Tembelea... |
 |
Kalenda |
 |

Marafiki wetu |
 |
Habari Zilizopita |
 |



Nani Yupo / Alikuwepo |
 |
|
|
 |
|
|
 |

 |
|
 |
Mfanyabiashara maarufu ndani na nje ya nchi anayekabiliwa na tuhuma za kufanya ufisadi kwa kuchota zaidi ya bilioni katika akaunti ya mfuko wa madeni ya nje (EPA) leo amewekewa dhamana baada ya kutimiza masharti.  Picha Jeetu akitoka nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar leo mchana. HUU NDIO USAFIRI ALIOTUMIA JEETU LEO Huu ndio usafiri aliotumiwa aliotumia Jeetu kuonmdoka eneo la Mahakama ya Kisutu baada ya kuwekewa dhamana. NYIE MAAFANDE MNAPENDA SANA MRUNGULA. Martha Samwel akiwachamba maafaande wa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa kumuwekea Zengwe na kummnyima dhamana mwanae aliyemtaja kwa jina la Omary. MAMA SASA TUMEKUCHOKA  Bi. Martha akiondolewa na Askari wa Kike wa Jeshi la Magereza eneo la Mahakama ya Kisutu na kupewa onyo la kufanyiwa kitu mbaya kama ataendelea kutoa maneno yasiyofaa. PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS GPL |
|
 |
 |
|
SERA YA KUPAMBANA NA UKIMWI KATIKA VYOMBO VYA HABARI YA ZINDULIWA
|
photos |
|
|
 |
Sera ya kupambana na ugonjwa hatari wa UKIMWI katika vyombo vya habari nchini, imezinduliwa mapema hii leo na Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) Dr. Fatma H.Mrisho. Akizindua Sera hiyo ,Dr.Fatma ametoa wito kwa waandishi wa habari kujenga tabia ya kujiendeleza kielimu ili kujiongezea ufahamu hasa kuhusu masuala ya afya na UKIMWI. Katika hafla fupi ya uzinduzi huo iliyofanyika katika Hoteli ya Kilimanjaro Kempinski Jijini Dar es Salaam, Kampuni ya Global Publishers &General Enterprises Ltd wachapishaji wa magazeti pendwa ya Ijumaa, Risasi, Amani, Uwazi, Championi na Ijumaa Wikienda ilipongezwa kwa kuwa kampuni ya kwanza ya habari nchini, kuunda sera yake binafsi ya kupambana na UKIMWI pamoja na kuanza utekelezaji wa sera hiyo. Akitoa mada katika hafla hiyo Meneja Mkuu wa Global Publishers Abdalah Mrisho alisema kuwa kampuni yake imekuwa mstari wa mbele wa kuhakikisha kuwa wafanyakazi wake wanapata elimu ya kutosha juu ya ugonjwa hatari wa UKIMWI. “Hivi sasa tumeanza utekelezaji wa sera hii na tumejiwekea utaratibu wa kutoa elimu ya UKIMWI kwa wafanyakazi kila siku ya Jumamosi”alieleza Mrisho.  Pichani Dr.Fatma (kushoto) akikata utepe kama ishara ya kuzindua sera hiyo.Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Constela Feature Bi.Halima Sharif . Constela Feuture ni waratibu wa mchakato mzima wa mpango wa elimu ya UKIMWI katika vyombo vya habari wakishirikiana na Chama cha wamiliki wa vyombo vya habari nchini (MOAT) KITABU NDIO HIKI Dr.Fatma akinyanyua juu kitabu cha sera hiyo mara baada ya kuzindua. MRISHO NAE ALONGA Meneja Mkuu wa Global Publishers Abdalah Mrisho, akiwasilisha mada wakati wa hafla ya uzinduzi wa sera hiyo. KUMBUKUMBU MUHIMU: Mkurugenzi wa Constela Features Bi.Halima Sharif (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Meneja wa Global Publishers Abdala Mrisho (kushoto), kulia ni Mhariri mshauri wa gazeti la Uwazi Elvan Stambuli mara baada ya hafla ya uzinduzi huo kumalizika. |
|
 |
 |
|
T MARC YAENDELEA KUMWAGA ZAWADI
|
photos |
|
|
 |
 Mtaalam wa teknolojia na mawasiliano wa T MARC, Bwana Geofrey Millinga (kushoto) akimkabidhi zawadi ya simu ya mkononi Bw. Christopher Lukas, leo mchana baada ya kujishindia Bahati Nasibu ya sikia kengele. DROO YA SIKIA KENGELE HAINA KIFICHO Mshindi wa Droo ya nne ya sikia Kengele, Bwana Masoud Omary katikati akiwatazama Meneja wa SELCOM, Juma Mgori kulia na Mtaalam wa teknolojia na mawasiliano wa T MARC, Geofrey Millinga wanavyochezesha Bahati Nasibu hiyo. Millinga, amewataka watu wote kushiriki Bahati Nasibu hiyo kwa kutuma neno Sikia kengele kwenda 15796 zawadi nono zinaendelea kutolewa ikiwemo pikipiki aina ya Slang. PICHA NA RICHARD BUKOS /GPL |
|
 |
 |
|
HIVI NDIVYO BEN MTOBWA ALIVYOIACHA NYUMBA YAKE
|
photos |
|
|
 |
 Mwili wa Mwandishi mahiri wa magazeti na vitabu Ben Mtobwa ukitolewa ndani ya nyumba yake jana jioni na kwenda kuhifadhiwa kwenye nyumba ya milele nje nyumba yake hiyo. KIFO CHA BEN MANZI KWA WOTE Mtoto wa Marehemu Ben Rabecka (kulia) akifarijiwa kufuatiwa msiba wa baba yake kipenzi. IBADA YA MWISHO YA BEN MTOBWA  Mchungaji Anyisise Mwasandube wa Kanisa la Kibaptist akiongoza ibada ya mazishi ya Ben Mtobwa yaliyoifanyika nyumbani kwake Bunju jijini Dar es Salaam. FAMILIA YA BEN YATOA SHUKRANI  Kaka wa Marehemu Ben Mtobwa aitwae Bazire Mtobwa akitoa shukrani kwa walioshirikiana naye kuanzia ugonjwa mpaka mazishi ya marehemu kaka yake Ben. PICHA NA RICHARD BUKOS /GPL |
|
 |
 |
|
MISS UTALI TANZANIA MWENDO MDUNDO
|
photos |
|
|
 |
 Rais wa Miss Utalii Tanzania Gedeoni Chipungahelo ?Chips? (kulia) akiongea na Waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema hii jana katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo Jijini Dar es Salaam, juu ya Ziara ya Miss Utalii Tanzania 2008 inayotarajiwa kuanza Desemba mwaka huu, yenye lengo la kuhamasisha Utalii, Utamaduni na uwekezaji.Kushoto ni Azizi Chinya ?Papaa Misifa? Mratibu wa ziara hiyo. YATIMA WALIA NA CRAYZ GK Baaadhi ya watoto yatima wa mitaani waliokuwa wamechukuliwa na aliyekuwa msanii nyota wa muziki nchini Gwamaka Kaihula ?king Crayz GK? kushiriki kucheza filamu ya Sauti ya Manka wameibuka na kumsilibia kinoma kuwa amewadhurumu haki zao. Akichonga na mtandao huu mmoja wa watoto hao Emmanuel Rodrick Salewa ?Dogo janja the Solota? (pichani) ambaye alishiriki kikamilifu kucheza filamu hiyo amesema kuwa mpaka sasa hakuna dalili yote ya GK kutimiza ahadi yake ya kuwalipa mafao yao baada ya kukamilisha kazi hiyo. PICHA ZOTE NA CHRISTOPHER LISSA/GPL |
|
 |

 |
|
MAJONZI, SIMANZI, HUZUNI
|
photos |
|
|
 |
Jana Rais JK aliungana na umati uliofurika katika Kanisa la Mtakatifu Martha lililoko Mikocheni jijini Dar es Salaam, kuuaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Vijijini (CCM) ambaye pia ni Mkurugenzi wa kampuni ya Business Times & Printers Mh, Richard Nyaulawa. Mheshimiwa Nyaulawa alifariki nyumbani kwake Kawe jijini Dar Novemba 9, huu baada ya kusumbuliwa na saratani ya ini. KWAHERI SHUJAA WETU Rais JK akiuaga mwili wa Mh. Nyaulawa MAMA SALMA AKIKUMBUKA ENZI ANANYONYESHA  Mke wa Rais JK, Mama Salma Kikwete akiwa amembeba mjukuu wa marehemu Nyaulawa wakati ibada ikiendelea. MUNGU ILAZE ROHO YA MAREHEMU PEMA PEPONI  Rais JK na Mama Salma wakiwa pamoja waombolezaji wengine wakifuatilia ibada ya Mazishi, kulia mke wa Mh. Nyaulawa Bi. Getrude Nyaulawa. BUNGE LIMEPOTEZA KIFAA MUHIMU Naibu Spika wa Bunge Mh, Anna Makinda naye akiuaga mwili wa Mh, Nyaulawa. KAZA BUTI KIJANA Rais JK akimfariji mtoto mkubwa wa marehemu Nyaulawa aitwae Rehule ambaye ndiye Mkurugenzi wa kituo cha redio cha Times FM. PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS /GPL |
|
 |
|