Tembelea... |
 |
Kalenda |
 |

Marafiki wetu |
 |
Habari Zilizopita |
 |



  
Nani Yupo / Alikuwepo |
 |
|
|
 |
|
|
 |
 |
|
IFM KIDEDEA MISS HIGHER LEARNING
|
photos |
|
|
 |
Chuo cha Usimamizi wa fedha cha IFM cha jijini Dar, kimeibuka kidedea katika Shindano la kumsaka mlimbwende wa Vyuo Vikuu nchini, Miss Higher Learning, baada ya Mwanafunzi wa chuo hicho, Betrice Lukindo, kutwaa taji hilo usiku wa kuamkia leo. Wakati Betrice akibatizwa umalkia wa Vyuo Vikuu nchini, Linda Mzinga kutoka Chuo cha Ustawi wa Jamii, Kijitonyama amechukua nafasi ya pili na Doris Donatus kutoka Dar es Salaam Institute of Technology (DIT) akiibuka mshindi wa tatu. Kwa ushindi huo, Magreth amepata tiketi ya moja kwa moja ya kujiunga na Kambi ya Miss Tanzania msimu huu, tayari kwa kuwania taji la Miss Tanzania, 2009/10. Shindano hilo lilifanyika ndani ya viunga vya Karimjee katikati ya jiji la Dar es Salaam, lililosababishwa kwa udhamini mkubwa wa Mtandao wa simu za mkononi wa Vodacom, Global Publishers Ltd, Clouds FM, Ndege Insuarance, kinywaji cha Overmeer na wadhamini wengine kibao.  Miss Vodacom Higher Learning 2009/10, Betrice Lukindo (katikati) akiwa katika picha ya pozi na mshindi wa pili, Linda Mzinga (kulia) na kushoto ni Doris Donatus, mshindi wa tatu.  Hii ndiyo ilikuwa Top 5.  Majaji, kutoka kushoto ni Miss Tanzania mwaka juzi , Jokate Mwegelo, Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashimu Lundenga ‘Anko’ na Miss Tz mwaka jana, Nasreen Mohamed, wakiwa makini kutazama warembo (hawapo pichani).  Warembo wakicheza staili ya Mugongo Mugongo jukwaani baada ya kupanda kwa mara ya kwanza.  Kundi la sanaa la International Youth Ferowship, likikonga nyoyo za wadau wa urembo kwa ngoma ya kichina kabla ya mrembo kutangazwa.  Wanenguaji wa bendi ya muziki wa dansi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ wakivamia jukwaa wakati wa shindano hilo.  Nani amesema wanenguaji siyo masister Duu? Hawa mamiss ila ni wanenguaji wa Twanga wakiwa chobingo wakijipodoa kwa ‘Mapouda’  Staa wa Kundi la ucheshi la Orijino Komed ‘Masanja Mkandamizaji” akiinama kukwepa kamera baada ya kubambwa ukumbini hapo akishuhudia mchuano mkali wa walimbwende hao. PICHA:CHRISTOPHER LISSA/GPL |
|
 |
 |
|
MBILI ABEL APAGAWISHA DAR
|
photos |
|
|
 |
Usiku wa kuamkia leo mkongwe wa muziki kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mbili Abel alifanya makamuzi ya kufa mtu katika onesho lililofanyika Ukumbi wa Police Oficers Mess Oysterbay, jijini Dar es Salaam. Katika onesho hilo mwanamuziki huyo alisindikizwa na ‘Wazee Sugu’ The Akapitale Band chini ya mkongwe, Kikumbi Mwanza Mpango 'King Kikii'  Mbili Abel akifanya majambozi jukwaani  Hapa akiserebuka na wacheza shoo wake  Mashabiki wakichizika na vibao vilivyowahi kutamba enzi hizo  Wazee Sugu wakipagawisha na kitambaa cheupeee... Ishara ya upendo  Mashabiki wakichizika kwa kibao cha Wazee Sugu, ‘kitambaa cheupe’ PICHA: RICHARD BUKOS /GPL |
|
 |
 |
|
WASAILIWA WA 'TEARS ON VALENTINE' WAFURIKA OFISI ZA TOLLYWOOD MOVIES
|
photos |
|
|
 |
Wasanii waliochukua fomu za kushiriki kucheza filamu ya Tears on Valentine leo tena wameendelea kufurika katika Ofisi za Tollywood,zilizopo Sinza Bamaga, jijini Dar es Salaam tayari kwa kufanyiwa usaili. Mkurugenzi wa filamu hiyo, Hammie Rajab, ambaye pia ni mmoja wa majaji, amesema kuwa kila kukicha wasanii wamekuwa wakijitokeza kwa wingi hivyo kuwapa wakati mgumu wa kuwafanyia usaili kulingana na ratiba. Aliendelea kusema kwamba mbali na hilo, wamekuwa pia wakishangazwa na uwezo mkubwa wa washiriki hao kwani kila mmoja anaonekana kuwa na kipaji hicho ukizingatia kuwa, wengi wao hajawahi kucheza filamu hata mara moja.  Wasanii wakisubiri kuingia ndani ya ofisi za Tollywood kwa ajili ya usaili.  Waliokaa mezani kutoka kulia ni Hammie Rajab, Mkurugenzi wa Filamu hiyo na kushoto kwake ni Jaji Joseph Shaluwa wakiwatwanga maswali washiriki hao.  Cleopatra 3, mwenye sketi nyeupe, akiwa kwenye moja ya majaribio ya shughuli hiyo na Anither Tibigenda (anayemnyoshea kidole) Kushoto ni Debora Sanga mmoja wa majaji wa Tollywood Movies. Picha zote:Musa Mateja/GPL. |
|
 |
 |
|
BBC Radio 3 - Samba Mapangala at Sauti za Busara 2009
|
photos |
|
|
 |
 If you are lucky enough to hear BBC Radio 3 - then don't miss a special programme recorded during Sauti za Busara 2009 about SAMBA MAPANGALA. It will be broadcast on Saturday 4th July 2009 at 3pm (UK time) - and also available from their archive for a week. More details at [url=http://www.bbc.co.uk/radio3]www.bbc.co.uk/radio3 |
|
 |
 |
|
 |
 Wazungu hawa hawakuona tabu kuburuza begi laola nguo na kukatiza mitaa ya jiji la Dar es salaam kama walivyonaswa na kamera yetu leo mitaa ya Sokoine.  Kufuatia Tangazo la Halmashauri ya Jiji la Dar la kuwataka wamiliki wa majengo kulipia kodi ZA MAJENGO, hivi sasa kumekuwepo misululu mirefu katika ofisi za TRA, karibu kila tawi.  ..Manati mjini hutumika kuwindia nini? Kijana akipita kwenye rodi akijiuzia manati yake!  Unaweza usiamini, lakini anayeingia ndani ya gari hii ni Mohamed Mpakanjia kama alivyokutwa na mpiga picha wetu mitaa ya Magomeni Mapipa alipokuwa akiongea na pedeshee mwenzie Papa Msofe. PICHA: ISMAIL MANG'OLA/GPL |
|
 |
 |
|
TOLLYWOOD TAYARI KWA USAILI
|
photos |
|
|
 |
Kufuatia matangazo yaliyokuwa yakitolewa na kuchapishwa kwenye magazeti mbalimbali ya Kampuni ya Global Publishers & General Enterprises yaliyohusiana na kuomba nafasi ya kushiriki kucheza filamu yaTears On Valentine Day, hatimaye usaili kwa ajili ya kuwapata wasanii watakaofaa kuigiza katika filamu hiyo umeanza katika ofisi za Tollywood zilizoko Sinza Bamaga, jijini Dar es Salaam. Katika usaili huo, waombaji kibao wamejitokeza kama wanavyoonekana pichani.  Wasanii wakiwa nje ya ofisi za Tollywood wakisubiri zamu yao kufanyiwa usaili.  Washiriki wakiwa ndani ya ofisi hizo kwa pamoja wakiteta jambo muda mfupi kabla ya kufanyiwa usaili.  Mratibu wa shughuli hiyo, Hammie Rajab na msaidizi wake, Deborah Sanga wakimfanyia usaili mshiriki Picha zote:Musa Mateja/GPL |
|
 |
 |
|
VITA DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA KWA VIJANA!
|
photos |
|
|
 |
 Maadhimisho ya kupiga vita Madawa ya kulevya duniani yameadhimishwa Bongo na yamewahusisha vijana mbalimbali kwa kuwapima kama kweli hawatumii madawa hayo (Bangi na unga) pamoja na madawa mengine yanayoathiri maisha yao, hapa baadhi ya vijana wa Mwembe Yanga Temeke wakishiriki mchezo wa kukimbiza kuku na aliyemkamata ilikuwa ni zawadi yake.  ...Jamaa wafurahia kuku wao na kutoka nduki  ...mabinti nao hawakuachwa nyuma katika mbi za kuku  Ni kama anasema: nani kasema mboga hamna, cheki bonge la mjogoo huu, siamini kama siku ya leo na mimi narudi nyumbani na kitoweo cha kuitosheleza familia yangu, hata kama tuko kumi, lazima atatosha tu.  Waandaaji wa Tamasha la kupiga vita madawa ya kulebya wakitafakari jambo mara baada ya washiriki wa zoezi hilo kuondoka na kuku bila kuruhusiwa huku Afisa Elimu kata ya Tandika akishuhudia mtanange huo.  Afisa Elimu kata ya Tandika Bi. Beatrice Nyangu, Afisa Elimu kata ya Tandika, akiwashuhudia jinsi vijana wanavyopambana na upigaji vita nadawa ya kulevya katika viwanja vya Mwembe Yanga jijini Dar Es Salaam leo. PICHA NA ISMAIL MANG’OLA / GPL. |
|
 |
|