Nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kuniwezesha kuumaliza mwaka na kuingia mwingine kwa mafanikio mengi. Sina shaka kuwa wema wake ndio ulioniwezesha kupita vikwazo vingi vya kimaisha na hatimaye kuwa mmoja kati ya mamilioni ya waliosherehekea ujio wa mwaka 2009...
Wiki jana tulizungumzia adha ambazo wanawake huzipata kutoka kwa wanaume wanaowahi kufika kileleni mapema, lakini pia tuliona namna wanaume kwa upande wao wanavyokerwa na kasoro hiyo. Pamoja na hayo tuliona uwezekano wa mtu kujitibu mwenyewe tatizo hili kwa kutambua kanuni za kisaikolojia ambazo huchangia ufikaji kileleni mapema....
Miongoni mwa matatizo makubwa kabisa yanayowakabili wanaume katika suala la kujamiiana ni kufika kileleni mapema. Takwimu zisizo rasmi zinaonesha kuwa, wanaume saba kati ya kumi wana kasoro hii...
Mada hii tulianza kuitazama wiki jana, niwashukuru watu walionipigia simu kukiri kwamba wanakabiliwa na tabia ya kujichua. Namshukuru Mungu kuwa mafundisho yangu yamekuwa na msaada kwa watu wengi. Natiwa moyo ninaposikia watu wanasoma na kubadili maisha yao. Baada ya shukurani hiyo tuendelee na mada hii kutoka pale tulipoishia wiki jana. Matatizo haya ni kwa uchache, lakini yapo mengine ya kiafya, ambayo ni pamoja na kuumwa na kichwa, mgongo na kupoteza nguvu za mwili, hasa kwa wale wanaojichua kwa zaidi ya mara tatu kwa siku...
Punyeto au kwa Lugha ya Kiingereza Masturbation ni kitendo cha mwanaume kujisugua tupu yake na kutoa manii. Neno hili limetambulika na jamii mbalimbali miaka mingi iliyopita . Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa 2004 na Jarida la NOW la Tolonto, ilibainika kuwa, asilimia 81 ya wanaume huanza kufanya kitendo hicho wakiwa na umri wa miaka kati ya 10 na 15...
Naomba tuanze mada hii kwa kila mmoja wetu kujiuliza kwa nini tunapatwa na mambo mabaya katika maisha yetu ya kila siku, ndoa zinavunjika, ajali zinatokea, tunafilisika kibiashara, tunagombana, tunafeli mitihani au inakuwaje tunajikuta katika misukosuko ya kimaisha ambayo tulikuwa na njia ya kuepuka? Jibu ni kwasababu TUNAFANYA MAKOSA!...
Kupenda ni jambo muhimu katika maisha ya mwanadamu, kwa sababu asilimia kubwa ya matendo ya mtu huongozwa na mapenzi. Miongoni mwetu kuna watu wanapenda waume/wake zao, mali, watoto, magari vyakula, vinywaji, michezo na pengine aina fulani ya maisha...
Watu wengi hasa wasomi huamini kuwa ujinga ni mzigo wa binadamu wasiosoma (illiterate), lakini wenye elimu ya juu wakiwemo viongozi wa serikalini wao hawawezi kuwa wajinga....
Wiki iliyopita mpenzi msomaji wangu nilianza kukuletea mada iliyowagusa moja kwa moja wanafunzi iliyokuwa inaeleza sababu mbalimbali zinazowafanya wanafunzi wengi kufeli katika masomo yao. Wiki hii basi nitaimalizia mada hii ili wiki ijayo niweze kuanza mada nyingine kali...
Umasikini ni kikwazo kikubwa cha mafanikio ya wanafunzi kimasomo, lakini tunashauri kwamba kila mwanafunzi anayetoka katika familia masikini ajitambue na awe tayari kuishi sawa na kipato cha familia yake wakati akitafuta elimu...
Namshukuru Mungu kwa kunijalia afya ya kuweza kuendelea na somo hili wiki hii. Sina budi kuwashukuru wale wote walioguswa na somo hili kiasi cha kuahidi kuwatafuta watalaka wao na kuwaomba radhi.
Binafsi nimefurahiswa sana na wanawake walioahidi kutoa ushuda wao nawakaribisha. Baada ya utangulizi huu tuendelee toka tulipoishia wiki iliyopita?
Kumekuwa na ushahidi mwingi kutoka kwa wanaume ambao wamepatwa na mabaya muda mfupi baada ya kuachana na wake zao. Jamii na hata wanawake wenyewe wamekuwa hawafahamu ni nguvu gani ambayo huwashukia wanaume na kuwaporomosha kimaisha muda mfupi baada ya kuwapa talaka au kutengana na wake zao. Wengine wanasema ni laana, lakini wapo wanaopinga tena kwa ushahidi kabisa kwamba kuna wanawake waliachwa na hakuna matokeo mabaya kwa waume zao....
Anayebisha kauli hii asome historia za watu mbalimbali atagundua kuwa udanganyifu ni sumu kubwa ya maisha ya mwanadamu. Nawafahamu viongozi wakubwa wa dunia kama Richard Nixon wa Marekani na wengine walivyoporomoka baada ya kuuchafua uaminifu wao kwa jamii...