arrowMake Homepage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » photos

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Picha Ya Week ...

Nani Yupo / Alikuwepo

 


 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» JE, UNGEPENDA KUPATA RAFIKI ...
» MSHANGAO!
» Rais Kabila aomba wakafungw ...
» Waraka wa Papii watua kwa J ...
» Aunt Ezekiel alivyopigika k ...
» JERRY: NASAKWA NIUAWE!
» KIGOGO WA MURO NAYE KUKAMAT ...
» Mkanada wa Uwoya awaliz ...
» MAMA KUMBENA!
» MH. PINDA ATEMBELEA WAG ...
» BENZ LATUMBUKIA MTONI
» Vilio Mirerani
» Kukosa mwenzi wa maisha ...
» Mbinu za kumrudisha mw ...

 

RIDHIWANI AAPISHA MAKAMANDA WAPYA

photos  
MJUMBE wa Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) taifa, Ridhiwani Kikwete, jana aliwasimika makamanda wapya wanne wa UVCCM, Kata ya Kijitonyama katika mkutano wa hadhara uliofanyika shule ya Msingi Kijitonyama, jijini Dar es Salaam.

Makamanda walisimikwa katika mkutano huo ni Shyrose Banji, Tonny Ngombale Mwiru, Reule Nyaurawa pamoja na Philip Komanya.
RIDHIWANI AAPISHA MAKAMANDA WAPYA
Wanachama na mashabiki wa CCM wakijimwaya na burudani katika mkutano huo.

RIDHIWANI AAPISHA MAKAMANDA WAPYA
Mbunge wa Kinondoni, Idd Azzan mwenye shati la kijani (kulia) akikaribishwa katika hafla hiyo. Kushoto (aliyevaa sare ya CCM) ni Shyrose Banji, ambaye naye alisimikwa ukamanda wa UVCCM Kata ya Kijitonyama

RIDHIWANI AAPISHA MAKAMANDA WAPYA
Shyrose Banji akicheza ‘kiduku’ wakati wa kumsubiri mgeni rasmi.

RIDHIWANI AAPISHA MAKAMANDA WAPYA
Baada kuwasili, mgeni rasmi alizindua shina la CCM la wakereketwa la madereva wa teksi wa Kijitonyama.

RIDHIWANI AAPISHA MAKAMANDA WAPYA
Bendera ikipandishwa na mgeni wa heshima kuashiria kufunguliwa kwa tawi hilo.

RIDHIWANI AAPISHA MAKAMANDA WAPYA
Shyrose Banji akisimikwa ukamanda kwa kuvalishwa gwanda maalum la ukamanda.

RIDHIWANI AAPISHA MAKAMANDA WAPYA
Kamanda mpya, Tonny Ngombale Mwiru, akisimikwa kwa kuvishwa gwanda na kofia za chama chake...
    (11 March 2010)
Views: 0 | Maoni (0) | Picha Zaidi

 

TWANGA YAWAPA MOTISHA WANAMUZIKI WAKE

photos  
Katika kuwatia moyo wa kufanyakazi, uongozi wa ASET umeamua kuwa unatoa zawadi kwa wafanyakazi bora wa mwezi kwa wanamuziki wa bendi ya African Stars. Utaratibu huo ulianza rasmi usiku wa kuamkia leo pale Club Bilicanas ambapo Mpiga Drum mmoja, mwimbaji mmoja na mnenguaji mmoja waliibuka kidedea na kujinyakulia zawadi....Asha Baraka amesema kuwa utaratibu kama huu utakuwa ni kila mwezi....mtandao wako nao ulikuwepo kunakiri matukio hayo na mengine kama ifutavyo:

TWANGA YAWAPA MOTISHA WANAMUZIKI WAKE
Ankal Issa Michuzi akimzawadia Salehe Kupaza zawadi ya mfanyakazi bora wa mwezi kwa upande wa waimbaji wa bendi hiyo huku Da'Asha Baraka akishuhudia tukio hilolililojiri ndani ya Club Billicanas jijini Dar usiku wa kuamkia leo.

TWANGA YAWAPA MOTISHA WANAMUZIKI WAKE
Nyota wa filamu bongo, Steve Kanumba The Great (kulia) akimkabidhi zawadi ya mfanyakazi bora wa mwezi wa Twanga Pepeta upande wa wanenguaji, Asha Said 'Sharapova', huku Da'Asha Baraka na MC wa shoo hiyo Richard 'Big Brothe'r wakishuhudia.

TWANGA YAWAPA MOTISHA WANAMUZIKI WAKE
Meneja Mkuu na mwendeshaji wa mtandao wa Global Publishers Ltd, Abdallah Mrisho (kulia), akimkabidhi zawadi yake mpiga drums bora wa mwezi, James Kibosho, ambaye ni miongoni mwa vijana wadogo wa bendi hiyo. Kushoto anayeshuhudia ni Mkurugenzi wao, Asha Baraka

TWANGA YAWAPA MOTISHA WANAMUZIKI WAKE
..Asha Baraka akiongea machache huku akisiklizwa kwa makini na Kanumba pamoja na Richard 'wa Big Brother,

TWANGA YAWAPA MOTISHA WANAMUZIKI WAKE
Baada ya kutoonekana kwa muda mrefu, hatimaye jana Aisha Madinda (kulia) alipanda jukwaani katika onesho la Twanga Pepeta ndani ya Club Bilicanas usiku wa kuamkia leo.

TWANGA YAWAPA MOTISHA WANAMUZIKI WAKE
Aisha Madinda...alikuwa kivutio cha mashabiki katika safu nzima ya wanenguaji wa Twanga ukumbini humo.

PICHA: Mussa Mateja/GPL

    (11 March 2010)
Views: 0 | Maoni (0) |

 

THEA, MONALISA NANI ZAIDI?

photos  
Na Paparazi Wetu
Wiki hii katika Nani Zaidi wanaochuana ni mastaa wa kike katika Kiwanda cha Filamu Ndumbangwe Misaya a.k.a Thea na Ivony Cherly a.k.a Monalisa...

    (10 March 2010)
Views: 23 | Maoni (1) | Picha Zaidi

 

MKAPA ATOA POLE KWA BALOZI MSTAAFU DARAJA

photos  
MKAPA ATOA POLE KWA BALOZI  MSTAAFU DARAJA
Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, akishuka kwenye gari nyumbani kwa balozi mstaafu, Andrew Mhando Daraja, huko Kimara Temboni jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumpa pole kwa kufiwa na mkewe marehemu Bi Anna Daraja.

MKAPA ATOA POLE KWA BALOZI  MSTAAFU DARAJA
Mkapa akisalimiana na baadhi ya maofisa wastaafu majira ya saa 10 adhuhuri leo. Kushoto kwake, mwenye kandambili, ni Balozi Daraja aliyefiwa na mkewe.

MKAPA ATOA POLE KWA BALOZI  MSTAAFU DARAJA
Mkapa akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa balozi huyo.

MKAPA ATOA POLE KWA BALOZI  MSTAAFU DARAJA
Mkapa akiwa ameketi kwenye kochi na maofisa wengine waandamizi akipewa taarifa na balozi kuhusu msiba wa mkewe.

PICHA ZOTE na HARUNI SANCHAWA /GPL
    (10 March 2010)
Views: 110 | Maoni (2) |

 

TWANGA PEPETA WAKIWAJIBIKA MAZOEZINI

photos  
Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta International’ jana walinaswa na kamera yetu wakiwajibika vikali na mazoezi katika ofisi za bendi hiyo zilizopo Kinondoni Vijana jijini Dar es Salaam. Akiongea na mwanahabari wetu, Mkurugenzi wa Kampuni ya (ASET), Asha Baraka, alisema kuwa kutokana na ratiba yenye ‘pressure’ ameamua kuongeza muda wa mazoezi tofauti na walivyokuwa wakifanya siku za nyuma ambapo wanamuziki walitakiwa mazoezi kuanzia saa sita mchana na hadi saa kumi jioni, na sasa wanatakiwa kuanza mazoezi saa nne asubuhi hadi saa kumi na moja jioni.

TWANGA PEPETA WAKIWAJIBIKA MAZOEZINI
Baadhi ya wanenguaji wa Twanga Pepeta wakiwajibika mazoezini.

TWANGA PEPETA WAKIWAJIBIKA MAZOEZINI
Mpiga ‘drum’ wa bendi hiyo, James Kibosho, akiwa shughulini mazoezini. Aliyesimama ni mpiga tumba wa bendi hiyo ajulikanaye kwa jina la kisanii kama ‘MCD’ akiwa mazoezini.

TWANGA PEPETA WAKIWAJIBIKA MAZOEZINI
Joseph Shamba ‘Vengu’ (kushoto) akiwa na kiongozi wa African Stars ‘Twanga Pepeta’, Luiza Mbutu (katikati), na kulia ni mkurugenzi wa bendi hiyo, Asha Baraka.

TWANGA PEPETA WAKIWAJIBIKA MAZOEZINI
Mchekeshaji mahiri wa kundi la Orijino Komedi, Emmanuel Mgaya ‘Masanja’ (kushoto aliye na kamera) akijaribu kuwapiga picha wanamuziki wa bendi hiyo wakiwa mazoezini. Kulia kwake) ni Kalala Juniour, muimbaji wa bendi hiyo.

TWANGA PEPETA WAKIWAJIBIKA MAZOEZINI
Joseph Shamba ‘Vengu’ (aliyesimama) akiongea kwa msisitizo mkali na mataalam wa tiba za jadi maarufu kwa jina la Manyaunyau wakiwa katika Kinyaiya Pub iliyo karibu na ofisi za (ASET).

TWANGA PEPETA WAKIWAJIBIKA MAZOEZINI
Kalala Juniour akimlisha firigisi mchekeshaji ‘Vengu’ muda mfupi baada ya kupumzika mazoezi.

TWANGA PEPETA WAKIWAJIBIKA MAZOEZINI
Alex Chalamila ‘Mac Reagan’ akigandamiza kinanda katika shughuli hizo za kurekodi.


ORIJINO KOMEDI WAKIREKODI KIPINDI
KIKUNDI cha vichekesho cha Orijino Komedi kinachorushwa hewani kupitia luninga ya ‘TBC1’ jana kilinaswa na mpiga picha wetu kikirekodi kipindi ndani ofisi za ASET Kinondoni jijini Dar es Salaam.
TWANGA PEPETA WAKIWAJIBIKA MAZOEZINI
Isaya Mwakilasa ‘Wakuvanga’ akipiga gitaa na kuporomosha songi la nguvu wakati Emmanuel Mgaya ‘Masanja’ akiwa katika harakati za kurekodi kipindi hicho.

TWANGA PEPETA WAKIWAJIBIKA MAZOEZINI
Joseph Shamba ‘Vengu’ akiwa ‘siriazi’ na gitaa la bass katika moja ya shughuli za kuwezesha kipindi chao kwenda hewani vizuri.

TWANGA PEPETA WAKIWAJIBIKA MAZOEZINI
Mpiga picha wa kundi la Orijino Komedi aliyejitambulisha kwa jina moja la Kissoky, (kushoto) akiwa na ‘Masanja’ (katikati) na Rogert Hegga mwanamuziki ‘Twanga Pepeta’ ndani ya Kinyaiya Pub muda mfupi baada ya kutoka mazoezini.

PICHA:MUSA MATEJA /GPL
    (10 March 2010)
Views: 35 | Maoni (1) |

 

WATEJA WA ZANTEL ZANZIBAR KUNUFAIKA NA PROMOSHENI YA CHOMOKA NA VESPA

photos  
 WATEJA WA ZANTEL ZANZIBAR KUNUFAIKA NA PROMOSHENI YA CHOMOKA NA VESPA
Zantel imezindua promosheni ya CHOMOKA NA VESPA maalum kwa wakazi wa Zanzibar. Promosheni hii itawawezesha wateja wa zantel kisiwani humu kupata nafasi ya kujishindia pikipiki aina ya Vespa ambayo ni chombo maarufu sana cha usafiiri visiwani humo. Akizungumwa na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa promosheni hiyo, Meneja masoko wa kampuni ya Zantel Bw. William Mpinga alisema kwamba zawadi katika
    (10 March 2010)
Views: 26 | Maoni (0) | Picha Zaidi

 

TWIGA STARS WALIVYOPIGA BAO ETHIOPIA!

photos  
TWIGA STARS WALIVYOPIGA BAO ETHIOPIA!
Mchezaji wa Twiga stars akijaribu kumtoka mchezaji wa Ethiopia katika mechi iliyofanyika nchini humo mwishoni mwa wiki iliyopita

TWIGA STARS WALIVYOPIGA BAO ETHIOPIA!
Wachezaji wa twiga wakishangilia bao la ushindi

TWIGA STARS WALIVYOPIGA BAO ETHIOPIA!
Timu ya twiga na baadhi ya viongozi waliofuatana na timu hiyo wakiwa aktika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Balozi Mohamed Maundi.

PICHA: SALEH ALI_ETHIOPIA /GPL
    (9 March 2010)
Views: 8 | Maoni (0) |

 

BREAKING NEWS: NYUMBA YA MBUNGE YAUNGUA MOTO!

photos  
BREAKING NEWS: NYUMBA YA MBUNGE YAUNGUA MOTO!
Mbunge wa Lupa CCM wilayani Chunya, Victor Mwambalaswa

Nyumba ya Mheshimiwa Victor Mwamalaswa, Mbunge wa jimbo la Lupa, Chunya Mkoani Mbeya, imenusurika kuteketea kwa moto usiku huu baada ya Kikosi cha Zima Moto kufika mapema na kuudhibiti moto huo ambao chanzo chake hakikuweza kujulikana mara moja. Eneo la tukio, ambalo liko maeneo ya Kinondoni maeneo ya Leaders Club jirani na Ubalozi wa India, kulitawaliwa na majonzi na vilio kwa mama wa familia ambaye alikuwa akimshukuru Mungu kwa kumuepusha na janga hilo ambalo liliepushwa kwa kiasi kikiubwa na majirani wachahche waliokuwepo kwa kutoa msaada wa hapa na pale, ikiwemo kuwaita zimamoto...
BREAKING NEWS: NYUMBA YA MBUNGE YAUNGUA MOTO!
..sehemu ya ndani ya nyumba baada ya moto kuzimwa

BREAKING NEWS: NYUMBA YA MBUNGE YAUNGUA MOTO!
..faya wakiendelea kumwaga maji ili kuuzima kabisa moto huo

BREAKING NEWS: NYUMBA YA MBUNGE YAUNGUA MOTO!
..majirani wakimuangalia mama mwenye nyumba na mwanae wakilia kwa uchungu

BREAKING NEWS: NYUMBA YA MBUNGE YAUNGUA MOTO!
..faya wakiwa eneo la tukio

BREAKING NEWS: NYUMBA YA MBUNGE YAUNGUA MOTO!
..binti akimtuliza mama yake aliyekuwa akilia kwa uchungu. Moto huo ulitokea majira ya saa 2 usiku leo.

PICHA: Abdallah Mrisho/GPL
    (9 March 2010)
Views: 104 | Maoni (0) |

 

TANZANIA MUSIC AWARDS 2010 YAANIKA CATEGORY!

photos  
Kamati ya kuratibu tamasha la Tanzania Music Awards 2010 usiku huu imeweka hadharani categorie zitakazoshindaniwa mwaka huu na wasanii kupata wasaa wa kuvijadili, ingawa ushauri na mapendekezo yao mengi hayawezi kufanyiwa kazi kwa tunzo za mwaka huu bali mwakani. Tunzo za safari hii ziko jumla ya 22 ambazo ni: MWIMBAJI BORA WA KIKE. MWIMBAJI BORA WA KIUME. WIMBO BORA WA TAARAB. ALBAM BORA YA TAARAB. WIMBO BORA WA MWAKA. WIMBO BORA WA KISWAHILI (BENDI). ALBAMU BORA YA BENDI. WIMBO BORA WA R&B. WIMBO BORA WA ASILI YA KITANZANIA. WIMBO BORA WA HIP HOP. WIMBO BORA WA REGE. WIMBO BORA WA RAGA. RAPA BORA WA MWAKA (BENDI) MSANII BORA WA HIP HOP. WIMBO BORA WA AFRIKA MASHARIKI. MTUNZI BORA WA NYIMBO. MTAYARISHAJI BORA WA NYIMBO. VIDEO BORA YA MWAKA. WIMBO BORA WA AFRI POP. MSANII BORA ANAYECHIPUKIA. WIMBO BORA WA KUSHIRIKIANA.MDAU WA MUZIKI ALIYECHANGIA MAFANIKIO (HALL OF FAME).

Sura za wasanii wafuatao zimenaswa ndani ya kamera ya mtandao wako, ndani ya Paradise City Hotel Benjamin Mkapa Building, lililopo Mkabala na Posta mpya jijini Dar kama ifuatavyo:

TANZANIA MUSIC AWARDS 2010 YAANIKA CATEGORY!
Ndani ya ukumbi wa savanna semina ikiendelea

TANZANIA MUSIC AWARDS 2010 YAANIKA CATEGORY!
Meza ya waratibu ikijibu hoja za wasanii

TANZANIA MUSIC AWARDS 2010 YAANIKA CATEGORY!
Wahusika wakuu wakifuatilia semina hiyo: Kutoka kulia: Minja kutoka TBL, Mr. Malaba kutoka Basata, Kavishe kutoka TBL na Fina kutoka One Plus Comm.

TANZANIA MUSIC AWARDS 2010 YAANIKA CATEGORY!
Jay Moe na Lady Jaydee nao kama kawa..

TANZANIA MUSIC AWARDS 2010 YAANIKA CATEGORY!
..Ray C na wa ubani wake Lord Eyez nao hawakukosa

TANZANIA MUSIC AWARDS 2010 YAANIKA CATEGORY!
..K-sher (kulia) nae alikuwepo kuwakilisha

TANZANIA MUSIC AWARDS 2010 YAANIKA CATEGORY!
Hassan Bitchuka (kulia), Banza Stone (kushoto kabisa) nao walikuwepo

TANZANIA MUSIC AWARDS 2010 YAANIKA CATEGORY!
Waimbaji wakongwe nchini Mzee King Kikii na Swabah Salum mwimbaji hodari wa muziki wa Taarab.

TANZANIA MUSIC AWARDS 2010 YAANIKA CATEGORY!
MC wa shughuli..Masoud Kipanya

TANZANIA MUSIC AWARDS 2010 YAANIKA CATEGORY!
Wakali wa Hip Hop...AY (kushoto) na Mwana FA ndani ya nyumba

TANZANIA MUSIC AWARDS 2010 YAANIKA CATEGORY!
Wakali wa muziki wa Dansi Bongo...Jose Mara (kushoto), Khalid Chokoraa na Kalala Jr

TANZANIA MUSIC AWARDS 2010 YAANIKA CATEGORY!
..Mjomba Mrisho Mpoto akiwa na patna wake Afande Sele

TANZANIA MUSIC AWARDS 2010 YAANIKA CATEGORY!
Kundi la wateule Original..Mchizi Mox (kushoto) akifuatiwa na Jay Moe na Jafarai nao walikuwepo kutoa hoja..
PICHA: Abdallah Mrisho/GPL
    (9 March 2010)
Views: 5 | Maoni (0) |

 

HOMA YA UCHAGUZI

photos  
HOMA YA UCHAGUZI
Nguo zenye rangi, nembo na maneno yanayokisifia Chama Cha Mapinduzi zikiuzwa mitaani kama zilivyonaswa na kamera yetu. Katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi, nguo hizi huwa na wateja wengi.
    (9 March 2010)
Views: 19 | Maoni (1) |

 

WANAMUZIKI KUTOKA BRAZIL WAJA NA NGOMA ZA SAMBA BONGO

photos  
Wasanii wa muziki wa asili kutoka nchini Brazil, Bernado Aguiar (Pandeiro) na Gabriel Policarpo (Repique) wako nchini kwa ajili ya ziara ya kimuziki. Wasanii hao wataungana na wasanii wengine wa muziki wa asili kutoka hapa nchini, Ashimba wa Tabora na Carola Kinasha, ambapo kwa pamoja wanatarajia kufanya maonesho katika mikoa ya Arusha ( Maasai Camp), Mkoa wa Pwani, Bagamoyo na jijini Dar es Salaam katika kijiji cha Makumbusho kuanzia Machi 11 hadi Machi 19 mwaka huu.

WANAMUZIKI KUTOKA BRAZIL WAJA NA NGOMA ZA SAMBA BONGO
Kutoka kushoto ni: Ashimba kutoka Tanzania, Bernado Aguiar (Pandeiro) na Gabriel Policarpo (Repique) kutoka Brazil wakati wakitambulishwa kwa waandishi wa habari kwenye ukumbi wa habari Maelezo, leo asubuhi.

WANAMUZIKI KUTOKA BRAZIL WAJA NA NGOMA ZA SAMBA BONGO
Muunganiko wa Wabrazil na Watanzania wakionyesha ‘Free style’ kwa waandishi wa habari.

    (9 March 2010)
Views: 5 | Maoni (0) |

 

UKARABATI KATIKATI YA JIJI

photos  
Eneo la barabara katika mtaa wa Azikiwe, mkabala na Posta Mpya, katikati ya jiji la Dar es Salaam, linafanyiwa matengenezo kufuatiwa kuharibika. Eneo hili limekuwa na matatizo sugu ya mashimo na harufu mbaya inayosababishwa na kuziba kwa mifereji ya kupitishia maji machafu, hali ambayo imekuwa kero kubwa kwa wakazi wa jiji.
UKARABATI KATIKATI YA JIJI
Eneo linalofanyiwa matengenezo.

UKARABATI KATIKATI YA JIJI
Kibao kinachowatahadharisha madereva kuwa makini wanapopita eneo hilo.

    (9 March 2010)
Views: 9 | Maoni (0) |

 

KAHAWA NI SALAMA KWA AFYA YA BINADAMU

photos  
Mkurugenzi wa bodi ya kahawa nchini, Bwana Pius Ngeze kutoka Bukoba, amewataka Watanzania kujenga mazoea ya kunywa kahawa ili kuongeza soko la ndani la zao hilo linalolimwa kwa wingi katika mikoa ya Mbeya, Kilimanjaro na Kagera. Pia amewatoa hofu Watanzania kuwa wasitishwe na uzushi kwamba kahawa ina madhara kwa afya ya binadamu kwani kama ingekuwa hivyo, kahawa isingekuwa inanywewa dunia nzima.

KAHAWA NI SALAMA KWA AFYA YA BINADAMU
Bwana Pius Ngeze (katikati) akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa habari Maelezo, leo jijini Dar es Salaam.

    (9 March 2010)
Views: 9 | Maoni (1) |

 

TWANGA KUTANGAZA WANAMUZIKI BORA WA MWEZI FEBRUARI NDANI YA CLUB BILLICANAS‏

photos  

TWANGA KUTANGAZA WANAMUZIKI BORA WA MWEZI FEBRUARI NDANI YA CLUB BILLICANAS‏
...wanenguaji wa kike wa Twanga Pepeta wakiwa katika pozi.

Kampuni ya African Stars Entertainment kupitia band yake African Stars "TWANGA PEPETA" imeanzisha utaratibu wa kuchagua mwanamuziki bora wa kila mwezi ili kuongeza motisha na bidii ya kufanya kazi ndani ya band. Siku ya jumatano ndani ya ukumbi wa Club Billicanas.
    (9 March 2010)
Views: 8 | Maoni (1) |

 

Chuo Kikuu cha Arusha chapeperusha Bendera ya Tanzania Zain Africa Challenge

photos  

Chuo Kikuu cha Arusha chapeperusha Bendera ya Tanzania Zain  Africa Challenge
Wanafunzi wa chuo cha Arusha wakijiandaa kujibu maswali ya Zain Africa Challenge.

Chuo Kikuu cha Arusha, cha Tanzania ambacho ni chuo kikuu kichanga kimepeperusha bendera ya Taifa na kuitoa kimasomaso Tanzania katika mashindano yanayoendelea ya mtoano ya Zain Africa Challenge, chemsha bongo ya mtoano ya kimataifa ya Vyuo Vikuu...
    (9 March 2010)
Views: 201 | Maoni (0) | Picha Zaidi
Back  <<  1 2 3 ... 182 183 184  >>  Next Page

Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

hit counter

 

2008 © globalpublisherstz.com