Baada ya misukosuko mingi, Thabit anaamini kabisa kuwa Nargis si mtu wa kawaida na kuamua kumueleza ukweli ili waachane. Lakini Nargis ambaye ni jini anamueleza ukweli kuhusiana na yeye alivyo na jinsi alivyoushikilia uhai wa Thabit kama ataamua kuachana naye. Thabit anaamua kukubali kuwa na Nargis ili kuokoa maisha yake. Nini hatma ya yote? TWENDE PAMOJA.... ILIPOISHIA: Ni mapenzi yangu mazito kwako ambayo yameambatana na siri nzito ambayo sina budi kuisema kwako kwa kuwa kila kitu sasa hivi kipo wazi. Thabit huwezi amini mwisho wa maisha yako ulikuwa jana Mwenge.” “Etii?” Thabiti alizidi kushtuka. “Katika watu waliotakiwa kufa jana wewe ni mmoja wapo.” “Nife mimi kwa kosa gani?” “Jana usiku uliona vitu gani?” “Vingi vya kutisha.” “Basi hivyo ndivyo vingeondoa maisha yako.” “Viniondoe kivipi?” SASA ENDELEA...
Taarifa za kifo cha Jeff zinaandikwa magazetini, Davina akiwa kwenye foleni akielekea ofisini kwake, alisoma habari hiyo kwenye magazeti. Ghafla akapoteza fahamu na kusababisha foleni kubwa! Nini kitatokea? Endelea...
“Sasa unauliza nini?” Alinijibu huku akitembea kwa kurukaruka kwa mguu mmoja. Alipoona mimi nimezubaa akanifuata: “Jipige kifuani kwa mkono.” Nikafanye hivyo.
“Hapo sawa sasa, nifuate mimi kwa kila hatua mpaka ndani na kuanza kazi, sawa?” Aliniuliza. Tulikwenda hadi kwenye mlango mkubwa, nikadhani atagonga ili tufunguliwe, kumbe sivyo bwana. “Kila ninachofanya mimi na wewe unaniiga, sawa?” Aliniambia akinigeukia, kwani nilikuwa nimesimama nyuma yake. “Sawa.”
“Haya tunaanza sasa.” Alijipiga tena kifua na mimi nikajipiga. Kufumba na kufumbua tukawa ndani, sebuleni. SASA ENDELEA…
Mpenzi msomaji, kijana Kafumu aliyefundishwa uchawi na bibi yake, anaendelea kusimulia mambo ya kichawi aliyokumbanayo katika maisha yake ambapo alirithishwa mkoba wa kichawi na uganga wa babu yake. Wiki iliyopita uliona akiwa na bibi yake walivyokwenda kwa mjomba wake anayeishi kijiji cha Kigwa kuhudhuria kikao cha kichawi cha ukoo wao ambapo mjomba huyo aliyekuwa kiongozi wa wachawi alimwambia mambo mbalimbali ambayo alikuwa akiyafanya babu yake Kafumu ili ayafahamu kabla ya kurithishwa mkoba wa kichawi wa babu yake. Baada ya kikao hicho, mjomba awalitaarifi juu ya kikao kingine muhimu cha kichawi ambacho kingefanyika katika Ziwa Igombe eneo ambalo wachawi hukutana kwa ajili ya kufanya mambo yao ya kilosi pamoja na mikutano. Mjomba wake huyo alimsisitiza sana bibi ampeleke Kafumu katika kikao hicho ambacho pamoja na mambo mengine, watoto waliotakiwa kurithishwa mikoba ya kichawi wangepewa kinga kabla ya kukabidhiwa rasmi mikoba ya kichawi. Baada ya kuelezwa hivyo, bibi na Kafumu walirudi nyumbani na siku ya kwenda Ziwa Igombe ilipofikia walimpitia mjomba wa Kafumu katika Kijiji cha Kigwa.
Je, nini kilijiri katika kikao hicho kilichofanyika kandokando ya Ziwa Igombe? Ungana na KULWA MWAIBALE katika mkasa huu wa kweli uliomkuta kijana Kafumu…
Ilipoishia Alimfungulia chakula ambacho kilikuwa na harufu nzuri iliyomvutia Thabit, baada ya kunawa alikishambulia chakula kitamu kilichopikwa kwa ustadi wa hali ya juu. Chakula kama kile hakuwahi kula katika maisha yake. Sasa endelea...
Ilipoishia wiki iliyopita Nililala kwa unyonge, asubuhi nilijaribu kutembea lakini sikuweza, maumivu yalikuwa makali hasa kwenye mapaja. Nilibaki kitandani muda wote. Yule muwindaji alishinda akinihudumia kama yai, ingawa sikufurahia chochote kutokana na kitendo alichonifanyia, ukijumlisha na maumivu niliyokuwa nayo, moyo ulijaa kinyongo...
Kinaja Thabit amekuwa akitokewa na mambo ambayo kwa huona kama ndoto yenye ukweli. Bado mwanamke Mrembo Nargis amekuwa akimuweka njia panda kwa kushindwa kumuelewa na kiumbe wa aina gani. Pia hajui nini hatma yake baada ya kufukuzwa kazi kwa kosa la uzembe kazini. Nini hatima ya yote hayo kutajua yote TWENDE PAMOJA.... ILIPOISHIA: “Karibu mpenzi,” Thabit alinyanyua mdomo wake kumkaribisha Nargis. “Asante nimekaribia,” alikwenda kukaa pembeni ya Thabit. “Pole kwa usumbufu.” “Asante, au uliponielekeza hukuamini naweza kufika huku?” “Basi tu, labda nilichanganya wakati wa kukuelekeza.” “Tuachane na hayo, Sule, mambo?” Nargis alimgeukia Sule. “Safi,” Thabit alishtuka kusikia jina la Sule na kujiuliza amelijulia wapi. “Mhu, kwanza pole mwenzangu?” “Pole! Pole ya nini?” “Si nilipita kazini kwenu kuulizia, rafiki yako Jose alinieleza kilichokusibu, lakini usijali sana mpenzi wangu kila kitu kitakwenda vizuri” SASA ENDELEA....
Dili la mauaji ya Jeff linafanyika chini ya Kundi la Kimafia la Nyamangumu Camp, linaloongozwa na Master, lakini Roy aliyepewa kazi hiyo, anaamua kufanya dili ndani dili! Mchezo mzima unafanyika kwa kuagiza maiti iliyoharibiwa sura kutoka kwa Kijasho.
Maiti inavalishwa nguo za Jeff, inawekewa nyaraka mbalimbali za Jeff ili kuhalalisha kwamba ilikuwa maiti yake. Zoezi hilo linafanyika kwa mafanikio makubwa. Baada ya hapo, Roy analiingiza gari kwenye mti na kusababisha ajali mbaya! Je, nini kitatokea? Endelea kufuatilia...
“Ndiyo jina lako au msafiri unakwenda mahali?” “Siendi popote.” “Khaa! Sasa hapa kwako?” “Hapana.” “Sasa kwanini umefungua mlango bila hodi na umepanda kitandani kulala bila ridhaa yangu?” “Nisamehe sana.” “Basi ondoka.” Kauli yangu hiyo haikupata jibu zaidi ya mlio wa kukoroma kusikika kama mwanzo. Nilimsogelea yule mtu pale kitandani kwa lengo la kumfunua shuka na kumwona vizuri. Niliishika shuka kwenye ncha moja, nikaifunua kwa nguvu…
Mpenzi msomaji, kijana Kafumu aliyefundishwa uchawi na bibi yake, anaendelea kusimulia mambo ya kichawi aliyokumbanayo katika maisha yake ambapo alirithishwa mkoba wa kichawi na uganga wa babu yake. Wiki iliyopita uliona alivyokwenda kuhudhuria katika kikao cha kichawi ambapo akiwa na watoto wenzake, walipelekwa makaburini ambako maiti sita walifufuliwa kisha kiongozi wa wachawi alikata kipande cha sanda aliyovikwa kila maiti kisha vipande hivyo akavifunga katika mkono wa Kafumu na wenzake. Baada ya kufanya hivyo, aliwaeleza kazi ya vitambaa hivyo vya sanda wataelezwa na wazee waliowaacha kwenye kikao. Waliporudi kwa wazee na wachawi wengine,kiongozi wao aliwafungua vitambaa hivyo na kuviweka ndani ya tunguri lake kisha aliharisha kikao lakini alitoa maagizo kwamba kila mzazi au mlezi wa watoto waliotakiwa kurithishwa mikoba ya kichawi, ampeleke mwanaye kwa kiongozi wa kichawi wa ukoo wake ili mtoto husika akaelezwe historia ya mtu anayetakiwa kuurithi mkoba wake ambapo yeye alipelekwa katika kijiji cha Kigwa kwa mjomba wake ambaye alimfahamisha uwezo aliokuwanao babu yake aliyeitwa Kafumu aliyetakiwa kuurithi mkoba wake.
Aliambiwa mambo mengi ambayo enzi za uhai wa babu yake aliyafanya, kama kuamuru mti upasuke kisha aliingia ndani yake, kugeuza nywele kuwa nyoka. Kufuatia muda wa wachawi kuwa nje ya nyumba zao kwisha, mjomba huyo aliharisha kikao na kumtaka bibi na Kafumu warudi tena kesho yake ili amalizie kumsimulia mambo ambayo babu yake aliyafanya.
Je, ni mambo gani hayo? Ungana na KULWA MWAIBALE katika mkasa huu wa kweli uliomkuta kijana Kafumu…
ILIPOISHIA Alikumbuka baada ya kuondoka na yule mrembo na kwenda naye mpaka kwake ambako kulikuwa na uzuri wa ajabu na kuweza kulala naye kitanda kimoja lakini hakukumbuka kama walifanya naye mapenzi. Na asubuhi alipoamka kujikuta chumbani kwake tena kitandani jambo lile lilizidi kumchanganya sana. SASA ENDELEA...
ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA Usiku ulipofika licha ya kwamba yule muwindaji alinionesha chumba tofauti cha kulala lakini alinifuata na kunishawishi nifanye naye mapenzi. Ulikuwa ni mtihani mgumu! ...
Thabit kijana aliyekuwa akitoka kazini muda mbaya wa usiku na kujikuta akiwa peke yake katika kituo cha basi cha Mwenge. Bila kutegemea anatokewa na miujiza ambayo kwake ilikuwa kama yupo ndotoni, lakini kila kitu kilikuwa kweli na kumchanganya na kushindwa kuelewa kile ni kitu gani. Pia anakutana na mwanamke mrembo Nargis ambaye anazidi kumchanganya. Yule ni mwanamke wa aina gani ambaye bado hajamuelewa ni mwanadamu kweli. Je ile hali iliyojitokeza kituoni ni kweli na yule mwanamke ni nani? Ili kuyajua yote TUWE PAMOJA… ILIPOISHIA Alinyanyuka na kutoka nje akipitia ndoo yake yenye maji machache na mswaki mkononi alielekea bafuni kuoga. Baada ya kuoga alibadili nguo haraka kuwahi kazini kutokana na kuamka muda mbaya, baada ya kujiandaa aliongozana na rafiki yake. Njiani rafiki yake alimuuliza swali lililozidi kumchanganya. “Jana nilijua unalala kazini, vipi Wahindi wako wamekuleta na gari nini?” “Wala.”SASA ENDELEA…
Roy na Jeff wameshaweka mipango yote sawa, tayari Jeff ameshampatia Roy milioni sita kwa ajili ya kazi ile. Safari ipo njiani, Jeff yupo na mpenzi wake Davina wanazungumza. Kitu cha kushangaza sana, Davina anaonekana hana imani kabisa na ile safari ya mpenzi wake. Je, nini kitatokea? Endelea kufuatilia...
Nilikaa sehemu ambayo kulikuwa na nafasi ya mtu mmoja, yule mtu niliyekwenda naye sikumwona tena alikopotelea. “Bwaba umekuja huku, uko tayari kwa lolote?” Aliniuliza mzee wa kanisani ambaye sikuwa na mazoea naye. “Kwani hapa ni wapi?” Nilihoji. “Hapa ni kwa wachawi.” “Wachawi!” “Eee, umekuja kwa wachawi, kazini kwetu, karibu.” Alipomaliza kusema, alikaa chini, akasimama sasa yule mzee ambaye siku ile kanisani walipoingia wale watu wawili wa ajabu, yeye alikaa katikati yao. SASA ENDELEA…