Pafri mmoja aliyekuwa na tabia ya kutembea na mke wa mtu kila mumewe alipokuwa kazini, siku moja siri ya uzinzi ilimfikia mwenye mali na kutakiwa arudi nyumbani ghafla. Jamaa alifanya hivyo na kukuta mlango umefungwa kwa ndani. Aligonga mkewe kwa woga wa kufumaniwa akachanganyikiwa, lakini Padri kwa kujiamini alivaa nguo na kujining’iniza dalini huku miguu ikionekana kwa chini. Jamaa alipoingia alianza kumshutumu mkewe; Jamaa: Nasikia unatembea na Padri?” Mke: Watu waongo mume wangu, huyo Padri yupo wapi?” Jamaa alianza kumtafuta kila kona lakini hakumuona alisahau kuangalia juu zaidi ya uvunguni na ndani ya kabati. Baada ya kuridhika kweli hakukuwa na mtu ndani, walikaa kitandani huku mkewe akiomba asiangalie juu. Padri aliyekuwa akining’inia juu ya kenchi mikono yake ilichoka na kujikuta akidondoka toka na kuanguka mbele ya yule mwanaume na mkewe. Wote walishtuka kumuona Padri, jamaa aliuliza; “Si huyu?” Padri: “Huyu nani, nimesikia mkiniteta kuwa natembea na mkeo, lakini kwa uwezo wa roho mtakatifu amenileta ndani mwako ili unithibitishie kuwa mimi natembea na mke wako” Jamaa alipoangalia juu hakuona sehemu yenye tundu alipopitia padri. Jamaa: “Umepitia wapi?” Padri: “Ni uwezo waroho mtakatifu aliyeniingiza kwa uwezo wake bila kuharibu bati wala kitu chochote” Jamaa: “Samahani baba Padri” Padri: “Nimekusamehe wewe na mkeo kwa kuwa hamkujua mtendalo” Jamaa: “Asante baba Padri walimwengu ni wagombanishi” Baada ya kusema hayo Padri alimfungulia mlango na kutoka huku mume akiamini kuwa ni kweli Padri kaletwa na roho mtakatifu. Kweli mjini shule.
NIMEWATOA NJE WAKACHEZE MPIRA Ndege moja iliyokuwa imepakiwa vichaa kufika angani walianza kucheza mpira kasoro kichaa mmoja alikuwa kimya amekaa kwenye siti akiwaangalia wenzake. Baada ya kuona kero zimezidi alifungua mlango wa ndege na kuwatoa nje wenzake naye akarudi kukaa. Rubani baada ya kuona vurugu zimetulia alijua vichaa wametulia baada ya kuchoka kucheza mpira. Ndege ilipofika alipokuwa akiwapeleka alishangaa kumkuta kichaa mmoja amekaa kwenye kiti. Rubani: Wenzako wako wapi? Kichaa: Walikuwa wakinisumbua niliwatoa nje wakacheze mpira wao Rubani alibakia kichwa wazi asijue atajibu nini.
ALIFANANISHWA NA MUNGU Kulikuwa na jamaa watatu kila mmoja alitoa sifa yake ya kufanana na mtu maarufu duniani. Wa 1, mimi wananifananisha na Idd Amini Kwa sababu gani? Kutokana na umbile langu refu na rangi yangu nyeusi watu wananifananisha na Marehemu Idd Amini dada. Wa pili: Mimi na Osama bin Laden Kwa sababu gani? Kutokana na weupe wangu na ndevu nyingi hata jina langu limekufa siku hizi naitwa Osama Wa tatu ambaye alikuwa na umbile dogo kuliko wote. Mimi nafanishwa na Mungu Watu wote walishtuka na kumuona yule jamaa kama anamkufuru Mungu lakini aliwathibitishia kweli kuna mtu alimfananisha na Mungu. Najua hamuwezi kuamini kama mjuavyo mimi mwenzenu mpenda ulabu na vifungu haviniishi, kila nilipopelekwa polisi nilihukumiwa na hakimu mmoja siku moja baada ya kupanda kizimbani hakunihukumu bali alinieleza kuwa ameniachia huru na nisirudie kufanya tena makosa. Lakini kwa bahati mbaya nilikamatwa na kupandishwa kizimbani, na hakimu alikuwa yule yule wakati napanda alikuwa ameinama akiandika ripoti baada ya kuandika aliponyanyua macho akaniona na kushtuka huku akisema. Mungu wangu umerudi tena Bado tu hamjaamini kuwa niliitwa Mungu, jamaa alibakia wakitazama kutokana na mwenzao kushindwa kumuelewa hakimu alikuwa na maana gani na si kumfananisha na Mungu.
NILIJIITA WAZIRI MKUU KIDOGO WANIUE Mkuu wa nchi moja alikwenda kutembelea hospitali ya wagonjwa wa akili ili kujua maendeleo na huduma wazipatazo, siku hiyo wendawazimu wenye kichaa kikali walifungiwa na kuachwa wenye nafuu. Basi Mkuu wa nchi alipofika hospitalini hapo alipokelewa na mganga Mkuu kisha alizungushwa katika wodi za wagonjwa wa akili.
Wodi ya kwanza ilikuwa ya igonjwa wenye afadhari ambao waliachwa ili kumpokea muheshimiwa hata kuzungumza nae mawili matatu. Mgonjwa wa kwanza aliyekutana naye alimuuliza mheshimiwa...