arrowMake Homepage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » photos

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Picha Ya Week ...

Nani Yupo / Alikuwepo

 


 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» Ray C: Mabuzi wa nje mwisho ...
» RICHARD: AKINA NANIHII WANA ...
» Nakaaya mzinzi?
» JOHARI: Mwili wake umepotez ...
» TUMEWABAMBA!
» KUtafuta maisha kumenifanya ...
» REDIHENDED!
» Ngwair kaishiwa mistari ...
» Arsenal, Man, Barca dim ...
» Happy at last (Hatimae ...
» MR II ATUA BONGO!
» Ben Kinyaiya anyanyapal ...
» Simu inavyoweza kukung’ ...
» Ray, Kanumba watishiana ...

 

DAR KILA SIKU CHRISTMAS

photos  
DAR KILA SIKU CHRISTMAS
Mpiga besi gitaa wa kundi moja la taarabu akiwapagawisha mashabiki wake katika onesho lililofanyika ukumbi wa Mango Garden jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo.
PICHA NA RICHARD BUKOS /GPL
    (21 November 2008)
Views: 14 | Maoni (1) |

 

KASEBA ASHINDA MPAMBANO WA MABINGWA

photos  
KASEBA ASHINDA MPAMBANO WA MABINGWA
Bingwa wa Dunia wa Kickboxing mkanda WKL Kg 79, Japhet Kaseba, hivi karibuni alitoka Japan kushiriki shindano la Mabingwa la Dunia na kufanikiwa kuwachakaza vilivyo wapinzani wake, pichani akionesha kombe alilopewa baada ya ushindi na CD iliyorekodiwa mpambano huo.

ACHENI UZUSHI, HAKUNA GOTI NILILOVUNJWA
KASEBA ASHINDA MPAMBANO WA MABINGWA
Wabongo wengine bwana, eti wamemzushia Kaseba amedundwa na kuvunjwa goti katika mpambano wa Mabingwa wa Kickboxing uliofanyika nchini Japan hivi karibuni, pichani mshikaji akiwaonesha waandishi wa habari magoti yake yote mawili baada ya kuzushiwa kuwa goti lake moja amefanyiwa oparesheni baada ya kuumizwa.

PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS
    (20 November 2008)
Views: 57 | Maoni (1) |

 

KATIBU WA TAHLISO KIZIMBANI

photos  
KATIBU WA TAHLISO KIZIMBANI
Katibu Mkuu wa chama cha wanafunzi wa vyuo vikuu nchini, Bwana Julius Mtatiro jana alipandishwa kizimbani kwa tuhuma za kuhamasisha mgomo katika Chuo Kikuu Dar es Salaam cha Mlimani, kupitia chama wanafunzi wa shuleni hapo DARUSO jamaa amewekewa dhamana mpaka Dec. 2 mwaka huu.

KIGOGO WA CCM NYAPINYAPI KWA UFISADI
KATIBU WA TAHLISO KIZIMBANI
Mweka Hazina wa CCM mkoa wa Kigoma, Bw. Shabani Maranda jana ombi lake la dhamana katika kesi ya ufisadi inayomkabili katika Mahakama ya Kisutu liligonga mwamba kurudishwa rumande mpaka kesho.
PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS /GPL.
    (20 November 2008)
Views: 53 | Maoni (2) |

 

HAPO VIPI?

photos  
HAPO VIPI?
Huyu ni muimbaji wa taarabu anayekuja juu kwa sasa, jina lake ni Samira Rashid – hapo vipi?
    (19 November 2008)
Views: 227 | Maoni (7) |

 

MIGOMO

photos  
MIGOMO

MIGOMO

Baada ya waalimu kugoma kuingia madarasani wakidai haki yao, wanafunzi nao wameamua kuingia barabarani kuandamana kuitaka serikali iwatimizie waalimu madai yao ili nao wapate kusoma…kila siku yamekuwepo maandamano ya hapa na pale ya wanafunzi wa shule za msingi jijini Dar es salaam, kama walivyokutwa wanafunzi hawa wa Shule ya Msingi Mbagala Kiburugwa, walisema wanataka kwenda hadi Ikulu..lakini waliishia njiani baada ya kupigwa mkwara na polisi..!.
    (19 November 2008)
Views: 18 | Maoni (0) |

 

JEETU PATEL AACHIWA

photos  
Mfanyabiashara maarufu ndani na nje ya nchi anayekabiliwa na tuhuma za kufanya ufisadi kwa kuchota zaidi ya bilioni katika akaunti ya mfuko wa madeni ya nje (EPA) leo amewekewa dhamana baada ya kutimiza masharti.

JEETU PATEL AACHIWA
Picha Jeetu akitoka nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar leo mchana.

HUU NDIO USAFIRI ALIOTUMIA JEETU LEO
JEETU PATEL AACHIWA
Huu ndio usafiri aliotumiwa aliotumia Jeetu kuonmdoka eneo la Mahakama ya Kisutu baada ya kuwekewa dhamana.

NYIE MAAFANDE MNAPENDA SANA MRUNGULA.
JEETU PATEL AACHIWA
Martha Samwel akiwachamba maafaande wa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa kumuwekea Zengwe na kummnyima dhamana mwanae aliyemtaja kwa jina la Omary.

MAMA SASA TUMEKUCHOKA
JEETU PATEL AACHIWA
Bi. Martha akiondolewa na Askari wa Kike wa Jeshi la Magereza eneo la Mahakama ya Kisutu na kupewa onyo la kufanyiwa kitu mbaya kama ataendelea kutoa maneno yasiyofaa.
PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS GPL
    (18 November 2008)
Views: 79 | Maoni (0) |

 

SERA YA KUPAMBANA NA UKIMWI KATIKA VYOMBO VYA HABARI YA ZINDULIWA

photos  
Sera ya kupambana na ugonjwa hatari wa UKIMWI katika vyombo vya habari nchini, imezinduliwa mapema hii leo na Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) Dr. Fatma H.Mrisho.

Akizindua Sera hiyo ,Dr.Fatma ametoa wito kwa waandishi wa habari kujenga tabia ya kujiendeleza kielimu ili kujiongezea ufahamu hasa kuhusu masuala ya afya na UKIMWI.

Katika hafla fupi ya uzinduzi huo iliyofanyika katika Hoteli ya Kilimanjaro Kempinski Jijini Dar es Salaam, Kampuni ya Global Publishers &General Enterprises Ltd wachapishaji wa magazeti pendwa ya Ijumaa, Risasi, Amani, Uwazi, Championi na Ijumaa Wikienda ilipongezwa kwa kuwa kampuni ya kwanza ya habari nchini, kuunda sera yake binafsi ya kupambana na UKIMWI pamoja na kuanza utekelezaji wa sera hiyo.

Akitoa mada katika hafla hiyo Meneja Mkuu wa Global Publishers Abdalah Mrisho alisema kuwa kampuni yake imekuwa mstari wa mbele wa kuhakikisha kuwa wafanyakazi wake wanapata elimu ya kutosha juu ya ugonjwa hatari wa UKIMWI.

“Hivi sasa tumeanza utekelezaji wa sera hii na tumejiwekea utaratibu wa kutoa elimu ya UKIMWI kwa wafanyakazi kila siku ya Jumamosi”alieleza Mrisho.

SERA YA KUPAMBANA NA UKIMWI KATIKA VYOMBO VYA HABARI YA ZINDULIWA
Pichani Dr.Fatma (kushoto) akikata utepe kama ishara ya kuzindua sera hiyo.Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Constela Feature Bi.Halima Sharif . Constela Feuture ni waratibu wa mchakato mzima wa mpango wa elimu ya UKIMWI katika vyombo vya habari wakishirikiana na Chama cha wamiliki wa vyombo vya habari nchini (MOAT)

KITABU NDIO HIKI
SERA YA KUPAMBANA NA UKIMWI KATIKA VYOMBO VYA HABARI YA ZINDULIWA
Dr.Fatma akinyanyua juu kitabu cha sera hiyo mara baada ya kuzindua.

MRISHO NAE ALONGA
SERA YA KUPAMBANA NA UKIMWI KATIKA VYOMBO VYA HABARI YA ZINDULIWA
Meneja Mkuu wa Global Publishers Abdalah Mrisho, akiwasilisha mada wakati wa hafla ya uzinduzi wa sera hiyo.

KUMBUKUMBU MUHIMU:
SERA YA KUPAMBANA NA UKIMWI KATIKA VYOMBO VYA HABARI YA ZINDULIWA
Mkurugenzi wa Constela Features Bi.Halima Sharif (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Meneja wa Global Publishers Abdala Mrisho (kushoto), kulia ni Mhariri mshauri wa gazeti la Uwazi Elvan Stambuli mara baada ya hafla ya uzinduzi huo kumalizika.
    (18 November 2008)
Views: 2 | Maoni (0) |

 

GLOBAL YATIMIZA AHADI KWA WAFUNGWA

photos  
GLOBAL YATIMIZA AHADI KWA WAFUNGWA
Afisa Utawala wa Kampuni ya Global Publishers, Soud Kivea (Kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Gereza la Ukonga jijini Dar, ACP Samwel Nyakitinya, msaada wa katuni 229 zenye jumla ya miche ya sabuni 2,290 ambazo zimetolewa kwa ajili ya kupewa mche mmoja kila mfungwa wa gereza hilo. Hii ilikuwa ni kutimiza ahadi aliyoitoa Mkurugenzi wa Global Publishers, Eric Shigongo wakati alipoongea na wafungwa hao katika Bonanza liloandaliwa na Global Publishers kupitia gazeti lake la michezo la Championi, Aug 14 mwaka huu.
    (18 November 2008)
Views: 1 | Maoni (0) |

 

MDADI NI BALAA

photos  
MDADI NI BALAA
Shabiki wa Msondo Music Band Iche Mang'enya akiwa amepandishwa midadi na midundo ya bendi hiyo katika onesho lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita ukumbi wa Africentre jijini Dar.

MREMBO AKIGOMBEA BIA KWA STAILI HII
MDADI NI BALAA
Mmoja wa wateja waliokuwa wakipata kinywaji katika Bar ya Royal, akiwa amebinuka baada ya kuanzishwa shindano la wateja kugombea bia katika bar hiyo.
PICHA:RICHARD BUKOS NA MUSA MATEJA.
    (15 November 2008)
Views: 2 | Maoni (0) |

 

T MARC YAENDELEA KUMWAGA ZAWADI

photos  
T MARC YAENDELEA KUMWAGA ZAWADI
Mtaalam wa teknolojia na mawasiliano wa T MARC, Bwana Geofrey Millinga (kushoto) akimkabidhi zawadi ya simu ya mkononi Bw. Christopher Lukas, leo mchana baada ya kujishindia Bahati Nasibu ya sikia kengele.

DROO YA SIKIA KENGELE HAINA KIFICHO
T MARC YAENDELEA KUMWAGA ZAWADI
Mshindi wa Droo ya nne ya sikia Kengele, Bwana Masoud Omary katikati akiwatazama Meneja wa SELCOM, Juma Mgori kulia na Mtaalam wa teknolojia na mawasiliano wa T MARC, Geofrey Millinga wanavyochezesha Bahati Nasibu hiyo.
Millinga, amewataka watu wote kushiriki Bahati Nasibu hiyo kwa kutuma neno Sikia kengele kwenda 15796 zawadi nono zinaendelea kutolewa ikiwemo pikipiki aina ya Slang.
PICHA NA RICHARD BUKOS /GPL
    (14 November 2008)
Views: 7 | Maoni (0) |

 

HIVI NDIVYO BEN MTOBWA ALIVYOIACHA NYUMBA YAKE

photos  
HIVI NDIVYO BEN MTOBWA ALIVYOIACHA NYUMBA YAKE
Mwili wa Mwandishi mahiri wa magazeti na vitabu Ben Mtobwa ukitolewa ndani ya nyumba yake jana jioni na kwenda kuhifadhiwa kwenye nyumba ya milele nje nyumba yake hiyo.

KIFO CHA BEN MANZI KWA WOTE
HIVI NDIVYO BEN MTOBWA ALIVYOIACHA NYUMBA YAKE
Mtoto wa Marehemu Ben Rabecka (kulia) akifarijiwa kufuatiwa msiba wa baba yake kipenzi.

IBADA YA MWISHO YA BEN MTOBWA
HIVI NDIVYO BEN MTOBWA ALIVYOIACHA NYUMBA YAKE
Mchungaji Anyisise Mwasandube wa Kanisa la Kibaptist akiongoza ibada ya mazishi ya Ben Mtobwa yaliyoifanyika nyumbani kwake Bunju jijini Dar es Salaam.

FAMILIA YA BEN YATOA SHUKRANI
HIVI NDIVYO BEN MTOBWA ALIVYOIACHA NYUMBA YAKE
Kaka wa Marehemu Ben Mtobwa aitwae Bazire Mtobwa akitoa shukrani kwa walioshirikiana naye kuanzia ugonjwa mpaka mazishi ya marehemu kaka yake Ben.
PICHA NA RICHARD BUKOS /GPL
    (14 November 2008)
Views: 33 | Maoni (1) |

 

MISS UTALI TANZANIA MWENDO MDUNDO

photos  
MISS UTALI TANZANIA MWENDO MDUNDO
Rais wa Miss Utalii Tanzania Gedeoni Chipungahelo ?Chips? (kulia) akiongea na Waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema hii jana katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo Jijini Dar es Salaam, juu ya Ziara ya Miss Utalii Tanzania 2008 inayotarajiwa kuanza Desemba mwaka huu, yenye lengo la kuhamasisha Utalii, Utamaduni na uwekezaji.Kushoto ni Azizi Chinya ?Papaa Misifa? Mratibu wa ziara hiyo.

YATIMA WALIA NA CRAYZ GK
MISS UTALI TANZANIA MWENDO MDUNDO
Baaadhi ya watoto yatima wa mitaani waliokuwa wamechukuliwa na aliyekuwa msanii nyota wa muziki nchini Gwamaka Kaihula ?king Crayz GK? kushiriki kucheza filamu ya Sauti ya Manka wameibuka na kumsilibia kinoma kuwa amewadhurumu haki zao.
Akichonga na mtandao huu mmoja wa watoto hao Emmanuel Rodrick Salewa ?Dogo janja the Solota? (pichani) ambaye alishiriki kikamilifu kucheza filamu hiyo amesema kuwa mpaka sasa hakuna dalili yote ya GK kutimiza ahadi yake ya kuwalipa mafao yao baada ya kukamilisha kazi hiyo.
PICHA ZOTE NA CHRISTOPHER LISSA/GPL
    (14 November 2008)
Views: 26 | Maoni (1) |

 

Mh. NYAULAWA AZIKWA!

photos  
Mh. NYAULAWA AZIKWA!
..makazi ya milele ya Mh. Nyaulawa....
Mh. NYAULAWA AZIKWA!
..baadhi ya waombolezaji waliohudhuria maziko leo kijijini Inyala.

ILIKUWA NI WIKI YA MAJONZI TASNIA YA HABARI! Mh. Richard Nyaulawa amezikwa mchana wa leo kijijini kwake Inyala, Mbeya na maziko yake kuhudhuriwa na Rais Jakaya Kikwete. Kwake tulitoka na kwake tutarejea, Mungu alilaze Roho yake Peponi - Amen!
    (13 November 2008)
Views: 28 | Maoni (0) |

 

BURIANI BEN MTOBWA!

photos  
Mwandishi wa Habari na Mwandishi wa vitabu mkongwe nchini Tanzania, Ben Mtobwe, aliyefariki mapema wiki hii, amezikwa leo nyumbani kwake Bunju, nje kidogo ya jiji la Dar es salaa. Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi - Amen!

BURIANI BEN MTOBWA!
Marehemu Ben Mtobwa akiagwa na ndugu na Jamaa leo Nyumbani kwake Bunju A, jijini Dar es salaam jioni ya leo

BURIANI BEN MTOBWA!
Rehema ben Mtobwa, ambaye alikuwa mke wa marehemu, akilia kwa uchungu baada ya kumuaga marehemu.
    (13 November 2008)
Views: 14 | Maoni (0) |

 

MAJONZI, SIMANZI, HUZUNI

photos  
Jana Rais JK aliungana na umati uliofurika katika Kanisa la Mtakatifu Martha lililoko Mikocheni jijini Dar es Salaam, kuuaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Vijijini (CCM) ambaye pia ni Mkurugenzi wa kampuni ya Business Times & Printers Mh, Richard Nyaulawa.

Mheshimiwa Nyaulawa alifariki nyumbani kwake Kawe jijini Dar Novemba 9, huu baada ya kusumbuliwa na saratani ya ini.

KWAHERI SHUJAA WETU
MAJONZI, SIMANZI, HUZUNI
Rais JK akiuaga mwili wa Mh. Nyaulawa

MAMA SALMA AKIKUMBUKA ENZI ANANYONYESHA
MAJONZI, SIMANZI, HUZUNI
Mke wa Rais JK, Mama Salma Kikwete akiwa amembeba mjukuu wa marehemu Nyaulawa wakati ibada ikiendelea.

MUNGU ILAZE ROHO YA MAREHEMU PEMA PEPONI
MAJONZI, SIMANZI, HUZUNI
Rais JK na Mama Salma wakiwa pamoja waombolezaji wengine wakifuatilia ibada ya Mazishi, kulia mke wa Mh. Nyaulawa Bi. Getrude Nyaulawa.

BUNGE LIMEPOTEZA KIFAA MUHIMU
MAJONZI, SIMANZI, HUZUNI
Naibu Spika wa Bunge Mh, Anna Makinda naye akiuaga mwili wa Mh, Nyaulawa.

KAZA BUTI KIJANA
MAJONZI, SIMANZI, HUZUNI
Rais JK akimfariji mtoto mkubwa wa marehemu Nyaulawa aitwae Rehule ambaye ndiye Mkurugenzi wa kituo cha redio cha Times FM.
PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS /GPL
    (13 November 2008)
Views: 108 | Maoni (4) |
Back  <<  1 2 3 ... 85 86 87  >>  Next Page

Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

hit counter

 

2008 © globalpublisherstz.com