Tembelea... |
 |
Kalenda |
 |

Marafiki wetu |
 |
Habari Zilizopita |
 |



  
| |
 |
|
|
 |
 |
|
 |
MTOTO AMUUMBUA MGONI WA BABA YAKEJamaa mmoja alikuwa anasafiri kwenda bara akitokea pwani. Baada ya safari ndefu akasikia hamu ya kuvuta sigara, basi akatoa sigara yake taratibu akaanza kuvuta huku basi likizidi kuvuta kasi. Kondakta wa basi alisikia ile harufu ya sigara akaenda kumkataza asiendelee kuvuta kwani kwenye basi si ruhusa kufanya hivyo. Yule abiria alielewa kosa lake haraka na kuiminya sigara yake kisha akaiweka kwenye mfuko wa shati. Kumbe jamaa hakuizima vizuri ikaanza kuunguza shati na kutoa moshi. Abiria mmoja aliyekuwa karibu aliona ile shati inatoa moshi akasema huku anaonyesha kwa kidole alipo yule jamaa, Inatoka moshi, inatoka moshi! Yule jamaa akajibu, haitoki Moshi hii baba inatoka Zanzibar na nimeinunua juzi tu... |
|
 |
 |
|
 |
Ubishi wa mmakonde na mmasaiMmasai na mmakondo walikuwa wakibisha na ilikuwa kama ifuatavyo: Mmakonde: Chichi atuchemi bwana hata baba wa taifa alikuwa anajua. Mmasai: Yero, inasema nini hii mutu, masai ni kiboko kwa kasi ya ulinsi. Mmakonde: Chibaya chinajitembeza na chizuri chinajiuza. Mmasai: Yeroo! Kinalinda na rungu tu si kinahatarisha maisha yake? Mmakonde: Ahaa! Nchakujua kumbe wewe unataka kujue chilaha zangu ili uje kuiba. Chacha chikwambii kama nina nchale wa chumu na nkuki, wewe njoo kuiba ndio utajiona chilaha zangu... |
|
 |
 |
|
 |
KUOA MKE KWA RUNGU MBILI Msela mmoja alikutana na rafiki yake wa damu huku akiwa mwenye furaha sana.Jamaa akamuuliza kulikoni siku hiyo kachangamka kupita maelezo na maongezi yakawa hivi: Msela: Duh! Mwana nimepata mke kirahisi ile mbaya karibuni nitaoa. Rafiki: Mahari ni bei gani mzee. Msela:Nimeambiwa nipeleke rungu mbili tu sasa sijui nitazipata wapi hapa ndo naenda Mwenge kwa wauza vinyago wanipe rungu. Rafiki: Rungu mbili ni hela, (laki mbili) we vipi sio upeleke rungu... |
|
 |

 |
|
 |
Gauni lainii la Mwalimu Mtoto mmoja aitwaye John alirudi shule uso wake ukiwa umevimba sana na mazungumzo kati ya mtoto huyo na baba yake yakawa hivi: Baba: Mwanangu nini kimekupata, mbona uso wako umevimba hivyo? Mtoto: Si lile gauni la mwalimu Sara Baba: Limefanyaje? Mtoto: Lilikuwa limeingia katikati ya makalio yake nikaenda kulichomoa ndio akanipiga kibao Baba: Hiyo ni tabia mbaya usirudie tena mwanangu. Kesho yake yule mtoto akarudi tena amevimba uso. Baba yake akamuuliza imekuwaje tena? Mtoto akajibu gauni ya ticha Sara iliingia tena katikati ya makalio yake, Tom akaitoa, nikaona ni tabia mbaya nikaenda kuirudishia. Baba akabaki ameduwaa... |
|
 |
 |
|
 |
MTOTO KIKOJOZIMtoto mmoja alikuwa na tabia ya kukojoa kitandani kila siku na mama yake akaweka utaratibu kwamba kila akiamka kama mtoto huyo amekojoa anamchapa. Basi siku moja mtoto huyo alikojoa mpaka akaloanisha shuka lote. Mama alipoamka kama kawaida siku hiyo alimchapa sana hadi yule mtoto akawa ameumia matakoni. Usiku yule mtoto ambaye hulala chumba kimoja na wazazi wake, akakosa usingizi kabisa ndipo alipomsikia mama yake akimwambia baba yake akojoe. Mtoto kusikia vile akainuka na kusema, hata sikubali, mimi nikikojoa unanichapa lakini baba unamwambia aachie kojo. Duh! Mama kusikia vile alijisikia aibu na kuanzia siku hiyo mtoto akawa analala ‘sitting room’ |
|
 |
 |
|
 |
Kahaba lenye ujauzito
 Changudoa mmoja aliyekubuhu katika biashara ya kuuza mwili alijikuta amenasa mimba, wakati yeye hakuhitaji kuzaa, akaamua kwenda hospitali kutoa, alipofika kwa daktari alikutana na maswali kadhaa ambayo alitakiwa kujibu kabla ya kutolewa ujauzito huo. Mazungumzo kati ya daktari na kahaba huyo yalikuwa hivi: Daktari: Binti hivi unamjua aliyekupa mimba? Changu: Kwani ukila maharage mengi tumbo likikuuma utatambua ni harage gani limesababisha wewe kudhurika? Daktari kusikia vile hakutaka tena mazungumzo aliamua kumtoa nduki changudoa huyo. |
|
 |
 |
|
 |
Mambo ya menyu bwana!
 Jamaa mmoja alitia fora katika hoteli moja ya kifahari ambapo alifika na kukuta Menyu ikisomeka, Kuku mzima 3000/= Jamaa alipoona vile fasta aliagiza ili aweze kujipoza, baada ya muda aliletewa huyo kuku aliyeagiza na mambo yakawa hivi. Jamaa: Huyu ndiye kuku mzima? Mhudumu: Ndiyo! Jamaa: Shenzi taipu! Hivi unaweza kunitapeli mimi nimekuagiza kuku mzma mbona kichwa sikioni, utumbo je? Yaani hata miguu na shingo yake havipo....! utalipa mwenyewe. Wateja wote wakabaki mdomo wazi, jamaa huyoo!... |
|
 |
 |
|
 |
 Ubishoo mwingine ni soo! Brothermen mmoja aliyekuwa akijifanya anajua ung?eng?e huku akijifanya yeye ni matawi ya juu alikwenda kupata msosi yeye na demu wake.Si unajua mabishoo kwa kupenda kujikweza? Basi demu akaagiza chipsi kuku jamaa akaagiza wali nyama. Baada ya kumaliza wakaletewa bili yao ambayo ilikuwa ni sh, elfu (15,000). Kumbe jamaa mfukoni alikuwa na kiasi hicho hicho cha pesa, akalipa lakini kwa shingo upande huku akimuomba Mungu yule demu asijekuagiza kitu kingine maana ataumbuka. Ile wanainuka tu demu si akamuomba mhudumu amletee ?tooth stick? za kuchokonolea meno ambazo hutolewa bure kwa mteja. Yule brothermen kusikia vile akaanza kuwaka akijua kwamba atatakiwa kulipa wakati hana kitu mfukoni na kuwaka akisema ?Sweet yaani unaagiza tena? Hizo ?tooth stick? utalipa mwenyewe? Demu kusikia vile akajua jamaa kumbe hakwenda hata darasa moja! Palepale kila mtu akashika njia yake.... |
|
 |
 |
|
 |
 Kuna mshikaji mmoja alikuwa kinyozi. Saluni yake ilikuwa katika ghorofa ya tatu. Kadiri siku zilivyokuwa zinakwenda wateja wakaanza kupungua na ikafika kipindi hakuna hata mtu anayekwenda kunyoa kwenye saluni yake hiyo. Jamaa akajaribu kufanya utafiti na kwa mahesabu ya haraka haraka akaona huenda inatokana na saluni yake kuwa juu na kwamba watu wanaona uvivu kupandisha ngazi. Basi siku moja akaamua kufanya utaratibu wa kuhamia ghorofa ya kwanza na mlangoni akaandika hivi; YULE KINYOZI ALIYEKUWA ANANYOA JUU, SASA HIVI ANANYOA CHINI KWA BEI NAFUU! Mpo hapoo?... |
|
 |
|
|
 |
Kura Yako / Poll |
 |
Habari Katika Picha |
|
 |

Nani Yupo / Alikuwepo |
 |
|