Tembelea... |
 |
Kalenda |
 |

Marafiki wetu |
 |
Habari Zilizopita |
 |



  
| |
 |
|
|
 |
 |
|
 |
Muddy, mlemavu ambaye si rahisi kumgundua kuwa ni muuaji kutokana na alivyoonekana machoni mwa wananchi analisumbua Jeshi la Polisi kwa kipindi kirefu, kazi yake kubwa ni kuua wanawake na kuwakata sehemu zao za siri kisha kuwagonga muhuri wenye alama ya 10000DY! Kazi ambayo ana ndoto kubwa ya kujipatia utajiri baada ya kumuuzia mganga wa kienyeji mwenyeji wa Zambia kwa ajili ya mambo ya kishirikina, wakiamini viungo hivyo hufanya migodi itoe dhahabu nyingi.
Baada ya kufanikiwa kuwatoroka askari hatimaye Muddy anapata lift ya Fuso akijifanya mwanafunzi nia yake atoke katikati ya Jiji la Dar es Salaam anapotafutwa kwa udi na uvumba, hata hivyo ndani ya Fuso alipowekwa nyuma ya bodi inasikika harufu kali sana, mwisho anajitetea kuwa ni dawa ya tumbo aliyoiweka.
Askari wanaamua kumfuatilia muuaji huyo na kuweka geti kila njia inayotoka jijini ili kukagua magari ya abiria na mizigo wakimtafuta Muddy. Ndani ya Fuso alipokuwa Muddy dereva anaulizwa na askari iwapo amebeba abiria mlemavu, bila kuficha kutokana na maelezo ya askari anafichua siri kuwa amebeba mlemavu mwenye mfuko unaotoa harufu kali, zoezi la kumtia mikononi Muddy linakuwa rahisi, wanamfikisha Kituo cha Polisi Kibaha na baadaye akasafirishwa mpaka jijini Dar es Salaam, wakuu wote wa jeshi hilo pamoja na Inspekta Jenerali anamshuhudia Muddy aliyekuwa akiwanyima usingizi. Anapigwa hali inayomfanya aombe kuelezea kilichotokea. Je, Muddy anataka kuwaeleza nini askari? SONGA NAYO... |
|
 |
 |
|
 |
Msichana mrembo Deborah Minja, anashiriki mashindano ya urembo na mara zote anaibuka mshindi, ila utata mkubwa unaibuka kutokana na vifo vinavyotokea katika mazingira ya kutatanisha kwa wasichana wenzake ambao walikuwa wanapewa nafasi kubwa ya kushinda!
Anashinda Miss Sinza, Kinondoni na hatimaye Miss Tanzania kabla ya kwenda New Delhi, India kushiriki mashindano ya dunia ambapo aliibuka na ushindi ila baada ya kutokea vifo kama vilivyotokea katika mashindano mengine yaliyopita. Anarudi nchini akiwa na ushindi huo mzito, matokeo ya kidato cha sita yalipotoka alikuwa amefaulu katika kiwango kizuri, hivyo akapata nafasi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambapo alianza kutafuta Shahada yake ya Kwanza ya Uchumi. Akiwa chuoni hapo alijikuta akiwa na uhusiano wa kimapenzi na kijana Bryson ambaye walikubaliana kutoshiriki tendo la ndoa hadi watakapofunga ndoa.
Siku moja Bryson anashindwa kuvumilia na kumbembeleza Deborah akubali kufanya naye mapenzi! Deborah hakuwa na ujanja tena, tamaa za mwili zilikuwa zimewaka, akajikuta akikubali! Baada ya kumalizika kwa tendo hilo, Bryson akafariki papo hapo! Baada ya hapo Deborah hakuwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi tena hadi alipomaliza masomo yake na kuanza kufanya kazi katika Benki ya CRDB Tawi la Moshi Mjini. Hapo ndipo alipokutana na James Simalenga ambaye alisoma naye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Baada ya mazungumzo waliyoyafanya katika Hoteli ya Coffeetree, walijikuta wakiingia katika uhusiano wa kimapenzi lakini katika mazingira ya kushangaza James alipata ajali mbaya ya gari wakiwa njiani wakitokea Bomang’ombe walipokwenda kufurahia maisha huko kwa usiku mzima.
Anitha ambaye sasa anaishi na Bw. & Bi. Massawe, amefunguliwa duka la simu katika eneo la Stendi Kuu ya Mkoa, ambapo baadaye aliamua kufungua akaunti. Akiwa amekwenda Benki, akashangaa kukutana na mtu aliyefanana kwa kila kitu na Malikia Jinani. Msichana huyo ni Deborah, kwanza alisita kumwambia, lakini baadaye walipozoeana na kukubali kwenda kwa Deborah, alimweleza ukweli.
Hapo ndipo Anitha alipoona giza nene mbele yake, kabla ya mwanga kurudi taratibu na kuwa katika hali ya kawaida. Hakuwa nyumbani kwa Deborah tena, alikuwa katika mazingira mengine mapya, mbele yake akiwa Deborah aliyemhakikishia yeye ndiye Malikia Jinani wa Gamboshi na kwamba asingetoroka tena baada ya kumkata ulimi. Je, nini kitatokea? Hali ya Richard na wazazi wa Anitha ikoje huko Gamboshi? SONGA NAYO... |
|
 |
 |
|
 |
Kazi ya kumsaka Dk. Terrence inazidi kuwa ngumu kwa Greyson, kila anapokaribia kupata mwanzo wa kuelekea kwenye mafanikio, anakutana na vikwazo. Akiwa bado anashangazwa na hali ya afya ya Suleiman Yakubu ambaye alikuwa akiumwa ugonjwa wa akili, anakutana na maiti ya Hamid Usuni akiwa amejinyonga, pembeni kukiwa na majibu ya ukimwi pamoja na ujumbe aliouacha unaosema ameamua kufa baada ya kugundua ana ukimwi.
Greyson hakubaliani na matukio hayo, anachokifanya ni kwenda kupima alama za vidole vya mtu aliyetumia kamba pamoja na barua iliyoachwa iliyokuwa ikionyesha kwamba marehemu alikufa kwa ugonjwa wa ukimwi. Baada ya kupima majibu anayoyapata yanaonyesha kwamba alama za vidole siyo vya Hamid Usuni.
Akiwa anatafakari, akaamua kwenda kupumzika katika msitu wa Nyandah, lakini akiwa huko akashangaa kuona akifuatiliwa na magari mawili meusi na baadaye kukutana na mengine yakiwa yameegesha mbele yake. Mpambano wa kurushiana risasi unaanza, lakini baada ya Greyson kupigwa risasi ya paja na kuanguka chini, anagundua bastola yake ilikuwa imeisha risasi!
Hakuwa na ujanja tena, akakamatwa na kufungwa bomu kwenye mti! Bomu likawa limetegeshwa lilipuke baada ya saa moja, akaachwa porini akisubiria kifo chake. Greyson alijitahidi kujinasua lakini hakufanikiwa. Zikiwa zimebaki dakika tano tu, kabla bomu halijalipuka, Michelle mke wake alifika porini ambapo alijitahidi kulitoa lile bomu na kulitupia pembeni. Likalipuka mbele ya macho yao, baada ya hapo akajitahidi kumfungua minyororo na kufanikiwa. Wakakumbatiana wakilia kwa huzuni, lakini msimamo wa Greyson ulikuwa ule ule, kumsaka Dk. Terrence na kumtia mikononi mwake. Je, nini kitatokea? SONGA NAYO... |
|
 |

 |
|
 |
Muddy ni mlemavu wa kutambaa chini anayetafutwa kwa udi na uvumba na polisi kwa kosa la mauaji ya mtungo, yanayohusisha wanawake ambao huwaua na kuwakata sehemu zao za siri kisha kuwagonga muhuri wenye alama ya 10000DY! Kazi hii ametumwa na mganga wa kienyeji mwenyeji wa Zambia anayevihitaji viungo hivyo kwa ajili ya mambo yake ya Kishirikina, eti viungo hivyo hufanya migodi iteme dhahabu!
Mara kadhaa Muddy amenusurika kukamatwa na sasa yupo ndani ya teksi akijaribu kuwatoroka polisi wanaomfukuza kwa nyuma, lengo lake ni kufika stesheni ya Tazara ambako atapanda treni na kusafiri mpaka Zambia, huko atamkabidhi mganga bidhaa zake na kupokea kitita kikubwa cha fedha na kurudi tena mjini kuendelea na mauaji! Ana ndoto za kujipatia utajiri kwa njia haramu.
Dakika kumi na tano baadaye dereva akiendesha gari kwa kasi akiwa maeneo ya Tabata Relini, muda mfupi tu kabla hajafika Buguruni, alishangaa kuona ving’ora vikija kwa kasi nyuma yake, moyo wake ukashtuka, hakuelewa ni kitu gani kilikuwa kikija, alipotazama vizuri aligundua kwamba magari hayo yalikuwa ni ya polisi, moyo wake ukazidi kudunda. Je, nini kitafuata? Muddy atakamatwa? SONGA NAYO… |
|
 |

 |
|
 |
Dk. Terrence alikisumbua sana kichwa cha Greyson, ni muuaji aliyekuwa katika kiwango cha juu sana. Pamoja na kumfuatilia kwa umakini mkubwa lakini bado jitihada zake hazikuzaa matunda! Kuwepo kwa Padri Sylvester Gavon ambaye alikuwa akifurahia sana kifo cha Dk. Terrence kulimfurahisha sana. Siku moja wakapanga ahadi ya kwenda kumtembelea katika Hospitali yake aliyoifungua porini.
Walipofika huko akiwa na Michelle alishangaa kumuona Padri huyo mzee akinyofoa nywele pamoja na ndevu zake, akawa mwingine kabisa! Alikuwa ni Dk. Terrence ambaye alimhakikishia kifo! Greyson akiwa amefungwa minyororo kwenye nguzo, mchumba wake Michelle alikuwa amelazwa chini huku jitihada za kuutoa moyo wake kwa kutumia shoka zikiendelea.
Greyson hakuwa tayari kumpoteza mpenzi wake mbele ya macho yake, akaanza kutoa maneno makali ili afunguliwe ambapo hapo alipanga kufanya mapinduzi ya hali ya juu. Tofauti na matarajio yake, alipofunguliwa alipuliziwa dawa za usingizi ambapo mara moja alipoteza fahamu.
Alipozinduka alijikuta akiwa hospitalini ambapo alielezwa wazi kwamba polisi wa Interpol ndiyo waliomsaidia. Akaamua kumsafirisha Michelle ili yeye aendelee na kazi ya kumsaka Dk. Terrence! Taarifa za kwamba alikufa ndani ya ndege iliyolipuka akiwa anajaribu kutoroka hazikuingia kabisa akilini mwake.
Siku ya pili yake baada ya Michelle kuondoka, Greyson akapiga simu nyumbani kwao Tanzania, lakini mama yake akamwambia Michelle hakuwa amefika! Hofu inamvaa, mara moja anafuatilia Kenya Airways ambapo anapewa taarifa kwamba Michelle alizidiwa akiwa angani hivyo kushushwa Kenyatta Hospital kwa matibabu.
Anakwenda kuonana naye ambapo siku chache baadaye anaruhusiwa. Akiwa nyumbani Tanzania, Greyson anajaribu kumuaga mpenzi wake Michelle kwamba anarejea Khartoum kumfuatilia Dk. Terrence, jambo linalopingwa vikali na Michelle. Anakuwa tayari kuachana naye kama akiendelea kung’ang’ania kwenda Sudan. Je, nini kitaendelea? Kwanini Michelle anamkataza Greyson kurudi Khartoum? SONGA NAYO... |
|
 |
|
|
 |
Kura Yako / Poll |
 |
Habari Katika Picha |
|
 |

Nani Yupo / Alikuwepo |
 |
|