MJUMBE wa Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) taifa, Ridhiwani Kikwete, jana aliwasimika makamanda wapya wanne wa UVCCM, Kata ya Kijitonyama katika mkutano wa hadhara uliofanyika shule ya Msingi Kijitonyama, jijini Dar es Salaam.
Makamanda walisimikwa katika mkutano huo ni Shyrose Banji, Tonny Ngombale Mwiru, Reule Nyaurawa pamoja na Philip Komanya.
Wanachama na mashabiki wa CCM wakijimwaya na burudani katika mkutano huo.
Mbunge wa Kinondoni, Idd Azzan mwenye shati la kijani (kulia) akikaribishwa katika hafla hiyo. Kushoto (aliyevaa sare ya CCM) ni Shyrose Banji, ambaye naye alisimikwa ukamanda wa UVCCM Kata ya Kijitonyama
Shyrose Banji akicheza ‘kiduku’ wakati wa kumsubiri mgeni rasmi.
Baada kuwasili, mgeni rasmi alizindua shina la CCM la wakereketwa la madereva wa teksi wa Kijitonyama.
Bendera ikipandishwa na mgeni wa heshima kuashiria kufunguliwa kwa tawi hilo.
Shyrose Banji akisimikwa ukamanda kwa kuvalishwa gwanda maalum la ukamanda.
Kamanda mpya, Tonny Ngombale Mwiru, akisimikwa kwa kuvishwa gwanda na kofia za chama chake...
Katika kuwatia moyo wa kufanyakazi, uongozi wa ASET umeamua kuwa unatoa zawadi kwa wafanyakazi bora wa mwezi kwa wanamuziki wa bendi ya African Stars. Utaratibu huo ulianza rasmi usiku wa kuamkia leo pale Club Bilicanas ambapo Mpiga Drum mmoja, mwimbaji mmoja na mnenguaji mmoja waliibuka kidedea na kujinyakulia zawadi....Asha Baraka amesema kuwa utaratibu kama huu utakuwa ni kila mwezi....mtandao wako nao ulikuwepo kunakiri matukio hayo na mengine kama ifutavyo:
Ankal Issa Michuzi akimzawadia Salehe Kupaza zawadi ya mfanyakazi bora wa mwezi kwa upande wa waimbaji wa bendi hiyo huku Da'Asha Baraka akishuhudia tukio hilolililojiri ndani ya Club Billicanas jijini Dar usiku wa kuamkia leo.
Nyota wa filamu bongo, Steve Kanumba The Great (kulia) akimkabidhi zawadi ya mfanyakazi bora wa mwezi wa Twanga Pepeta upande wa wanenguaji, Asha Said 'Sharapova', huku Da'Asha Baraka na MC wa shoo hiyo Richard 'Big Brothe'r wakishuhudia.
Meneja Mkuu na mwendeshaji wa mtandao wa Global Publishers Ltd, Abdallah Mrisho (kulia), akimkabidhi zawadi yake mpiga drums bora wa mwezi, James Kibosho, ambaye ni miongoni mwa vijana wadogo wa bendi hiyo. Kushoto anayeshuhudia ni Mkurugenzi wao, Asha Baraka
..Asha Baraka akiongea machache huku akisiklizwa kwa makini na Kanumba pamoja na Richard 'wa Big Brother,
Baada ya kutoonekana kwa muda mrefu, hatimaye jana Aisha Madinda (kulia) alipanda jukwaani katika onesho la Twanga Pepeta ndani ya Club Bilicanas usiku wa kuamkia leo.
Aisha Madinda...alikuwa kivutio cha mashabiki katika safu nzima ya wanenguaji wa Twanga ukumbini humo.
Na Paparazi Wetu Wiki hii katika Nani Zaidi wanaochuana ni mastaa wa kike katika Kiwanda cha Filamu Ndumbangwe Misaya a.k.a Thea na Ivony Cherly a.k.a Monalisa...
Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, akishuka kwenye gari nyumbani kwa balozi mstaafu, Andrew Mhando Daraja, huko Kimara Temboni jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumpa pole kwa kufiwa na mkewe marehemu Bi Anna Daraja.
Mkapa akisalimiana na baadhi ya maofisa wastaafu majira ya saa 10 adhuhuri leo. Kushoto kwake, mwenye kandambili, ni Balozi Daraja aliyefiwa na mkewe.
Mkapa akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa balozi huyo.
Mkapa akiwa ameketi kwenye kochi na maofisa wengine waandamizi akipewa taarifa na balozi kuhusu msiba wa mkewe.
Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta International’ jana walinaswa na kamera yetu wakiwajibika vikali na mazoezi katika ofisi za bendi hiyo zilizopo Kinondoni Vijana jijini Dar es Salaam. Akiongea na mwanahabari wetu, Mkurugenzi wa Kampuni ya (ASET), Asha Baraka, alisema kuwa kutokana na ratiba yenye ‘pressure’ ameamua kuongeza muda wa mazoezi tofauti na walivyokuwa wakifanya siku za nyuma ambapo wanamuziki walitakiwa mazoezi kuanzia saa sita mchana na hadi saa kumi jioni, na sasa wanatakiwa kuanza mazoezi saa nne asubuhi hadi saa kumi na moja jioni.
Baadhi ya wanenguaji wa Twanga Pepeta wakiwajibika mazoezini.
Mpiga ‘drum’ wa bendi hiyo, James Kibosho, akiwa shughulini mazoezini. Aliyesimama ni mpiga tumba wa bendi hiyo ajulikanaye kwa jina la kisanii kama ‘MCD’ akiwa mazoezini.
Joseph Shamba ‘Vengu’ (kushoto) akiwa na kiongozi wa African Stars ‘Twanga Pepeta’, Luiza Mbutu (katikati), na kulia ni mkurugenzi wa bendi hiyo, Asha Baraka.
Mchekeshaji mahiri wa kundi la Orijino Komedi, Emmanuel Mgaya ‘Masanja’ (kushoto aliye na kamera) akijaribu kuwapiga picha wanamuziki wa bendi hiyo wakiwa mazoezini. Kulia kwake) ni Kalala Juniour, muimbaji wa bendi hiyo.
Joseph Shamba ‘Vengu’ (aliyesimama) akiongea kwa msisitizo mkali na mataalam wa tiba za jadi maarufu kwa jina la Manyaunyau wakiwa katika Kinyaiya Pub iliyo karibu na ofisi za (ASET).
Kalala Juniour akimlisha firigisi mchekeshaji ‘Vengu’ muda mfupi baada ya kupumzika mazoezi.
Alex Chalamila ‘Mac Reagan’ akigandamiza kinanda katika shughuli hizo za kurekodi.
ORIJINO KOMEDI WAKIREKODI KIPINDI KIKUNDI cha vichekesho cha Orijino Komedi kinachorushwa hewani kupitia luninga ya ‘TBC1’ jana kilinaswa na mpiga picha wetu kikirekodi kipindi ndani ofisi za ASET Kinondoni jijini Dar es Salaam. Isaya Mwakilasa ‘Wakuvanga’ akipiga gitaa na kuporomosha songi la nguvu wakati Emmanuel Mgaya ‘Masanja’ akiwa katika harakati za kurekodi kipindi hicho.
Joseph Shamba ‘Vengu’ akiwa ‘siriazi’ na gitaa la bass katika moja ya shughuli za kuwezesha kipindi chao kwenda hewani vizuri.
Mpiga picha wa kundi la Orijino Komedi aliyejitambulisha kwa jina moja la Kissoky, (kushoto) akiwa na ‘Masanja’ (katikati) na Rogert Hegga mwanamuziki ‘Twanga Pepeta’ ndani ya Kinyaiya Pub muda mfupi baada ya kutoka mazoezini.
Zantel imezindua promosheni ya CHOMOKA NA VESPA maalum kwa wakazi wa Zanzibar. Promosheni hii itawawezesha wateja wa zantel kisiwani humu kupata nafasi ya kujishindia pikipiki aina ya Vespa ambayo ni chombo maarufu sana cha usafiiri visiwani humo. Akizungumwa na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa promosheni hiyo, Meneja masoko wa kampuni ya Zantel Bw. William Mpinga alisema kwamba zawadi katika
Mchezaji wa Twiga stars akijaribu kumtoka mchezaji wa Ethiopia katika mechi iliyofanyika nchini humo mwishoni mwa wiki iliyopita
Wachezaji wa twiga wakishangilia bao la ushindi
Timu ya twiga na baadhi ya viongozi waliofuatana na timu hiyo wakiwa aktika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Balozi Mohamed Maundi.
Mbunge wa Lupa CCM wilayani Chunya, Victor Mwambalaswa
Nyumba ya Mheshimiwa Victor Mwamalaswa, Mbunge wa jimbo la Lupa, Chunya Mkoani Mbeya, imenusurika kuteketea kwa moto usiku huu baada ya Kikosi cha Zima Moto kufika mapema na kuudhibiti moto huo ambao chanzo chake hakikuweza kujulikana mara moja. Eneo la tukio, ambalo liko maeneo ya Kinondoni maeneo ya Leaders Club jirani na Ubalozi wa India, kulitawaliwa na majonzi na vilio kwa mama wa familia ambaye alikuwa akimshukuru Mungu kwa kumuepusha na janga hilo ambalo liliepushwa kwa kiasi kikiubwa na majirani wachahche waliokuwepo kwa kutoa msaada wa hapa na pale, ikiwemo kuwaita zimamoto... ..sehemu ya ndani ya nyumba baada ya moto kuzimwa
..faya wakiendelea kumwaga maji ili kuuzima kabisa moto huo
..majirani wakimuangalia mama mwenye nyumba na mwanae wakilia kwa uchungu
..faya wakiwa eneo la tukio
..binti akimtuliza mama yake aliyekuwa akilia kwa uchungu. Moto huo ulitokea majira ya saa 2 usiku leo.
Kamati ya kuratibu tamasha la Tanzania Music Awards 2010 usiku huu imeweka hadharani categorie zitakazoshindaniwa mwaka huu na wasanii kupata wasaa wa kuvijadili, ingawa ushauri na mapendekezo yao mengi hayawezi kufanyiwa kazi kwa tunzo za mwaka huu bali mwakani. Tunzo za safari hii ziko jumla ya 22 ambazo ni: MWIMBAJI BORA WA KIKE. MWIMBAJI BORA WA KIUME. WIMBO BORA WA TAARAB. ALBAM BORA YA TAARAB. WIMBO BORA WA MWAKA. WIMBO BORA WA KISWAHILI (BENDI). ALBAMU BORA YA BENDI. WIMBO BORA WA R&B. WIMBO BORA WA ASILI YA KITANZANIA. WIMBO BORA WA HIP HOP. WIMBO BORA WA REGE. WIMBO BORA WA RAGA. RAPA BORA WA MWAKA (BENDI) MSANII BORA WA HIP HOP. WIMBO BORA WA AFRIKA MASHARIKI. MTUNZI BORA WA NYIMBO. MTAYARISHAJI BORA WA NYIMBO. VIDEO BORA YA MWAKA. WIMBO BORA WA AFRI POP. MSANII BORA ANAYECHIPUKIA. WIMBO BORA WA KUSHIRIKIANA.MDAU WA MUZIKI ALIYECHANGIA MAFANIKIO (HALL OF FAME).
Sura za wasanii wafuatao zimenaswa ndani ya kamera ya mtandao wako, ndani ya Paradise City Hotel Benjamin Mkapa Building, lililopo Mkabala na Posta mpya jijini Dar kama ifuatavyo:
Ndani ya ukumbi wa savanna semina ikiendelea
Meza ya waratibu ikijibu hoja za wasanii
Wahusika wakuu wakifuatilia semina hiyo: Kutoka kulia: Minja kutoka TBL, Mr. Malaba kutoka Basata, Kavishe kutoka TBL na Fina kutoka One Plus Comm.
Jay Moe na Lady Jaydee nao kama kawa..
..Ray C na wa ubani wake Lord Eyez nao hawakukosa
..K-sher (kulia) nae alikuwepo kuwakilisha
Hassan Bitchuka (kulia), Banza Stone (kushoto kabisa) nao walikuwepo
Waimbaji wakongwe nchini Mzee King Kikii na Swabah Salum mwimbaji hodari wa muziki wa Taarab.
MC wa shughuli..Masoud Kipanya
Wakali wa Hip Hop...AY (kushoto) na Mwana FA ndani ya nyumba
Wakali wa muziki wa Dansi Bongo...Jose Mara (kushoto), Khalid Chokoraa na Kalala Jr
..Mjomba Mrisho Mpoto akiwa na patna wake Afande Sele
Kundi la wateule Original..Mchizi Mox (kushoto) akifuatiwa na Jay Moe na Jafarai nao walikuwepo kutoa hoja.. PICHA: Abdallah Mrisho/GPL
Nguo zenye rangi, nembo na maneno yanayokisifia Chama Cha Mapinduzi zikiuzwa mitaani kama zilivyonaswa na kamera yetu. Katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi, nguo hizi huwa na wateja wengi.
Wasanii wa muziki wa asili kutoka nchini Brazil, Bernado Aguiar (Pandeiro) na Gabriel Policarpo (Repique) wako nchini kwa ajili ya ziara ya kimuziki. Wasanii hao wataungana na wasanii wengine wa muziki wa asili kutoka hapa nchini, Ashimba wa Tabora na Carola Kinasha, ambapo kwa pamoja wanatarajia kufanya maonesho katika mikoa ya Arusha ( Maasai Camp), Mkoa wa Pwani, Bagamoyo na jijini Dar es Salaam katika kijiji cha Makumbusho kuanzia Machi 11 hadi Machi 19 mwaka huu.
Kutoka kushoto ni: Ashimba kutoka Tanzania, Bernado Aguiar (Pandeiro) na Gabriel Policarpo (Repique) kutoka Brazil wakati wakitambulishwa kwa waandishi wa habari kwenye ukumbi wa habari Maelezo, leo asubuhi.
Muunganiko wa Wabrazil na Watanzania wakionyesha ‘Free style’ kwa waandishi wa habari.
Eneo la barabara katika mtaa wa Azikiwe, mkabala na Posta Mpya, katikati ya jiji la Dar es Salaam, linafanyiwa matengenezo kufuatiwa kuharibika. Eneo hili limekuwa na matatizo sugu ya mashimo na harufu mbaya inayosababishwa na kuziba kwa mifereji ya kupitishia maji machafu, hali ambayo imekuwa kero kubwa kwa wakazi wa jiji.
Eneo linalofanyiwa matengenezo.
Kibao kinachowatahadharisha madereva kuwa makini wanapopita eneo hilo.
Mkurugenzi wa bodi ya kahawa nchini, Bwana Pius Ngeze kutoka Bukoba, amewataka Watanzania kujenga mazoea ya kunywa kahawa ili kuongeza soko la ndani la zao hilo linalolimwa kwa wingi katika mikoa ya Mbeya, Kilimanjaro na Kagera. Pia amewatoa hofu Watanzania kuwa wasitishwe na uzushi kwamba kahawa ina madhara kwa afya ya binadamu kwani kama ingekuwa hivyo, kahawa isingekuwa inanywewa dunia nzima.
Bwana Pius Ngeze (katikati) akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa habari Maelezo, leo jijini Dar es Salaam.
...wanenguaji wa kike wa Twanga Pepeta wakiwa katika pozi.
Kampuni ya African Stars Entertainment kupitia band yake African Stars "TWANGA PEPETA" imeanzisha utaratibu wa kuchagua mwanamuziki bora wa kila mwezi ili kuongeza motisha na bidii ya kufanya kazi ndani ya band. Siku ya jumatano ndani ya ukumbi wa Club Billicanas.
Wanafunzi wa chuo cha Arusha wakijiandaa kujibu maswali ya Zain Africa Challenge.
Chuo Kikuu cha Arusha, cha Tanzania ambacho ni chuo kikuu kichanga kimepeperusha bendera ya Taifa na kuitoa kimasomaso Tanzania katika mashindano yanayoendelea ya mtoano ya Zain Africa Challenge, chemsha bongo ya mtoano ya kimataifa ya Vyuo Vikuu...