arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » Vichekesho na Udaku

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» Mpenzi mwenye tabia hizi m ...
» (SIMULIZI ZA CHUMBANI) MDUA ...
» Mduara wa Mahaba (19)
» (SIMULIZI ZA CHUMBANI) MDUA ...
» Aisha Madinda: NGONO INANIU ...
» JACKLINE AMUANIKA ALIYEMTOA ...
» KANUMBA: NARGIS ALINITESA ...
» NI KIZIWI LAKINI KWA TA ...
» Mtoto wa Kigogo apiga p ...
» Jinsi ya kuonyesha na ...
» Unavyoweza kukabiliana ...
» KATANGULIA SISI TUPO NY ...
» Chenge amuweka Kikwete ...
» SHEREHE ZA MIAKA KUMI Y ...

 

Vunja mbavu

Vichekesho na Udaku  
Vunja mbavu
MTOTO AMUUMBUA MGONI WA BABA YAKE

Jamaa mmoja alikuwa anasafiri kwenda bara akitokea pwani. Baada ya safari ndefu akasikia hamu ya kuvuta sigara, basi akatoa sigara yake taratibu akaanza kuvuta huku basi likizidi kuvuta kasi. Kondakta wa basi alisikia ile harufu ya sigara akaenda kumkataza asiendelee kuvuta kwani kwenye basi si ruhusa kufanya hivyo.
Yule abiria alielewa kosa lake haraka na kuiminya sigara yake kisha akaiweka kwenye mfuko wa shati. Kumbe jamaa hakuizima vizuri ikaanza kuunguza shati na kutoa moshi.
Abiria mmoja aliyekuwa karibu aliona ile shati inatoa moshi akasema huku anaonyesha kwa kidole alipo yule jamaa, Inatoka moshi, inatoka moshi! Yule jamaa akajibu, haitoki Moshi hii baba inatoka Zanzibar na nimeinunua juzi tu...

    (25 December 2008)
Views: 204 | Maoni (3) | Soma Zaidi

 

Vunja mbavu

Vichekesho na Udaku  
Vunja mbavu
Ubishi wa mmakonde na mmasai

Mmasai na mmakondo walikuwa wakibisha na ilikuwa kama ifuatavyo:
Mmakonde: Chichi atuchemi bwana hata baba wa taifa alikuwa anajua.
Mmasai: Yero, inasema nini hii mutu, masai ni kiboko kwa kasi ya ulinsi.
Mmakonde: Chibaya chinajitembeza na chizuri chinajiuza.
Mmasai: Yeroo! Kinalinda na rungu tu si kinahatarisha maisha yake? Mmakonde: Ahaa! Nchakujua kumbe wewe unataka kujue chilaha zangu ili uje kuiba. Chacha chikwambii kama nina nchale wa chumu na nkuki, wewe njoo kuiba ndio utajiona chilaha zangu...
    (18 December 2008)
Views: 239 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

Vunja mbavu

Vichekesho na Udaku  
Vunja mbavu

KUOA MKE KWA RUNGU MBILI
Msela mmoja alikutana na rafiki yake wa damu huku akiwa mwenye furaha sana.Jamaa akamuuliza kulikoni siku hiyo kachangamka kupita maelezo na maongezi yakawa hivi:
Msela: Duh! Mwana nimepata mke kirahisi ile mbaya karibuni nitaoa.
Rafiki: Mahari ni bei gani mzee.
Msela:Nimeambiwa nipeleke rungu mbili tu sasa sijui nitazipata wapi hapa ndo naenda Mwenge kwa wauza vinyago wanipe rungu.
Rafiki: Rungu mbili ni hela, (laki mbili) we vipi sio upeleke rungu...
    (11 December 2008)
Views: 178 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

Vunja mbavu

Vichekesho na Udaku  
Vunja mbavu
Gauni lainii la Mwalimu
Mtoto mmoja aitwaye John alirudi shule uso wake ukiwa umevimba sana na mazungumzo kati ya mtoto huyo na baba yake yakawa hivi:
Baba: Mwanangu nini kimekupata, mbona uso wako umevimba hivyo?
Mtoto: Si lile gauni la mwalimu Sara
Baba: Limefanyaje?
Mtoto: Lilikuwa limeingia katikati ya makalio yake nikaenda kulichomoa ndio akanipiga kibao
Baba: Hiyo ni tabia mbaya usirudie tena mwanangu.
Kesho yake yule mtoto akarudi tena amevimba uso. Baba yake akamuuliza imekuwaje tena? Mtoto akajibu gauni ya ticha Sara iliingia tena katikati ya makalio yake, Tom akaitoa, nikaona ni tabia mbaya nikaenda kuirudishia. Baba akabaki ameduwaa...

    (4 December 2008)
Views: 289 | Maoni (2) | Soma Zaidi

 

Vunja mbavu

Vichekesho na Udaku  
Vunja mbavu
MTOTO KIKOJOZI
Mtoto mmoja alikuwa na tabia ya kukojoa kitandani kila siku na mama yake akaweka utaratibu kwamba kila akiamka kama mtoto huyo amekojoa anamchapa.
Basi siku moja mtoto huyo alikojoa mpaka akaloanisha shuka lote. Mama alipoamka kama kawaida siku hiyo alimchapa sana hadi yule mtoto akawa ameumia matakoni.
Usiku yule mtoto ambaye hulala chumba kimoja na wazazi wake, akakosa usingizi kabisa ndipo alipomsikia mama yake akimwambia baba yake akojoe.
Mtoto kusikia vile akainuka na kusema, hata sikubali, mimi nikikojoa unanichapa lakini baba unamwambia aachie kojo.
Duh! Mama kusikia vile alijisikia aibu na kuanzia siku hiyo mtoto akawa analala ‘sitting room’
    (20 November 2008)
Views: 265 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

Vunja mbavu

Vichekesho na Udaku  
Vunja mbavu

Vunja mbavu
Mwanamke mpenda rusha roho
Kuna mama mmoja alikuwa anapenda sana rusha roho. Siku moja kwake kulitokea msiba. Na nyumba ya jirani kukawa kuna rusha roho.
Sasa shughuli hizo zilitenganishwa na ukuta. Yule mama kote kote alikuwa anataka kuhudhuria.
Ikabidi atafute nyundo na kuutoboa ukuta na kupitisha kichwa chake. Sasa ilikuwa kichwa kipo upande wa msiba na kiwiliwili kwenye rusha roho. Usoni akawa analia na kiwiliwili kinakata mauno, ushawahi kuiona hiyo?
    (13 November 2008)
Views: 232 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

KATUNI

Vichekesho na Udaku  
KATUNI
    (12 November 2008)
Views: 49 | Maoni (0) |

 

VUNJA MBAVU!

Vichekesho na Udaku  
Kahaba lenye ujauzito
VUNJA MBAVU!
Changudoa mmoja aliyekubuhu katika biashara ya kuuza mwili alijikuta amenasa mimba, wakati yeye hakuhitaji kuzaa, akaamua kwenda hospitali kutoa, alipofika kwa daktari alikutana na maswali kadhaa ambayo alitakiwa kujibu kabla ya kutolewa ujauzito huo. Mazungumzo kati ya daktari na kahaba huyo yalikuwa hivi:
Daktari: Binti hivi unamjua aliyekupa mimba?
Changu: Kwani ukila maharage mengi tumbo likikuuma utatambua ni harage gani limesababisha wewe kudhurika?
Daktari kusikia vile hakutaka tena mazungumzo aliamua kumtoa nduki changudoa huyo.
    (6 November 2008)
Views: 372 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

KATUNI

Vichekesho na Udaku  
KATUNI
    (4 November 2008)
Views: 65 | Maoni (1) |

 

VUNJA MBAVU!

Vichekesho na Udaku  
Mambo ya menyu bwana!

VUNJA MBAVU!

Jamaa mmoja alitia fora katika hoteli moja ya kifahari ambapo alifika na kukuta Menyu ikisomeka, Kuku mzima 3000/= Jamaa alipoona vile fasta aliagiza ili aweze kujipoza, baada ya muda aliletewa huyo kuku aliyeagiza na mambo yakawa hivi.
Jamaa: Huyu ndiye kuku mzima?
Mhudumu: Ndiyo!
Jamaa: Shenzi taipu! Hivi unaweza kunitapeli mimi nimekuagiza kuku mzma mbona kichwa sikioni, utumbo je? Yaani hata miguu na shingo yake havipo....! utalipa mwenyewe. Wateja wote wakabaki mdomo wazi, jamaa huyoo!...


    (16 October 2008)
Views: 308 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

VUNJA MBAVU!

Vichekesho na Udaku  
VUNJA MBAVU!

Ubishoo mwingine ni soo!

Brothermen mmoja aliyekuwa akijifanya anajua ung?eng?e huku akijifanya yeye ni matawi ya juu alikwenda kupata msosi yeye na demu wake.Si unajua mabishoo kwa kupenda kujikweza? Basi demu akaagiza chipsi kuku jamaa akaagiza wali nyama.
Baada ya kumaliza wakaletewa bili yao ambayo ilikuwa ni sh, elfu (15,000). Kumbe jamaa mfukoni alikuwa na kiasi hicho hicho cha pesa, akalipa lakini kwa shingo upande huku akimuomba Mungu yule demu asijekuagiza kitu kingine maana ataumbuka.
Ile wanainuka tu demu si akamuomba mhudumu amletee ?tooth stick? za kuchokonolea meno ambazo hutolewa bure kwa mteja. Yule brothermen kusikia vile akaanza kuwaka akijua kwamba atatakiwa kulipa wakati hana kitu mfukoni na kuwaka akisema ?Sweet yaani unaagiza tena? Hizo ?tooth stick? utalipa mwenyewe? Demu kusikia vile akajua jamaa kumbe hakwenda hata darasa moja! Palepale kila mtu akashika njia yake....
    (2 October 2008)
Views: 473 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

Ndani ya 18 dimbani

Vichekesho na Udaku  
Ndani ya 18 dimbani
    (26 September 2008)
Views: 220 | Maoni (3) |

 

VUNJA MBAVU!

Vichekesho na Udaku  
VUNJA MBAVU!

Kasheshe la kopo la chooni


Kuna mshkaji mmoja alikuwa anatoka safari ghafla tumbo la kuhara likambana njiani.Alipofika nyumbani akafikia kuchukua kopo la chooni bila kujua kama zima au.
Alipolichukua akamimina maji kutoka kwenye ndoo na kuweka kwenye kopo. Kumbe kopo lile lilikuwa limetoboka. Alipofika chooni akavua nguo na kuanza kujisaidia. Mara akabaini kuwa kopo lile lilikuwa limetoboka na lilikuwa likivujisha maji.
Unajua alichokifanya? Jamaa fasta akachukua lile kopo na kuanza kujinawisha akihofia kwamba maji yangeisha na baada ya hapo akaendelea kujisaidia.

    (11 September 2008)
Views: 318 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

SASA TUNANYOLEA CHINI

Vichekesho na Udaku  
SASA TUNANYOLEA CHINI
Kuna mshikaji mmoja alikuwa kinyozi. Saluni yake ilikuwa katika ghorofa ya tatu. Kadiri siku zilivyokuwa zinakwenda wateja wakaanza kupungua na ikafika kipindi hakuna hata mtu anayekwenda kunyoa kwenye saluni yake hiyo.
Jamaa akajaribu kufanya utafiti na kwa mahesabu ya haraka haraka akaona huenda inatokana na saluni yake kuwa juu na kwamba watu wanaona uvivu kupandisha ngazi.
Basi siku moja akaamua kufanya utaratibu wa kuhamia ghorofa ya kwanza na mlangoni akaandika hivi; YULE KINYOZI ALIYEKUWA ANANYOA JUU, SASA HIVI ANANYOA CHINI KWA BEI NAFUU! Mpo hapoo?...
    (4 September 2008)
Views: 321 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

VUNJA MBAVU!

Vichekesho na Udaku  
VUNJA MBAVU!

Shuka nikumeze


Mama mmoja alikuwa akiishi ghorofani peke yake lakini alikuwa muoga sana. Siku moja asubuhi wakati anashuka kuelekea chini akasikia sauti ikisema, Shuka nikumeze! Shuka nikumeze!
Mh! Yule mama kusikia vile moyo ukaanza kumwenda mbio akijua kwamba kuna jitu kubwa ambalo ndilo linalomwambia hivyo na kwamba kweli akishuka litammeza.
Basi akaamua kupiga simu polisi ili waje wamsaidie. Haikupita muda polisi wakafika nyumbani kwa yule mama wakiwa wamejikoki vizuri huku wakiwa na silaha nzito.
Cha ajabu sasa walipofika wakakutana na kichaa mmoja mdogo kadhoofika akiwa amelala chini ya lile ghorofa, kamasi zikimtoka mithili ya dawa ya mswaki iliyominywa huku akiimba Shuka nikumeze! Shuka nikumeze, akimaanisha kamasi zishuke azimeze! Ukitaka cheka ukitaka nuna lakini habari ndio hiyo!




    (28 August 2008)
Views: 426 | Maoni (0) | Soma Zaidi
Back  <<  1 2 3 4 5 6 7 8  >>  Next Page
 

Kura Yako / Poll

Habari Katika Picha


Gazeti la Uwazi


Nani Yupo / Alikuwepo


Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

hit counter

 

2008 © globalpublisherstz.com