Ikiwa leo ni siku ya mwisho wa 2008 huku tukijiandaa kuukaribisha mwaka mpya, 2009, ndugu wawili, msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nakaaya Abraham Sumary ‘Mr. Politician’ na aliyekuwa Miss Tanzania 2005, Nancy Abraham Sumary wamedaiwa kuwa katika bifu zito ‘jino kwa jino’ kutokana na kutokuelewana kwao kwa mwaka mzima...
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete hivi karibuni amefanya kali ya mwaka na kuwashangaza wabongo baada ya kutinga katika studio za Kituo cha Televisheni cha TBC1 na kutangaza kipindi cha watoto...
Zikiwa zimesalia siku nne mwaka 2008 kumalizika, wale wanyange wawili waliodaiwa kuwa na bifu kwa kile kilichosemekana kuwa ni wivu wa mapenzi kwa msanii maarufu wa Filamu nchini, Wema Sepetu na Irene Uwoya wamefikia pabaya kutokana na sakata lao kuchukua sura mpya....
Katika hali inayoonekana kuwa ni kufuru kwa ‘bethidei’ ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo, Krismasi, watu wengi Jijini Dar es Salaam walisherehekea kwa kufanya vitendo vya laana ikiwa ni pamoja na ngono, kulewa kupita kiasi na kutwangana makonde kiasi cha kumwaga damu....
Sakata la mwanafunzi Mtanzania anayesoma chuo kimoja nchini Uganda kujipiga picha chafu kisha Boifrendi wake kuzisambaza mtandaoni baada ya kuzinasa limeingia sura ya pili kufuatia Mbunge aliyedaiwa ni baba wa denti huyo kujitokeza na kukanusha vikali...
Mrembo aliyewahi kuwa Miss Mbeya Mwaka 2002,Hellen Fotunatus hivi karibuni alinusurika kubakwa chooni ndani ya Ukumbi wa Msasani Club uliopo jijini Dar es Salaam...
Mfanyabiashara Ibrahim Gulamhussein Albhai juzi (Jumatatu), aliwasilisha hati ya kuiomba Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi kutoa amri ya kukamatwa kwa wadhamini wa mradi wa jengo la CCM, Plot 11, Block 53, Nyumba namba 107, Mtaa wa Sikukuu, Kariakoo, jijini Dar es Salaam...
Katika kuonesha kwamba Wanaume Halisi na Wanaume TMK wako pamoja, baadhi ya wasanii wa Kundi la Wanaume Halisi walitinga katika harusi ya Amani James Temba ‘Mheshimiwa Temba’ iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita ndani ya Ukumbi wa Princess, uliyopo Sinza, Dar es Salaam,...
Ule uchumba wa kukata na mundu ambao ulikuwa gumzo jijini Dar na pembezoni mwa nchi kati ya Meneja Uhusiano wa Benki ya NMB, Mwanaharakati wa masuala ya Kijamii, Shyrose Bhanji na mwanamuziki wa Kizazi Kipya, Jaffari Ali ‘Jafarai’ umekufa rasmi...
Mwanamuziki wa Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta,’ Kalala Junior anadaiwa kuhongwa gari na mrembo mmoja aliyetajwa kwa jina moja la Mary kwa kile kilichodaiwa na washambega kuwa ni kuchanganywa kimapenzi na mwanamuziki huyo...
Na Christopher Lissa Mawaziri wawili wa zamani , Basil Pesambili Mramba, aliyekuwa Waziri wa Fedha na Daniel Yona Waziri wa Nishati na Madini wanaokabiliwa na kesi za matumizi mabaya ya Ofisi na kulisababishia Taifa hasara ya zaidi ya Shilingi bilioni 11, huenda wakamtoa Lupango aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Grey Mgonja, ikiwa kesi zao zitaunganishwa...
Kundi la vichekesho nchini la Orijino Komedi wamemvaa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Ali Mohamed Shein baada ya kuvalia mavazi ya kike na kumvamia jukwaani huku wowowo la msanii Lukas Mhuvile ‘Joti, likisababisha watu kupiga kelele...
Imebainika kuwa mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Salma Kikwete, alimfundisha Elimu ya msingi mwanamuziki maarufu nchini, Judith Wambura 'Lady Jaydee' wakati 'first lady' huyo alipokuwa mwalimu katika Shule ya Msingi Mbuyuni, jijini Dar es Salaam...
Miss Ruvuma 2006, Isabela Mpanda amekiri kumuibia mzungu kiasi cha dola za kimarekani 1800, sawa na zaidi ya shilingi milioni 2 za kitanzania, kwa madai kuwa jamaa huyo hupenda kuwafanyia mchezo mchafu wasichana...
Msanii wa filamu nchini Aunt Ezekiel ambaye aliwahi kuwa mke wa Pedeshee Jack Pemba hivi karibuni alinaswa na kamera yetu akiwa amejiweka kwa kaka wa Mwanamuziki wa kizazi kipya Joseph Mbilinyi ‘Mr. ll’, aitwae Baraka Mbilinyi...