsaidia kabla ya kifo chake. Lakini alipomaliza sala hiyo na kuangalia dhahabu iliyokuwa kwenye mfuko wake, aliumia sana moyo wake.
Alijipa matumaini ya kutoka, akiamini kufanikiwa kwake kutoka kungekuwa mwisho wa maisha ya kifukara na mateso. Akamuomba Mungu kwa mara nyingine amsaidie kutoka akiwa hai. Je, atafanikiwa? SONGA NAYO...
    (1 January 2009)
Views: 351 | Maoni (5) | Soma Zaidi

 

(Mtumwa wa ngono-59

hadithi za Shigongo  
Dina anapelekwa Hospitali ya Homerton University mjini London kupata matibabu ya afya yake baada ya kugundulika kuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa ngozi na upungufu wa vitamini hali inayomfanya afya yake irejee vema siku chache na kupewa wadhifa wa mwenyekiti wa Dijojo Group Companies watoto wake Joan na Joseph wakiwa wakurugenzi wa kampuni hizo kubwa nchini Uingereza.

Utajiri unaongezeka zaidi na kuwafanya Joan na Joseph kufahamika miongoni mwa matajiri wakubwa jijini London, miaka mitano baadaye Joan anapata mchumba mwanamuziki wa Rock kutoka nchini Marekani, Bravo Benedict na kufunga ndoa katika kanisa kubwa nchini Uingereza la Kingsway International Christian Center (KICC), baadaye kwenda kufanya sherehe kubwa iliyohudhuriwa na watu maarufu nchini Marekani na Uingereza katika hoteli ya kifahari ya The Milestone. Ilikuwa sherehe iliyowavutia watu wengi sana na iligharimu fedha nyingi kukamilisha sherehe hiyo ikiwa imeongoza kutangazwa na vyombo vingi vya habari nchini Uingereza.

Bwana harusi Bravo alisimama akamlisha keki mkewe mpendwa Joan wimbo wake ukiwatumbuiza taratibu, wote nyuso zao zilipabwa na furaha isiyoelezeka. Joan alibubujikwa na machozi ya furaha akishindwa kuamini iwapo anaitwa Mrs Bravo Benedict.

Ilipofika zamu ya Joan kumlisha mumewe keki, watu wote walishtushwa na mwanamke aliyesimama na kutembea haraka akibubujikwa machozi sura yake ikionyesha dalili za jambo muhimu la kuwaeleza wanandoa hao, anashindwa na kuishia kuwaita majina yao akidai haamini kisha kudondoka chini na kupoteza fahamu. Je, mwanamke huyu ni nani? Kwanini amedondoka na kupoteza fahamu? SONGA NAYO...
    (31 December 2008)
Views: 435 | Maoni (4) | Soma Zaidi

 

THE LAST HOPE (tumaini la mwisho) 31

hadithi za Shigongo  
Kazi inazidi kuwa ngumu kwa Greyson, kitendo cha Mkuu wa Chuo kusita kumweleza kilichomsibu Suleiman Yakub kilimfanya azidi kuona giza nene mbele yake. Je, nini kitatokea? SONGA NAYO....
    (31 December 2008)
Views: 322 | Maoni (3) | Soma Zaidi

 

(Kazi ya damu- 27)

hadithi za Shigongo  
Muddy ni mlemavu wa kutambaa chini anayetafutwa kwa udi na uvumba na polisi kwa kosa la mauaji ya mtungo, yanayohusisha wanawake ambao huwaua na kuwakata sehemu zao za siri kisha kuwagonga muhuri wenye alama ya 10000DY! Kazi hii ametumwa na mganga wa kienyeji mwenyeji wa Zambia anayevihitaji viungo hivyo kwa ajili ya mambo yake ya Kishirikina, eti viungo hivyo hufanya migodi iteme dhahabu!

Mara kadhaa Muddy amenusurika kukamatwa na sasa yupo ndani ya teksi akijaribu kuwatoroka polisi wanaomfukuza kwa nyuma, lengo lake ni kufika stesheni ya Tazara ambako atapanda treni na kusafiri mpaka Zambia, huko atamkabidhi mganga bidhaa zake na kupokea kitita kikubwa cha fedha na kurudi tena mjini kuendelea na mauaji! Ana ndoto za kujipatia utajiri kwa njia haramu.

Dakika kumi na tano baadaye dereva akiendesha gari kwa kasi akiwa maeneo ya Tabata Relini, muda mfupi tu kabla hajafika Buguruni, alishangaa kuona ving’ora vikija kwa kasi nyuma yake, moyo wake ukashtuka, hakuelewa ni kitu gani kilikuwa kikija, alipotazama vizuri aligundua kwamba magari hayo yalikuwa ni ya polisi, moyo wake ukazidi kudunda.
Je, nini kitafuata? Muddy atakamatwa? SONGA NAYO…
    (30 December 2008)
Views: 449 | Maoni (7) | Soma Zaidi

 

GAMBOSHI- 26

hadithi za Shigongo  
Msichana mrembo Deborah Minja, anayesoma Shule ya Sekondari Jangwani anawashangaza wengi baada ya kushiriki mashindano ya urembo na kuibuka mshindi! Kitu cha kushangaza ni kwamba kila mashindano hayo yanapokaribia fainali, warembo wanaopewa nafasi za kushinda wanakufa kwa ugonjwa wa kuharisha!

Hali inaendelea kuwa hivyo hata baada ya kumaliza Miss Sinza, Kinondoni na Miss Tanzania. Baadaye anakwenda kushiriki mashindano makubwa duniani, Miss Word. Huko nako, washiriki wanne waliokuwa wakipewa nafasi za juu za kushinda wanafariki kwa ugonjwa ule ule wa kuharisha!

Wakati matokeo yanatangazwa, kijana mmoja ambaye alikuwa mdau mkubwa wa urembo nchini India, alikasirika sana baada ya kugundua msihiriki wao amefariki dunia na mrembo aliyetwaa taji hilo ni Deborah Minja ambaye alikuwa na skendo ya uchawi. Akaanza kupita katikati ya watu akielekea jukwaani akiwa na nia moja tu, kumuua Deborah! Je, atafanikiwa? SONGA NAYO...
    (28 December 2008)
Views: 569 | Maoni (8) | Soma Zaidi

 

Tumaini la mwisho - 30

hadithi za Shigongo  
Ni vita mbaya ambayo ingawa Greyson Alikuwa na silaha lakini anakuwa kama ameshika fimbo tu! Giza nene linatanda mbele yake, kila anachokifanya kinagonga mwamba. Anasumbuliwa na mtu mmoja tu, Dk. Terrence.

Dk. Terrence muuaji katili ambaye huiba mioyo ya watu na kwenda kuiuza Uingereza kwa matajiri wenye matatizo ya moyo anakisumbua kichwa cha Greyson. Mara ya kwanza wakati akisikia taarifa za kifo chake, akajikuta akiingia mikononi mwake akijifanya Padre mwenye hospitali kubwa porini kumbe alikuwa ni Dk. Terrence!

Hatua za mwisho kabisa kabla ya kupasuliwa vifua vyao yeye na mpenzi wake Michelle, anaokolewa na askari wa Interpol wa Sudan. Taarifa za kifo chake kwenye helkopta zikataa kabisa kuingia akilini mwake. Pamoja na majibu ya vipimo vya DNA kudhibitisha kwamba maiti iliyokuwa kwenye helkopta ilikuwa ya Dk. Terrence, bado Greyson hakuamini jambo hilo.

Watu ambao aliamini wangekuwa msaada mkubwa kwao ni Suleiman Yakubu na Hamid Usuni. Mtu wa kwanza kuonana naye alikuwa ni Hamidi Usuni ambaye anamhakikishia kwamba majibu waliyoyatoa yalikuwa na ukweli.
Alipomuulizia Suleiman Yakubu akaambiwa kwamba alikwenda masomoni Uingereza baada ya kupata scholarship. Hapo akachanganyikiwa, alikuwa na kazi ya ziada. Je, nini kitatokea? Ni kweli Suleiman Yakubu amekwenda masomoni Uingereza? SONGA NAYO...
    (28 December 2008)
Views: 365 | Maoni (5) | Soma Zaidi

 

The sex slave (Mtumwa wa ngono (60)

hadithi za Shigongo  
Baada ya Dina kuua akiwa na umri wa miaka kumi na sita anatumikia kifungo cha maisha jela zaidi ya miaka ishirini na tano ndani ya Gereza la Butimba jijini Mwanza. Mfungwa Dina anayevuja damu nyingi kupitia mfuko wa plastiki uliofichwa ndani ya sare zake na mirija iliyopenyeza kutoka tumboni mpaka sehemu za siri unamfanya kila mfungwa na askari jela kuamini hali yake ni mbaya, madaktari wanathibitisha ugonjwa unaomsumbua Dina ni Saratani ya Kizazi jambo lililofanywa kwa siri kubwa na Wakili John Cochran na Joan mwanaye Dina wakipigana kufa na kupona kumuombea msamaha kwa Rais, hatimaye Dina akaachiwa huru.

Muda mfupi baada ya kuachiwa huru, Dina na watoto wake Joan na Joseph, Dk. Ian Duncan pamoja na Wakili Mmarekani John Cochran wanarejea nchini Uingereza, ajabu Dina anabadilika muda mfupi ndege iliporuka angani hali inayomshangaza Joseph akitaka kujua nini kilitokea hadi mama yake aonekane mzima wa afya wakati muda mfupi uliopita alipandishwa kwenye ndege kutumia machela.

Kwa furaha aliyokuwa nayo Joan anashindwa kusimulia hatimaye kumuomba John Cochran amsaidie, lakini anamuomba Joseph avumilie hadi watakapofika Uingereza angemweleza kilichotokea.

Masaa saba baadaye ndege ilipotua Uwanja wa Ndege wa Healthrow, London, wanapokelewa na familia ya Dk. Duncan na kwenda eneo la East London ambako Wakili John Cochran anamuomba Dk. Duncan familia yake iondoke ili asimulie siri kubwa ambayo hakutaka itoke katika ukuta wa nyumba hiyo. Wanabaki peke yao na kusimulia sinema nzima ilivyochezwa hadi kumtoa Dina Gerezani Butimba. Kwa pamoja wakagonganisha glasi zao kwa furaha wakisherehekea ushindi mkubwa wa kumtoa mfungwa wa maisha uraiani. Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO...
    (27 December 2008)
Views: 588 | Maoni (5) | Soma Zaidi

 

GAMBOSHI (25)

hadithi za Shigongo  
Kitendo cha Anita kusikia sauti ya mumewe Richard ikiita mlangoni ilimshtua sana, hakuwa tayari kumuacha mumewe akateseke! Pamoja na kuzuiwa na wakwe zake Bwana na Bibi Massawe, Anita alitoka.
Muda mfupi baada ya Anita kwenda nje, ukimya ukatawala, walipotoka hawakumkuta. Kila mmoja akapigwa na butwaa. Wakasubiri hadi asubuhi lakini Anita hakutokea! Amekwenda wapi? Je, atapatikana? SONGA NAYO...
    (26 December 2008)
Views: 522 | Maoni (6) | Soma Zaidi

 

The last Hope -Tumaini la mwisho-29

hadithi za Shigongo  
Dk. Terrence alikisumbua sana kichwa cha Greyson, ni muuaji aliyekuwa katika kiwango cha juu sana. Pamoja na kumfuatilia kwa umakini mkubwa lakini bado jitihada zake hazikuzaa matunda!
Kuwepo kwa Padri Sylvester Gavon ambaye alikuwa akifurahia sana kifo cha Dk. Terrence kulimfurahisha sana. Siku moja wakapanga ahadi ya kwenda kumtembelea katika Hospitali yake aliyoifungua porini.

Walipofika huko akiwa na Michelle alishangaa kumuona Padri huyo mzee akinyofoa nywele pamoja na ndevu zake, akawa mwingine kabisa! Alikuwa ni Dk. Terrence ambaye alimhakikishia kifo! Greyson akiwa amefungwa minyororo kwenye nguzo, mchumba wake Michelle alikuwa amelazwa chini huku jitihada za kuutoa moyo wake kwa kutumia shoka zikiendelea.

Greyson hakuwa tayari kumpoteza mpenzi wake mbele ya macho yake, akaanza kutoa maneno makali ili afunguliwe ambapo hapo alipanga kufanya mapinduzi ya hali ya juu. Tofauti na matarajio yake, alipofunguliwa alipuliziwa dawa za usingizi ambapo mara moja alipoteza fahamu.

Alipozinduka alijikuta akiwa hospitalini ambapo alielezwa wazi kwamba polisi wa Interpol ndiyo waliomsaidia. Akaamua kumsafirisha Michelle ili yeye aendelee na kazi ya kumsaka Dk. Terrence! Taarifa za kwamba alikufa ndani ya ndege iliyolipuka akiwa anajaribu kutoroka hazikuingia kabisa akilini mwake.

Siku ya pili yake baada ya Michelle kuondoka, Greyson akapiga simu nyumbani kwao Tanzania, lakini mama yake akamwambia Michelle hakuwa amefika! Hofu inamvaa, mara moja anafuatilia Kenya Airways ambapo anapewa taarifa kwamba Michelle alizidiwa akiwa angani hivyo kushushwa Kenyatta Hospital kwa matibabu.

Anakwenda kuonana naye ambapo siku chache baadaye anaruhusiwa. Akiwa nyumbani Tanzania, Greyson anajaribu kumuaga mpenzi wake Michelle kwamba anarejea Khartoum kumfuatilia Dk. Terrence, jambo linalopingwa vikali na Michelle. Anakuwa tayari kuachana naye kama akiendelea kung’ang’ania kwenda Sudan.
Je, nini kitaendelea? Kwanini Michelle anamkataza Greyson kurudi Khartoum? SONGA NAYO...
    (26 December 2008)
Views: 348 | Maoni (3) | Soma Zaidi
Back  <<  1 2 3 ... 37 38 39  >>  Next Page
 

Kura Yako / Poll

Habari Katika Picha


Gazeti la Uwazi


Nani Yupo / Alikuwepo