Shakila msichana aliyekuwa mama ntilie anajikuta akiwatesa watoto wa mke mwenza ambaye alikufa kwa ajili ya gari, hakumbuki aliapa mbele ya mumewe kuwa asingewatesa watoto na angewalea kama wanawe kwasababu anawapenda kama anavyompenda mumewe. Ni watoto wadogo wanaoteseka na kunyanyasika maishani mwao wakilia na kuweweseka kutokana na baba yao kusafiri mara kwa mara kwenda mikoani kufanya biashara ya mahindi.Je, nini hatima ya watoto hao wasio na kosa?...
KUMRADHI MSOMAJI Katika toleo lililopita kwenye mfululizo wa makala haya, tulichanganya simulizi iliyowahi kutolewa katika matoleo yaliyopita, hivyo kusababisha usumbufu kwako msomaji. Tumelifanyia kazi hilo na tunaahidi kutorudia kosa ili kukufanya uendelee kuongeza kitu kipya katika simulizi hii ya kweli.
Ili kukufanya msomaji uwe sambamba na msimuliaji Zubeda Ruvanga, tunarudia sehemu ambayo ilisababisha kuvurugika kwa mtiririko wa stori na baada ya hapo, tunbaahidi hakutakuwa na mvurugiko mwingine mbele ya safari.
Zubeda Ruvanga, mwanamke mwenye umri wa miaka 38, anasimulia mateso aliyokumbana nayo tangu akiwa mtoto. Wachawi walianza kumpa tabu za maisha tangu akiwa darasa la tatu kwenye Shule ya Msingi Mwandiga Kigoma. Tunaanzia pale alipokuwa akiingiliwa na mwanaume ambaye hakumtambua kutokana na kupoteza uwezo wa kuona. Alikuwa anatoa harufu mbaya na alimpa usumbufu mkubwa. Endelea...
Wakati Julieth akiwa tayari kuwapeleka akina Sifael katika chumba cha Patii, ghafla wanasikia amri kutoka watu waliokuwa mbele yao, mikononi mwao wakiwa na bunduki! Walikuwa chini ya ulinzi. Je, nini kitatokea? Kalamu ya msimulizi wako inamwaga wino...
Mpenzi msomaji kijana Bakari anazidi kusimulia jinsi alivyofundishwa na babu mmoja alipokwenda Zanzibar kutafuta maisha. Wiki iliyopita nilisimulia jinsi alivyokwenda kuhudhuria katika kikao cha wachawi kilichofanyika nchini Nigeria. Baada ya kurejea Zanzibar, siku nyingine walikwenda kwenye mkutano wa wachawi uliofanyika Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza, mara ya tatu kwa kutumia ndege za kichawi (ungo) walikwenda kwenye kikao cha wachawi huko Mpanda Rukwa.
Akiwa katika kikao hicho, mmoja wa wazee watatu ambaye alikuwa kiongozi alimfutata sehemu aliyoketi na kumfahamisha kwamba walifika pale kutoka mikoa ya Tanga, Shinyanga na Mwanza kwa ajili yangu baada ya kusikia habari zangu hivyo nao walitaka kutoa baraka zao. Baada ya kunieleza hivyo, mzee huyo alisema nao walihitaji kunifundisha baadhi ya mambo ya kichawi. Je, ni mambo gani hayo? Ungana na Kulwa Mwaibale katika mkasa huu wa kweli…
Machozi yaliendelea kumiminika machoni mwao, wakiwa wamekumbatiana, kila mtu alikuwa akishangaa sana tukio lile, hakuna aliyekuwa aliyetarajia kwamba Mzee Muddy angerejewa na fahamu...
miezi michache baada ya ndoa yake, mama wa kambo anawachukia watoto wa mumewe aliowakuta na zaidi anawanyima chakula cha mchana na kuwanyima nauli za kwenda shule na kuwafanya watoto watembee umbali mrefu wakati mwingine walishindwa kwenda shule. Je, nini kitaendelea fuatilia habari hii ya kusisimua utajifunza jambo.... Nilikuwa mama katili katika familia yetu, mtoto huyo niliyempiga vibao na viboko bila kosa lolote alilia sana akiniambia namuonea ingawa sikujali nilipenda kusikia hivyo, kikubwa nilimwambia ole wake amwambie baba yake kwani ningemnyonga...
Zubeda Ruvanga mwanamke mwenye umri wa miaka 38, anasimulia mateso aliyokumbana nayo, tangu mtoto wachawi walianza kumpa sababu za maisha tangu akiwa darasa la tatu kwenye Shule ya msingi Mwandinga Kigoma. Ilipoishia wiki.
Hata hivyo, kwa sababu nilikuwa sioni, ilibidi niyanuse yale majimaji ili kubaini kama kweli ilikuwa ni damu. Mungu wangu! Ilikuwa kidogo nitapike. Yale majimaji yalitoa harufu kali mithili ya kitu kilichooza. Nilipata shida kujua kama yale yalitoka mwilini mwangu au kwa yule mwanaume...
Mpenzi msomaji, kijana Bakari anaendelea kusimulia mkasa aliokumbana nao wakati akitafuta maisha huko Bububu Zanzibar ambapo babu mmoja alimfundisha uchawi. Wiki iliyopita nilisimulia jinsi alivyopelekwa kwenye makazi ya Rusifa (Shetani) na gwiji la wachawi lililoko nchini Malawi. Akiwa mbele ya Rusifa, Rusifa alimueleza jinsi anavyosikitishwa sana na watu wanaomsaliti baada ya kufundishwa uchawi na kupewa vitendea kazi kwa kuvipeleka makanisani. Pia kijana huyo alisimulia jinsi alivyosafiri kwa ungo kwenda kuhudhuria mkutano wa kichawi uliofanyika Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza na nchini Nigeria. Je, nini kilifuata na nini kilitokea mpaka Profesa Vibuyu akapewa matunguri ya uganga na sasa anawasaidia watu wengi? Ungana na Mwandishi Wetu KULWA MWAIBALE katika mkasa huu wa kusisimua…
Alihisi mwili mzima ukijaa maji, ilikuwa ni jasho likimchukuruzika kwa kasi, woga ukamwingia na hakujua nini kingefuata mbele yake! Katika maisha yake hakuwahi kuona maajabu ya aina ile, kufika ujinini pekee kulimstaajabisha sana, lakini alijaribu kuwaza ikiwa yale majini yangeamua kumuua au kumtumia kwa kazi ingekuwaje?...
Itaendelea wiki ijayo Nilikuwa mama katili katika familia yetu, mtoto huyo alilia sana na kikubwa nilimwambia ole wake amwambie baba yake kwani ningemnyonga. Nilimuonyeshea kisu na kumwambia hicho ndicho kingemkata shingo. Aliitikia kwa kichwa kuwa asingesema jambo lolote, angebaki kimya. Nilimnasa kibao tena, ukiniuliza mtoto wa mke mwenzangu alinikosea jambo gani hata kesho siwezi kujibu zaidi ya kumuona mtoto mtukutu na ndivyo moyoni nilivyozidi kumchukia na kumuona asiyena haki ya kuishi kama mtoto....
Msichana mama ntilie anakutana na mfanyabiashara wa mahindi na kujikuta wakiwa marafiki na hatimaye kufunga ndoa, wanafika jijini Dar es Salaam ambako bwana Abed anaishi na wanawe wawili baada ya mkewe kufariki kwa ajali, hapo ndipo Shakila anapoanza kuwachukia watoto wa mumewe aliowakuta. Je, nini kitaendelea? Fuatilia habari hii ya kusisimua utajifunza jambo....
Zubeda Ruvanga mwanamke mwenye umri wa miaka 38, anasimulia mateso aliyokumbana nayo, tangu mtoto wachawi walianza kumpa sababu za maisha tangu akiwa darasa la tatu kwenye Shule ya msingi Mwandinga Kigoma. Ilipoishia wiki iliyopita... Lakini yule mtu hata yeye, hilo hakuona ni kikwazo, aliendelea kunibana mdomo kwa nguvu, alinilazimisha nitoe ulimi nje, maumivu yalipozidi, nilitoa ulimi nje kisha aliunyonya kwa mbwembwe. Alichukua muda mrefu kumaliza na kuna kipindi nilidhani hatomaliza. Sasa endelea...
Mpenzi msomaji, kijana Bakari anaendelea kusimulia mkasa aliokumbana nao wakati akitafuta maisha huko Bububu Zanzibar ambapo babu mmoja alimfundisha uchawi. Wiki iliyopita nilisimulia jinsi alivyopelekwa kwenye makazi ya Rusifa (Shetani) na gwiji la wachawi lililoko nchini Malawi. Akiwa mbele ya Rusifa, Rusifa alimueleza jinsi anavyosikitishwa sana na watu wanaomsaliti baada ya kufundishwa uchawi na kupewa vitendea kazi kwa kuvipeleka makanisani. Je, nini kilifuata na nini kilitokea mpaka Beka kawa mganga wa jadi anayewasaidia watu wengi? Ungana na Mwandishi Wetu KULWA MWAIBALE katika kisa hiki cha kweli…
Wakati mzee Muddy akionekana mgonjwa aliyelazwa katika hospitali ya Bombo, ukweli halisi ni kwamba mzee huyo alikuwa mzima wa afya njema ila alikuwa amesafirishwa kimazingira hadi ujinini! Akakutana na msichana aliyejitambulisha kwake kwa jina la Zahara, ambaye alimtaka waongozane kwa ajili ya kwenda kwenye kikao. Mzee Muddy akasita! Yule msichana (jini) akazidi kumuamrisha, bado mzee Muddy hakuwa tayari kuamini macho yake kwamba alikuwa ujinini. Je, nini kitatokea? Mwandishi Wetu JOSEPH SHALUWA anakuletea stori kamili...
Maisha ya Sebastian yanakuwa magumu baada ya kuzaa na dada yake aliyekuwa anatafuta utajiri wa kichawi na baadaye kushindwa kumudu masharti na hatimaye, kuuawa na majini yake; mtoto aliyezaa na dada yake anatokwa na damu bila kupata mchubuko wowote na kubwa zaidi mtoto huyu wa ajabu anatokwa udenda, hata hivyo, wakati Sebastian akihangaika huku na kule anapata mdhamini wa kumsaidia kumtibu na kumsomesha kwasababu anahitaji kusomea Upadri, huku kidonda horoni akiona amempa mama yake mzazi ujauzito.Je, nini kitaendelea? Fuatilia.....