Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Mwandishi wa habari za uchunguzi na Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC 1), Jerry Muro amekoswakoswa kupigwa na kitu kinachoaminiwa kuwa ni risasi nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu alikokwenda kusikiliza kesi yake Ijumaa iliyopita...
Katika hali isiyotarajiwa na watu wengi, jiji la Dar es Salaam limegubikwa na hofu kubwa kutokana na baadhi ya watu kufiwa na ndugu zao vifo vya kutatanisha na kisha kuchukuliwa misukule na kwenda kuishi kusikojulikana huku wao wakiamini kuwa waliyemzika ni ndugu yao...
Siku chache baada ya Ofisa Msaidizi wa Propaganda wa Chama Cha Mapinduzi Richard Tambwe Hizza kutangaza nia ya kuwania Ubunge Jimbo la Temeke jijini Dar es Salaam, tetemeko la kisiasa limelikumba jimbo hilo...
Kufuatia mauaji ya mke wa Balozi Mstaafu, Andrew Daraja kilichotokea wiki iliyopita Kimara Temboni, jijini Dar es Salaam, marehemu Anna Daraja (pichani), mapya yaibuka ikiwa ni pamoja na raia wema kuamua kumtafuta muuaji huyo ambaye baada ya kufanya ukatili huo alitoroka...
Mchumba wa marehemu, Musa Juma anayedaiwa kuawa na polisi, Rehema Kipanda ametoboa siri kuwa mara baada ya kupata habari za kukamatwa kwa mumewe mtarajiwa alifika polisi kwa nia ya kutaka kumuona lakini akawekwa chini ya ulinzi kwa mahojiano...
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Samuel Sitta.
Nimesikia kwamba, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Samuel Sitta (pichani) na Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa wamepatanishwa, hii ni baada ya msuguano mkubwa uliolitikisa taifa mpaka baadhi ya mawaziri kuamua kuachia ngazi. Kinachotajwa kwenye mzozo ni vita ya ufisadi ambapo mpaka sasa raia wamebaki njia panda hawamjui nani fisadi...
Na Jumbe Ismailly,Singida Kituo cha afya cha Sokoine,kilichopo katika Manispaa ya Singida kinakabiliwa na tatizo la kuwa na mbu wengi nyakati za mchana,hali ambayo hutishia wagonjwa wanaolazwa kulazimika kukaa ndani ya vyandarua hata nyakati za mchana kwa kuhofia kuumwa na hatimaye kuambukizwa ugonjwa wa malaria. Malalamiko hayo yalitolewa na wagonjwa waliolazwa kwenye kituo hicho,kwa Naibu Waziri wa afya na Ustawi wa jamii,Dk.Aisha Omari Kigoda aliyetembelea kituo hicho na kuzungumza na wafanyakazi pamoja na akina mama wajawazito.
Aidha walisema akina mama hao kuwa ni jambo la kawaida kwenye kila nyumba au kituo cha afya kuwepo mbu nyakati za usiku,lakini kwenye kituo hicho ni kinyume kabisa kwani hulazimika kukaa ndani ya vyandarua hata nyakati za mchana.
“Tumekuwa tukikaa ndani ya vyandarua hivi hata mchana kutokana na kuogopa kuumwa na wa na ambao wanaweza kuwaambukiza malaria.
Richard Bukos na Kyalaa Seheye Baada ya uvumi wa kifo cha mwanasiasa mkongwe nchini, Maalim Seif Sharif Hamad (pichani chini) ikichukua sehemu kubwa ya mijadala mitaani na mitandaoni jana, hatimaye Uwazi limeweza kukusanya ukweli kamili. Jana, waandishi wetu walizungumza Maalim Seif ambaye alisema, “Sijafa na uvumi huo hata mimi nimeusikia...
Haruni Sanchawa na Makongoro Oging’ Katika hali ambayo siyo ya kawaida kwa jamii ya Watanzania hasa wacha Mungu, hivi karibuni katika Msikiti wa Ijumaa, Mwenge jijini Dar es Salaam, kijana aliyefahamika kwa jina la Kassim Abdallah (28), alifika msikitini hapo na kuuza picha za ngono zenye mchanganyiko na kwaya za dini pamoja na mauaji ambazo zimerekondiwa katika CD, wakati ‘kava’la juu likieleza ni picha za Safari ya Hija, kitendo kilichotafsiriwa na waumini kuwa ni kufuru kwa Mungu...
Kamanda mpya wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UV-CC), Bw. Deo Filikunjombe.
Na Francis Godwin, Ludewa SHEREHE za kusimikwa kwa Kamanda mpya wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UV-CC), Bw. Deo Filikunjombe zilitikisa mji wa Ludewa mkoani Iringa baada ya wana CCM kutoka kata zote 22 za wilaya hiyo kushiriki huku wakiwa na furaha kubwa...
Na Musa Mateja Harusi ya mtoto wa Waziri wa Ajira, Kazi na Maendeleo ya Vijana, Mhe. Juma Athuman Kapuya, MzuriKwao Kapuya na Bwana harusi, Salim Kabola imeibua mshangao mkubwa kufuatia nyomi ya ‘wakubwa’ kufurika katika sherehe hiyo na mambo kufanyika kinyume na matarajio ya wengi...
Na Joseph Ngilisho, Arusha Jeshi la Polisi mkoani Arusha, limeingia katika lawama na msuguano mkali na familia moja ya marehemu, Athuman Ramadhan (42) mkazi wa Mbauda, jijini Arusha, anayedaiwa kuuawa na askari baada ya kufanya mapenzi na changudoa mmoja kwenye nyumba ya kulala wageni ya Shauri Moyo iliyopo Matejoo...
Na Mwandishi Wetu, Bagamoyo UPEPO unaonekana kugeuka kufuatia kuwepo taarifa kuwa, yule kigogo ambaye hivi karibuni, alikuwa kwenye mtafaruku na Mtangazaji wa Shirika la Habari Tanzania, (TBC 1), Bw. Jerry Muro ...
Na Mwandishi Wetu MAUAJI makubwa yametokea usiku wa Jumatano iliyopita, huko Mbagala Kuu, jijini Dar es Salaam, ambapo watu watatu akiwemo muendesha pikipiki za kukodi, ...
Na Elvan Stambuli MGOGORO kati ya Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship linaloongozwa na Askofu Mkuu, Zachary Kakobe (pichani) na Shirika la Umeme nchini (Tanesco) unaosimamiwa na Waziri ...