Nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kuweza kunipa nguvu na afya kwa siku ya leo ili niweze kuwaandikia haya nitakayoandika. Ndugu zangu, sina budi kukiri kwamba waliosema siasa ni mchezo mchafu kwa kweli hawakudanganya. Nakiri kwamba usemi huo kweli!...
NIMESOMA habari yenye kichwa cha habari “Mungai alimsaliti Sugu” kwenye gazeti la Dimba la Jumapili ya Machi 7, 2010, ambayo kwa mtazamo wangu naona ina lengo la kupotosha ukweli na ndio imenisukuma nipasue jipu hili. Hebu ndugu msomaji fumba macho hapo ulipo ufikirie mifano miwili ifuatayo:...
NDUGU zangu nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kuweza kuniweka mzima wa afya leo mnaponisoma katika safu hii. Niwakumbushe tu kwamba wiki iliyopita Rais Jakaya Mrisho Kikwete aliwaagiza maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, (Takukuru) kuwashughulikia ...
Hii ni nchi yetu, Hii ni ardhi yetu, Hapa ni kwetu sote, Kamwe hatutakiwi kupakatia tamaa, Hata kama kuna wachache wanaotuvunja moyo. Lazima tufanye kila linalowezekana, Kila mmoja wetu ajisikie kudaiwa na nchi yake hatimaye kutimiza wajibu wake...
Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne yametoka, nimekaa ofisini kwangu nina gazeti la Dar Leo mikononi nikisoma na kuyaangalia matokeo hayo, si kuangalia tu bali pia najaribu kulinganisha matokeo ya shule za Sekondari za Binafsi na serikali, inasikitisha!...
Miongoni mwa mambo ambayo namshukuru Mungu kwa kunipa ni nafasi ya kukutana na vijana wa nchi hii na kuongea nao bila kujali Itikadi zao za kisiasa, rangi za ngozi zao, dini nk. Mambo haya kwangu mimi huwa hayana maana kubwa sana, cha muhimu kwangu ni Utanzania na Uzalendo wa kweli wa mtu aliyesimama mbele yangu hata kama tunatofautiana kwa vipengele nilivyovitaja hapo juu...
Hivi karibuni nilisoma kupitia vyombo vya habari juu ya askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) MT. 74670 Koplo Katarama aliyehukumiwa kwenda jela miaka kumi na mbili kwa kosa la kumpiga askari wa Kike wa Usalama barabarani Namba 4116 Sajini Wegesa! Ingawa askari huyu anakwenda kutumikia kifungo kwa miaka yote hii, bila shaka ana familia, lakini niliipokea hukumu hii kwa mikono miwili na kusema hili ni fundisho kwa vijana wetu wa Jeshi letu la Wananchi wa Tanzania...
Namshukuru Mungu, Ni mwaka mpya wa 2010, mwaka ambao Watanzania wamejiandaa kwa Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge. Ni mwaka ambao nafasi ya mtu wa kawaida kumwadhibu mtu wa juu imewadia, mwaka ambao Watanzania wengi watauza haki yao ya Kikatiba na kuchagua viongozi wasiofaa kwa sababu tu wamepewa kitu fulani na kuteseka kwa miaka mingine mitano...
“Watanzania wanataka kujua mwisho wa mjadala huu kwa sababu kubwa mbili, moja kashfa yenyewe ya Richmond imeichafua serikali yao na pili kamati teule ya Bunge imetumia mamilioni ya fedha kufanyia uchunguzi na kukusanya taarifa ya jambo hilo."...
Nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kuniwezesha kusherehekea Sikukuu ya Krismas nikiwa salama tena wa afya tele! Wasomaji wote wa safu hii nawapa mkono wa Krismas nikitumaini kuwa nanyi Mungu amewalinda. Pia niwashukuru kwa kuendelea kutuunga mkono kwa kusoma magazeti yetu kwa kipindi chote cha mwaka 2009...
Namshukuru Mungu, Ndugu zangu, Yanayotokea nchini mwetu hivi sasa, kama Tanzania ingekuwa ni mwili wa mwanadamu basi kila kukicha tungesikia mtu huyo akisema naumwa kichwa, viungo, nina homa kali, naharisha nk. Ingawa tutakuwa hatujagundua kinachomsumbua mtu huyu ni nini, lakini kelele zake hizi zinatosha kabisa kuonesha kwamba mtu huyu anaumwa!...
Namshukuru Mungu, Ingawa watu wengi wanadai kwamba chanzo cha vurugu na mtafaruku ambao umekuwa ukitokea ndani ya Chama Cha Mapinduzi siku za hivi karibuni ni matokeo ya majeraha ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, binafsi bado sijaelewa vizuri undani wa dhoruba hii, ila bado naifanyia kazi kwa nguvu kubwa ingawa sababu iliyotajwa pia inaweza kuwa na ukweli...
Namshukuru Mungu, ZIKIWA zimebaki saa chache tu kufika tarehe 9, Desemba siku ya kuadhimisha Uhuru wa nchi yetu, tukiwa tunatimiza miaka 48 ya uhuru wetu nimeona ni vyema nami kama Mtanzania niseme yangu machache nikitimiza wajibu wangu. Ni miaka 48 ya Uhuru, hakika hii ni miaka mingi ambayo tumesafiri pamoja kama Watanzania, tukiwa tumepitia awamu tatu za uongozi kabla ya kuingia hii ya nne iliyo chini ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete, aliyeingia madarakani kwa ushindi wa asilimia 80 ushindi mkubwa kuliko mwingine wowote katika historia ya nchi yetu...
KUMRADHI: Wiki tatu zilizopita tulikuwa tukichapisha mfululizo wa maneno kutoka hotuba iliyotoka kwenye kitabu cha Nyerere kilichoitwa ‘TUJISAHIHISHE’ kilichotolewa Dar es Salaam Mei 1962, tulipomaliza, kwenye sehemu ya kutambua kazi hiyo, hatukueleza kwamba ndani ya machapisho hayo tulibadili maneno TANU, WanaTANU na wasio WanaTANU kwenda CCM na WanaMtandao na wasio WanaMtandao. Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza katika hilo.Mhariri...
SHAMBA letu kama halikutoa mavuno ya kutosha, jibu lilikuwa wazi: au limerogwa au ni amri ya Mungu. Watoto wetu walipokuwa wagonjwa daima jibu lilikuwa rahisi au wamerogwa au ni amri ya Mungu. Nyumba yetu ilipopigwa radi ikaanguka, jibu lilikuwa rahisi: au ni uchawi au amri ya Mungu...