Hivi, vibarua kama hawa hulipwa shilingi ngapi zinazowafanya wakubali kufanyakazi za ujenzi hatari kama hivi? Angalia urefu wa jengo na mahali aliko na jinsi alivyo kuwa hana kifaa chochote cha usalama, ina maana akiteleza na kuanguka amekufam, just like that!
Mkereketwa ‘namba one’ wa Machozi Band akisakata rhumba ndani ya ukumbi wa Zhong Hua Garden jijini Dar es Salaam wakati bendi hiyo ilipokuwa ikiporomosha burudani mfululizo kama ilivyo kawaida yake.
Jamaa huyu naye hakuwa nyuma kuonyesha ‘staili’ za kibaunsa na kareti ndani ya ukumbi wa Msasani Beach Club uliopo Kawe jijini Dar es Salaam ambapo bendi ya Akudo Impact ‘Vijana wa Masauti’ ilikuwa ikimwaga burudani mahari hapo
Kampuni ya simu za mkononi ya Zain imeandaa tamasha kubwa la Wasanii wa Sanaa mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na muziki, uchongaji, uchoraji, nk, linalotarajiwa kufanyika Machi 20 mwaka huu, katika Uwanja wa ‘Nafasi Arts Space’ uliopo Mikocheni jijini Dar.
Meneja Uhusiano wa Zain, Muganyizi Mutta, akiwatangazia tamasha hilo wanahabari (hawapo pichani) waliofika kwenye ofisi za kampuni hiyo zilizopo Kinondoni Morocco jijini Dar, kulia ni Mkurugenzi wa Trinity Communication, Sauda Simba na Fred Halla.
Mkurugenzi wa kampuni ya Trinity Communication, Sauda Simba, akionyesha albamu yake ya pili hiitwayo ‘Sauti ya Sauda’, ambayo ataizindua katika tamasha hilo.
Mkali wa michoro, Neema Kambona, akionyesha sanaa yake ya uchoraji.
Afisa Habari wa Zain, Leticia Kaijage, muda wote alihakikisha hapitwi na kitu ili kuwamegea wanahabari waliochelewa.
Mtaalamu wa kuchonga vinyago, Mandale Mwanyekwa ‘Big Mama’ akielezea hisia zake zilivyomtuma kuchonga kinyago anachofanana nacho. Kinyago hicho amekichonga bila mikono akipeleka ujumbe kwa mwanamke wenye ulemavu wa ngozi (albino) aliyefanyiwa ukatili wa kukatwa mikono mwaka jana.
Kinyago hiki kitakuwa miongoni mwa kazi zake atakazo kuwanazo siku hiyo.
TAFADHALI SOMA HII TAARIFA AMBAYO MDAU WA NETWORK HII AMETULETEA, KILA MMOJA WETU AWE MWANGALIFU NA WATU KAMA HAWA ,TAFADHALI USISITE KUTULETEA TAARIFA YA MEMBER YOYOTE MWENYE NIA KAMA HUYU WAKUJIITA SARAH, HAWA NI MATAPELI NIMESHA WABANNED WENGI TU. NAPENDA KUCHUKUA NAFASI HII KUKUSHURU NDUGU ANDY KWA TAARIFA HII NAAMINI TAYARI AMESHA CONTACT WENGI KATIKA MTINDO HUU. KWA SASA TAYARI TUMESHA MUONDOA.
Issue:Fraud
Additional Information:Am concerned about the behaviour of one of your member. Kuna member ambaye ni female na profile yake inaonyesha kuwa anaishi New York. Nimegundua within two days ya kuwasiliana naye..this particular person ana-fit profile ya scam artist! Nasema hivyo kwa sababu...in two days period ameniambia kwamba yeye ni mkimbizi kutoka DRC kwa sasa anaishi kwenye camp ya wakimbizi nchini Senegal. She goes on to say that ..baba yake alikuwa advisor wa former president wa DRC and that wazazi wake walipigwa risasi na askari during the war kule DRC...na kwamba she was the only child and the only one to survive. She further claim that, her Father left her with a lump sum of money in the WILL...and that pesa zake zipo kwenye account in a European bank, lakini hawezi, according to her story, kuzitoa. And this brings me to suspicion...Anataka nimpe my bank account hapa USA so that she can transfer dola million mbili mia nne, BUT once the funds are deposited into my bank..she will let me keep half and and wants the remaining half to be send to her in the senegalese refugees camp. The letter goes on..and on.. with numerous bogus explainations. My intention here is to alert the GFAMILY to be wary of this particular member. P'se, alert your members not to fall in the trap. Perhaps some members might have been subjected to this kind of scam and are shying away! P'se, try to inquire from members who have befriended a member named SARAH OF NEW YORK AND SEE WHAT THEY SAY ABOUT THEIR FRIENDSHIPS. Hii site is a good forum kwa Watanzania , tusiwaruhusu watu watuharibie kwani sisi wabongo ni watu wenye mapendo, haki na urafiki. Asante, Andy.
Sehemu ya maonyesho ya bidhaa na huduma za intaneti zinatolewa na Zantel.
Wageni waalikwa wakipewa maelekezo na wafanyakazi wa Zantel wakati wa hafla ya maonyesho ya bidhaa na huduma za intaneti zinazotolewa na kampuni ya Zantel.
Chief Commercial Officer wa Zantel Bw. Norman Moyo akiwahutubia wageni waalikwa wakati wa hafla ya maonyesho ya bidhaa na huduma za intaneti zinazotolewa na kampuni ya Zantel.
Meneja Maendeleo ya Biashara Zantel Bw. Michael Magambo akizingumzia bidhaa na huduma za intaneti zinazotolewa na Zantel wakati wa hafla ya maonyesho iliyofanyika jana jioni. Zantel, wakishirikiana na kampuni za Emitac Mobile Solutions na Research In Motion (RIM) wameanzisha huduma ya Blackberry nchini. Huduma ya Blackberry inaunganisha simu pamoja na softwares za kumuwezesha mteja mteja kupata huduma ya intaneti, barua pepe, ujumbe mfupi, kupiga au kupokea simu, kalenda pamoja na uwezo wa kutuma au kupokea picha na video. Wateja wa Zantel sasa watafaidi huduma hii ya simu za Blackberry kuwasiliana na ndugu, jamaa na marafiki na kupata habari wanapokuwa safarini au shughuli binafsi. “Zantel ikishirikiana na
Baada ya Kocha wa Simba Mzambia, Patrick Phiri kuiwezesha klabu hiyo kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom, huku Kocha wa Yanga Kosta Papic akionekana kuleta mapinduzi katika soka la wachezaji wa Yanga, kumeibuka ushindani kwa mashabiki kuwa nani ni mkali kati yao...
Msanii mkongwe katika sanaa ya uigizaji na filamu hapa bongo, Ivony Cherly a.k.a Monalisa amemfunika staa mwenzake katika 'Industry' ya filamu hapa bongo, Ndumbangwe Misaya a.k.a Thea, kwa kujizolea jumla ya asilimia 63 na kumwachia mpinzani wake asilimia 37 tu ya kura zote zilizopigwa na wadau wa burudani duniani kote kupitia mtandao huu pendwa.
Bliss [~2000] Bliss is the name of a photograph of a landscape in Napa County, California, east of Sonoma Valley. It contains rolling green hills and a blue sky with stratocumulus and cirrus clouds. The image is used as the default computer wallpaper for the "Luna" theme in Windows XP. The photograph was taken by the professional photographer Charles O'Rear, a resident of St. Helena in Napa County, for digital-design company HighTurn. O'Rear has also taken photographs of Napa Valley for the May 1979 National Geographic Magazine article Napa, Valley of the Vine. O'Rear's photograph inspired Windows XP's US$ 200 million advertising campaign Yes you can.
A married woman was having a really nice time with one of her boyfriends when there was a sudden knock on the door. Thinking that it was her husband, she instructed the man to jump into the ceiling only to find it was another boyfriend.
When the 2nd boyfriend was about to make love to her, the real hubby came. Boyfriend 2 had no other option except to jump into the ceiling also. "How are we getting out of here ?" asked # 2 to #1 "I do not know about you, for me I am going as soon as the hubby starts making love to the wife.
When the time came, # 1 jumped naked from the ceiling landed on the bed and said, "I am Jesus, God shall bless you with a baby girl! He quickly vanished.
Saleh Ally, ambaye ni Mhariri Kiongozi wa gazeti la michezo na burudani nchini Tanzania, Championi, akiwa katika darasa linaloendeshwa na AFP jijini Nairobi kuhusu masuala mbalimbali ya uandishi wa kisasa wa stori za michezo na hasa zile za wakati wa Kombe la Dunia linalotarajiwa kufanyika nchini Afrika Kusini baadae mwaka huu. Kulia kwake ni mwandishi wa habari mwenzie, Mwani Nyangasa kutoka gazeti la The African la New Habari Corp na anayeonekana kwa mbali ni mwalimu, Allan Kelly kutoka Shirika la Habari la Ufaransa (AFP). katika darasa hilo, AFP na FIFA walitoa nafasi kwa Watanzania wawili tu, lakini limeahidi kuwapa nafasi wandishi wengine mwakani ili kuimarisha uandishi wa habari za michezo.
Hali ya hewa ya jiji la Nairobi kwa sasa imekuwa ikibadilika mara kwa mara, ambapo wakati mwingine huwa joto na wakati mwingine baridi.
Hii Nairobi Hospital iliyoko katika eneo la Hurington jijini Nairobi Kenya. Kwa siku, hospitali hii hupokea zaidi ya wagonjwa 10 kutoka nje ya Kenya, ina madaktari bingwa wa magonjwa ya kila aina na ni hospitali yenye mfano wa kuigwa kwa nchi za Afrika Mashariki.
Mchana wa leo, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi Ruth Mollel amezungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari, Maelezo, kuzungumzia mambo mbalimbali yanayohusu muungano, ambapo kwa ujumla ameelezea kuwa hakuna matatizo kama watu wengi wanavyoamini, na akasisitiza kuwa kila kitu kiko shwari na muungano utaendelea kuwepo.
Bi Ruth Mollel akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari.
Hapa akisisitiza kuwa Zanzibar kuwa na bendera yake na wimbo wa taifa haimaanishi kuwa tayari imejitenga kwani bado inatambuliwa kimataifa kama sehemu ya Tanzania...
Saleh Kupaza (kushoto) akibadilishana mawazo na mwanamuziki mwenzake, Janeth Isnika katika ofisi za ASET Kinondoni jijini Dar es Salaam.Tukio hilo limenaswa leo.
Khaleed Chokoraa (kushoto) akiteta jambo na mpiga gitaa wa bendi hiyo, Emmanuel Mabele muda mfupi kabla ya kuanza mazoezi.
Mkali wa miondoko ya Dansi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambaye hivi sasa kazi zake anafanyia nchini Tanzania katika Bendi ya Akudo Impact ‘Vijana wa Masauti’ Christian Kwete Bella, hivi karibuni alipata pigo kubwa baada ya kufiwa na kaka yake mpendwa, Frank Kwete Bella aliyekuwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo kwa muda mrefu, Frank alifariki dunia Alhamisi iliyopita na kuzikwa jana huko Kongo ambapo jana wasanii wote kutoka Kongo walikusanyika ndani ya kambi ya Akudo Impact kwaajili ya kuomboleza kwa pamoja na msanii mwenzao.
Baadhi ya waombolezaji waliojumuika pamoja na Chiristian Bella (wa kwanza kulia) ambaye ni mfiwa wakipata mlo.
Baadhi ya wasanii wakiwa na mfiwa, Christian Bella wakipeana hai baada ya kukutana msibani hapo.....
Mchana wa leo, wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania, TRL chini ya Chama cha Wafanyakazi wa Reli nchini (TRAWU), wamefanya mkutano kujadili mambo mbalimbali yanayowahusu, hususani mgogoro mkubwa uliokuwa unatingisha nchi, kati ya serikali na mwekezaji ambaye ni kampuni ya RITES kutoka India.
Katika kikao cha leo, mengi yamezungumzwa, kubwa ikiwa ni kuipongeza serikali kwa kuamua kununua hisa zote za Kampuni ya Rites na kurejesha umiliki na uendeshaji wa shirika hilo muhimu mikononi mwake. Wafanyakazi hao wameipongeza serikali kwa kusikia kilio chao, ingawa wameitahadharisha kuwa makini na mikataba ya uwekezaji kama wa RITES ambao wameeleza kuwa ulikuwa ukiipeleka TRL kaburini.
Mwenyekiti wa Chama cha wafanyakazi wa Reli nchini (TRAWU) Bwana Bakari Kiswala akizungumza jambo katika kikao hicho.
Katibu Mkuu wa TRAWU, Bwana Sylivester Rwegasira ndiyo aliyekuwa mzungumzaji mkuu katika kikao hicho kilichofanyika kwenye moja ya karakana za TRL, mkao makuu jijini Dar es Salaam.
Kikao kilitanguliwa na dua kutoka kwa wakristo na waislamu...