Mwanamuziki anayefunika kwa mvuto wa kimahaba, sex, Rehema Chalamila ‘Ray C’ ameaminika hisia zake kuwa mapenzi yake kwa Mwana-Hip Hop kutoka Kundi la Nako 2 Nako Soldiers, Isaac Waziri Makuto ‘Lord Eyez’ hayapimiki. Ray C aliliambia Ijumaa Wikienda Jumamosi iliyopita kuwa kutokana na kukamatika kimahaba kwa mwana-Nako huyo, imefikia hatua anajiona yeye kwa Lord Eyez ni sawa na mbwa kwa chatu, kwani hata itokee nini, ‘akimmisi’ atamtafuta kwa udi na uvumba...
Afande Mstaafu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mugisha Peter aliuaga mwaka 2008 kwa balaa kubwa baada ya kushindwa kutinga ukumbini katika sherehe ya harusi yake kwa kuogopa kufumaniwa na mkewe ambaye alifunga naye ndoa halali Oktoba 6, 1979 (kopi tunayo)....
Wakati New Year ikiwa jirani, huku Kundi la Ucheshi la Orijino Komedi likizidi kujitanua kwenye Luninga ya Taifa (TBC1), hali ya mambo inaonesha kuwa wasanii wa ‘grupu’ hilo hawatousahau mwaka 2008...
Mwanamuziki ‘bitoz’ wa muziki wa Bongo Fleva ambaye hivi karibuni amekuwa huru kutoka kifungoni kwa ‘huruma’ ya Rais JK, Khaleed Mohamed 'TID' amedaiwa kuoga maji ya baharini kwa siku tatu mfululizo kwa kile kilichosemekana ni kuondoa mabalaa...
Mama wa Miss Tanzania, namba 5, 2006-2007, Irene Uwoya, mwishoni mwa wiki iliyopita alilianzisha timbwili la kufa mtu baada ya mwanae kutokomea kusikojulikana katika sherehe za siku yake ya kuzaliwa (Birthday)...
Mrembo Aileen Francisco ameweka hostoria nchini kwa kuwa Mchina wa kwanza kufanyiwa tohara ambayo ni mila ya baadhi ya makabila barani Afrika, inayopigwa vita hivi sasa kwamba ni potofu...
Mnenguaji mwenye ‘kismati’ cha kupendwa nchini, Aisha Mbegu ‘Madinda’, ametoa kile kinachoitwa kwa lugha ya Kiingereza My Confession (Kukiri Kwangu), baada ya kulitobolea gazeti hili kuwa, kinachomfanya awe hoi kitandani ni ngono...
Katika tukio linalosherehesha usemi kwamba mtunga sheria ndiye mvunja sheria, Mbunge wa Buchosa (CCM), Samuel Chitalilo hivi karibuni, anadaiwa kubambwa akimwaga ‘kojo’ hadharani, hivyo kuidhalilisha ‘taito’ yake.
Lile sakata la mfanyabiashara nguli nchini, Reginald Abraham Mengi kupewa siku saba za kuweka hadharani uthibitisho wake kwamba kuna waziri ‘yanki’ wa awamu ya nne amepania kumfanyia mufilisi, limeingia sura mpya baada ya baadhi ya wananchi kusema waziri huyo amejitaja...
Mrembo anayeiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya Dunia (Miss World), 2008 yatakayofanyika Desemba 13, 2008 nchini Afrika ya Kusini, Nasreen Karim ametajwa kuwa ni mwizi wa mume za mtu kwa asilimia mia moja...
HUZUNI Baba anaumia maabusu keko, bintiye anafunga ndoa, pengo la baba laonekana wazi! Hata hivyo utata watawala harusi nzima
Na Mwandishi Wetu
Huzuni kubwa ilitawala kwenye familia ya aliyekuwa Waziri wa Fedha katika Serikali ya Awamu ya Tatu, Basil Mramba Jumamosi iliyopita, kufuatia kigogo huyo kukosa ndoa ya binti yake, Aifena Mramba aliyeolewa na Evans Msiba ambaye ni mtoto wa bosi wa zamani wa Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA), Aristablus Elvis Musiba...
Taaban Mashitaka ya wizi yanayomkabili mista wake yampa uchizi, presha yamuweka pagumu, azimika baada y a kufakamia klaji kutuliza mawazo
Na Richard Bukos
Wakati hali ikiwa si shwari kwa washukiwa mbalimbali wa utafunaji wa noti za wananchi a.k.a mafisadi, mwanamke anayedaiwa kuwa ni nyumba ndogo ya mmoja wa watuhumiwa waliochota fedha za EPA yupo taaban...
Wakati ‘ishu’ ya ufisadi, ikigeuka wimbo wa taifa Tanzania kutokana na kujizolea umaarufu mkubwa hivi sasa, mmoja wa viongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kiluteri (KKKT) Dayosisi ya Mashariki amesema kuwa hali ya mambo inayoendelea nchini inamtesa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere...
Ndoa ya muimbaji maarufu wa muziki wa Kizazi Kipya nchini, Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee’ na mtangazaji wa Redio Clouds FM, Gadner Gabriel Fikirini Habash inadaiwa kushikiliwa na nyuzi moja tu kabla ya kukatika, imefichuka...